EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 21, 2015

MCHUNGAJI ADAIWA KUTELEKEZA MKE

Mchungaji wa kanisa analosali msanii wa filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ na wenzake lililopo Sinza, Dar, Godwin Mwamposa amekanyaga skendo kufuatia madai ya kumtelekeza mkewe aitwaye Sylvia mwenye mtoto mmoja ambayo imetua kwenye dawati la gazeti hili.
Mchungaji Godwin Mwamposa na mkewe siku ya ndoa yao.
Ndugu wa Sylvia afunguka
Awali, ndugu aliyejitambulisha kuwa anaishi na Sylvia (jina tunalihifadhi kwa sababu maalum) alisema mke wa mchungaji huyo kwa sasa anaishi maisha magumu maeneo ya Buza jijini Dar baada ya kuachwa kwenye mataa na mwenza wake huyo.
“Yaani mpaka nimeamua kuwaambia hii habari nimeona ndugu yangu anateseka sana, tena na mtoto wake ambaye amekuwa akimuulizia baba yake kila siku.
“Mgogoro ulianza siku nyingi wakiwa Moshi (Kilimanjaro) ambapo Mchungaji Mwamposa alimwambia Sylvia wanakuja Dar kwa ajili ya kutoa huduma lakini walipofika alimpeleka kwa wazazi wake Buza (Dar) na kumuacha huko.“Kuna wakati wazazi wa Sylvia walimuita lakini alichenga kwenda, hali iliyosababisha sintofahamu kwa wanandugu.
“Sylvia analia kila siku, mara ya mwisho alipata presha ya kushuka na kulazwa Muhimbili (Hospitali ya Taifa) mpaka akawekewa mashine ya kupumulia kwani alikuwa na hali mbaya lakini pamoja na hilo bado mchungaji huyo hakusogea wala kuulizia hali yake,” alisema ndugu huyo.

Wakiwa na nyuso za furaha siku ya ndoa yao.
Ilidaiwa kwamba, kutokana na mazingira hayo, wanandoa hao waliofunga ndoa mwaka 2008 huko Kilimanjaro kwenye Kanisa la Calvary Assemblies of God, walikwenda kwenye usuluhishi katika makao makuu ya kanisa hilo yaliyopo Morogoro lakini mambo hayakuweza kutengamaa.
Mke atafutwa

Baada ya kupata habari hizo, mwandishi wetu alimtafuta Sylvia na kuzungumza naye juu ya madai hayo ya kutelekezwa ambapo alikiri kuwepo tatizo lakini akasema asingependa kuliongelea kwa sababu hakuwa na hali nzuri.
“Samahani sitaweza kulizungumzia sana suala hilo kwani sipo vizuri,” alisema Sylvia na kuomba apewe muda.
Mtoto wa mchungaji naye anenaBaada ya kuzungumza na Sylvia, mtoto wa mchungaji huyo aliyefahamika kwa jina la Angelprincess alizungumzia mazingira magumu anayoishi kutokana na kuwa mbali na baba yake.
“Natamani kumuona baba yangu, naishi mazingira magumu na mama yangu. Yaani siku nikimuona baba nitafurahi sana,” alisema mtoto huyo.Mchungaji Mwamposa anasemaje?

Hii ni shahada ya ndoa yao.
Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili, mchungaji Mwamposa alionesha kuwapo kwa tatizo kati yake na mkewe na akaeleza kuwa, suala lao lipo kwenye uongozi wa juu wa kanisa lake.
“Kama mnaweza kumsaidia msaidieni lakini suala hili lipo kwa uongozi wa juu wa kanisa na mkitaka zaidi mtafuteni wakili wangu muongee naye.”
Licha ya kiongozi huyo wa dini kumpatia mwandishi namba ya simu anayotumia mwanasheria huyo, ilipopigwa iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa na hata alipotumiwa meseji hakujibu hadi tunakwenda mtamboni.
Gazeti hili linaendelea kufuatilia habari hii kwa karibu na chochote kitakachopatikana, utakisoma kwenye Magazeti ya Global.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate