MSANII mkongwe kwenye gemu la filamu Bongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’
amefunguka kwamba siyo mgumba wala hana gundu ila ni muda tu haujafika
wa kuzaa au kuolewa.

Maya
aliyasema hayo kutokana na maneno ya watu wanaomuandama kwamba hazai na
ana gundu ndiyo maana haolewi ambapo alisema siyo kweli ila anasubiri
wakati ukifika atazaa kwani ana uzazi na hajawahi kutafuta mtoto na
kumkosa.
“Bado sijapata mwanaume wa kunioa na sina gundu, kuzaa bado wakati
haujafika ila ukifika naamini Mungu atanipatia maana mayai ya uzazi
ninayo ya kutosha,” alisema Maya.
No comments:
Post a Comment