EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 13, 2015

MCHUNGAJI AMWITA JIDE AMUOMBEE!

Imelda Mtema/Ijumaa
SIKU moja tu baada ya mwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ kutupia kwenye mtandao wa Instagram, Jumanne iliyopita akisema baadhi ya watu wanamsakama kuhusu kutozaa bora auawe, mchungaji ameibuka na kumtaka staa huyo kufika kanisani kwake ili amwombee.

Mwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’.
Mchungaji Overcomer Daniel wa Kanisa la Mlima wa Makimbilio, Boko, Dar es Salaam ndiye aliyemtaka staa huyo akisema tatizo lake la kutopata mtoto analijua kwa vile linawakabili wanawake wengi kwa sasa.

JIDE aliandika hivi
Hivi watu hamuelewi Kiswahili au ni nini??? Nimesema tumbo limevimba sababu ya sahani, nikimaanisha mlo na niliposti nakula hapo awali.Sasa hapo maneno mengine yanatokea wapi? Au niwe naandika Kichina? Kwani mliambiwa nitazaa rais atakayewatoa kwenye shida zote mpaka mnishikilie mimba mimba...Hebu niacheni basi, khaa! Nisiishi kisa mimba? Basi niueni kisa sizai....

KOANZIA
Baada ya kupata ujumbe wa Jide kupitia mtandao huo huku pia akiwa ameshasoma habari zake muda mrefu kuhusu kutopata mtoto kwenye ndoa yake, Mchungaji Overcomer alipiga simu chumba cha habari cha Magazeti Pendwa ya Global Publishers na kuongea na Mhariri Kiongozi wa magazeti hayo, Oscar Ndauka.

Baada ya salamu, akasema: “Mimi ni Mchungaji wa Kanisa la Mlima wa Makimbilio, lipo Boko. Aaa! Naitwa Overcomer Daniel. Nina ibada ya kuwaombea watu mbalimbali wenye mahitaji ambayo kwao ni mlima.
“Sasa nimeona mwanamuziki Lady Jaydee anazungumzia suala la kukosa mtoto. Hapa kwetu Mungu anatenda. Si kwa Jide tu, kwa mtu yeyote, awe mwanamuziki, mcheza mpira, mama wa nyumbani, baba wa kawaida, mwanafunzi, yaani mtu yeyote yule, namkaribisha kuja kumwombea kwa matatizo aliyonayo.
“Naamini watabarikiwa na matatizo yao yatapata ufumbuzi kwa muujiza wa Mungu aliye hai,” alisema mchungaji huyo.
WANAWAKE KUKOSA KUZAA
Mchungaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, wanawake kukosa kushika mimba si suala la miaka hii. Tangu zamani zile, ilikuwa hivyo.“Mfano, mke wa Ibrahim (Abrahamu), Sara (Sarai) naye alikuwa hashiki ujauzito tangu ameolewa. Lakini akiwa na umri wa miaka karibia themanini, Mungu alimwonesha kwamba hata katika umri huo, mwanamke anaweza kutendewa muujiza akapata mtoto (Mwanzo 21:1-2).

Aliyekuwa mume wa Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ Gardner G. Habash.
“Sara alipata ujauzito akamzaa Isaka. Sasa baadhi ya binadamu wa leo wanapokuwa katika hali hiyo wanakata tamaa mapema. Ndiyo maana nawaita wote wenye shida hiyo na nyingine waje Mlima wa Makimbilio,” alisema Mchungaji Overcomer.

IJUMAA LAMSAKA JIDE
Baada ya ujumbe wa mchungaji huyo, Ijumaa lilimtuma paparazi wake kumtafuta Jide ili kumpa mwaliko huo.Jide hakupatikana kwenye simu yake ya mkononi baada ya namba zake kuwa za tabu kupatikana. Hata hivyo, Ijumaa lilifika nyumbani kwake, Kimara Temboni, Dar ambako hivi karibuni ilidaiwa amerudi kuishi hapo.


NYUMBA YA JIDE TUPU
Ijumaa liliikuta nyumba hiyo ikiwa na dalili zote za kutoishi watu kutokana na mazingira ya nje. Baadhi ya majirani walisema hakuna binadamu yeyote anayeishi ndani ya nyumba hiyo kwa sasa.
“Jide hakai hapa. Siku nyingi hatujamuona. Lakini pia mnavyoona kwa nje, nyumba hii hakai mtu. Kuhusu hiyo namba yake, sisi majirani hatuna,” alisema jirani mmoja aliyekataa kujitambulisha kwa jina.


IJUMAA LAMSAKA GARDNER
Baada ya kutoka Kimara, Ijumaa lilimsaka ‘mtalaka’  wa Jide, Gardner G. Habash ambapo mazungumzo yake na gazeti hili yalikuwa hivi:
Ijumaa: “Habari za kazi?”
Gardner: “Njema.”

Ijumaa: “Samahani sana, nawezaje kupata namba za simu za Jide?”
Gardner: “Mh! Kwa kweli siwezi kukupatia kwa sababu mwenyewe hataki kabisa. Sasa kwa sababu hataki, kukupa namba yake ni sawa na kumsaliti.”   

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate