EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, April 23, 2015

BASATA WAMPONGEZA MAYUNGA KWA KUWAKILISHA VYEMA TANZANIA‏


Mkurugenzi Ukuzaji Sanaa na Masoko Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Vivian Msao Shalua (kulia)akipokea tuzo aliyoipata Nalimi Mayunga mara baada ya kuibuka  mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Afrika.  Shughuli hii imefanyika jana katika halfa ya kumpongeza  Mayunga kwa kuiwakilisha vyema Tanzania katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars iliyofanyika  katika ofisi za BASATA. Akishuhudia  kushoto ni meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando
Mkurugenzi Ukuzaji Sanaa na Masoko Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Vivian Msao Shalua (Katikati) akiongea katika halfa ya kumpongeza mwakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya Airtel Trace Music Stars Afrika kwa kuibuka mshindi wa mashindano hayo na kuiwakilisha vyema Tanzania . halfa hiyo ilifanyika katika ofisi za BASATA Ilala Dar es Saalam. kushoto ni meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando
Baraza la sanaa Tanzania BASATA leo limempongeza mwakiliwa wa Tanzania katika mashindano ya Airtel Trace kufatia ushindi alioupata katika mashindano ya muziki yaliyoshirikisha washiriki 13 toka nchi za Afrika .
Mwisho mwa mwezi wa tatu BASATA ilimkabidh bendera Mayunga na kumpa kibali cha kwenda kushiriki mashindano hayo yaliyokuwa yanafanyika nchini Kenya  na kumtakia kila  laheri katika mashindano hayo ambapo mwakilishi huyu aliweza kufanya vizuri na kuibuka kuwa mshindi wa Airtel Trace Music Star wa Afrika
Mkurugenzi Ukuzaji Sanaa na Masoko Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Vivian Msao Shalua katika halfa fupi ya pongezi kwa Nalimi Mayunga katika ofisi za BASATA alisema”  Ushindi huu ni  furaha kubwa kwetu sisi Baraza la Sanaa la Tanzania kwani tunayo dhamana ya kuhakikisha tunaendeleza sanaa nchini  kwa tunashirikiana na wadau mbalimbali nchini katika kuwawezesha   vijana wenye vipaji kukuza sanaa zao ndani na nje ya nchi.
Nachukua fulsa hii kwa niaba ya BASATA kumpongeza Mwakilishi wetu Nalimi Mayunga kwa kufanya vizuri na kushinda mashindano haya. 
Nawashukuru sana Airtel kwa kufata taratibu stahiki na kushirikisha BASATA tangu mashindano haya yaanze ikiwa ni kusajili  kampuni yao na kupata hati ya kufanya shughuli za sanaa na pia kutushirikisha katika mchakato mzima wa mashindano haya na kumleta mshindi huyu kuchukua hati maalumu ya kusafiri na kuagwa rasmi wakati wa kuondoka kwenda kwenye mashindano ya Afrika.  Kwakweli huu ni mfano wa kuigwa na wadau wengi na wasanii kwa ujumla, kufata taratibu na kupata vibali maalumu pindi wanapoenda nje ya nchi kufanya shughuli za sanaa na kuwakilsisha nchi yetu.
Natoa wito kwa watanzania kujitokeza kwa wingi pindi awamu ya msimu wa pili wa mashindano haya ya Airtel Trace yatakapotangazwa ili nao waweze kupata nafasi ya kushiriki na kuinua vipaji vyao. Aliongea Shalua
Akiongea kwa niaba ya Airtel Meneja Uhusiano wa Airtel  Bw Jackson Mmbando alisema  Tunawashukuru watanzania wote walioshiriki katika shindano hili  tangu tulipolizindua.  tunampongeza sana mayunga kwa ushindi huu. Nalimi Mayunga ameweza kujishindia dili la kwenda marekani na kupata mafunzo chini ya usimamizi wa Akon,na pia kuweza kurekodi wimbo na video yake ya kwanza vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya dola za kimarekai 500,000/= Tunategemea baada ya mafunzo hayo na kutoa wimbo wake na Akon basi mayunga ataendelea kufanya vizuri na hatimae kuweza kuzifikia ndoto zake.
Airtel ilimkabithi Mayunga zawadi ya shilingi million 50 za kitanzania kufatia ushindi wake hapa nchini  na sasa anajiandaa kwenda marekani na kufanya kazi na msaani nguli Akon.
Akiongelea ushindi wake Mayunga alisema, nawashukuru sana watanzania kwa kunipigia kura toka mashindano haya yaanze, najisikia furaha kupata nafasi hii ya pekee na naamini safari yangu nchini marekani itakuwa ya mafanikio makubwa na mwanzo wa mafanikio katika kuzifika ndoto zangu za kuwa mwanamuziki nyota ndani na nje ya nchi.
Nawashukuru Airtel  kwa kuanzisha mashindano haya na BASATA kwa kunipa ushirikiano wakati wote wa mashindano. Natoa wito kwa watanzania na vijana wenzangu kuchangamkia fulsa hii pindi msimu wa pili wa mashindano haya yatakapotangazwa na kuanza .
Mashindano ya Afrika yalimalizika  kwa mtanzania kushika nafasi ya kwanza , Nigeria nafasi ya pili  na Congo Brazavile nafasi ya tatu.
 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate