EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 21, 2015

MTOTO WA MIAKA 3 BONGO ANAYEFUNDISHA SEKONDARI


Stori: MWANDISHI WETU/Risasi
MTOTO Nice Valentino mwenye umri wa miaka mitatu na miezi tisa, ambaye ana vitu vingi vya kushangaza, ikiwemo kufundisha wanafunzi wa shule za sekondari, ameibuka ndani ya mjengo wa Global Publishers Ltd, Bamaga-Mwenge akiwa na baba yake mzazi na kuanika maajabu saba ya kushangaza, Risasi Jumamosi linakujuza.
Mtoto Nice Valentino akikokotoa maswali aliyopewa na waandishi.
AJABU LA KWANZA
Kwa mujibu wa baba mzazi wa mtoto huyo, Valentino Swenya, aliyezaliwa katika wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, Nice alianza kuandika maneno na namba za Kiingereza akiwa na umri wa miezi sita, jambo ambalo liliwashangaza sana.
AJABU LA PILI
Kadiri alivyokuwa akikua, ndivyo uwezo wake wa kuzungumza kiingereza ulivyozidi, lakini katika hali ya kushangaza, Nice hafahamu kabisa kuzungumza Kiswahili, lugha ya wazazi wake na anapolazimika kuongea, basi huongea kwa shida kama inavyowatokea wageni wanaojifunza lugha hiyo ya taifa.
AJABU LA TATU
Jambo lingine linalowashangaza watu ni juu ya uwezo wake wa kufanya hesabu ngumu, licha ya ukweli kwamba katika maisha yake, hajawahi kusoma hata shule za chekechea.“Kuna wakati niliwahi kumpeleka shule moja ya sekondari ya kata, akawafundisha wanafunzi kufanya hesabu ambazo wao zinawashinda, hebu fikiria hao watoto ni wa kidato cha tatu.

...Akiendelea kufanya swali alilopewa.
Na wakati mwingine wanafunzi wakipita nyumbani kwangu, ninawapa swali lililo sawa na kuwaambia wafanya pamoja, Nice anawahi kumaliza akiwa amepatia, lakini hao wanafunzi wa vidato vya juu wanachelewa huku wakiwa wamekosa,” anasema baba wa mtoto huyo ambaye ni mwalimu kitaaluma.
AJABU LA NNE
Kana kwamba haitoshi, mtoto Nice ana ujasiri wa hali ya juu mbele ya macho ya watu, kwani haogopi tofauti na walivyo watoto wengi wa umri wake. Akiwa katika chumba cha habari cha gazeti hili, mtoto huyo alikuwa akijibu maswali mbalimbali aliyoulizwa kwa ufasaha na bila kuogopa na hata wakati kundi kubwa la waandishi waliokuwa wakishangaa uwezo wake walipompigia makofi, hakuonyesha kuwajali.
Kitendo cha kuzungukwa na watu wazima zaidi ya 60 waliokuwa chumba cha habari na yeye kutoonyesha uoga, kinaashiria kuwa kijana huyo anao uwezo wa kuhutubia hata mkutano wa hadhara bila hofu.
AJABU LA TANO
Kitu kingine kilichowaacha watu hoi, ni maelezo ya baba yake kuwa kijana huyo uelewa wake ni wa hali ya juu, kwani mara kadhaa anapojaribu kumuelekeza kitu, yeye hufanya mara mbili au tatu zaidi.
Nice Valentino akiwa na babaa'ke.
“Kuna siku nilimfundisha kuandika namba hadi nikafikia laki moja kwa tarakimu. Cha kushangaza, yeye aliweza kuniandikia tarakimu za milioni moja na kuitamka bila wasiwasi,” alisema.
AJABU LA SITA
Jambo lingine linalomtofautisha kijana huyo na hali ya kawaida, ni kitendo chake cha kuwa na uwezo wa kusoma maandishi yaliyoandikwa kwa lugha ya kiingereza tu, lakini hawezi kabisa kusoma maandishi ya Kiswahili au lugha nyingine yoyote.
“Anajua kusoma kwa ufasaha kabisa maneno yote ya kiingereza, jambo hili linatushangaza sana na hata anapozungumza, anajua vema kuhusu wakati uliopo, uliopita na hata ujao (tenses), lakini kama ukimwandikia kiswahili, anasoma kama Wahindi wanavyosomaga,” anasema baba yake.

...Akipozi.
AJABU LA SABA
Waandishi wetu walimuuliza kama anamfahamu msanii Diamond Platnumz, alisema hamjui, lakini alipoulizwa kama anajua kuimba wimbo wowote, aliimba wimbo wa dini (Gospel) kwa lugha ya kiingereza uitwao Glory to the Lord ulioimbwa na mwanamuziki aliyezaliwa mwaka 1950, Mmarekani Donald James ‘Don Moen’ unaomaanisha Utukufu kwa Bwana.
Ili kumsikia na kumuona mtoto huyo laivu akikokotoa mahesabu sambamba na mahojiano yote akiwa chumba cha habari, tembelea tovuti ya www.globatvtz.com

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate