EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, April 20, 2015

LULU APATA KASHFA MPYA!

Waandishi wetu
WAKATI mwili wa bilionea Lusekelo Samson Mwandenga ‘Seki’ aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita ukitarajiwa kuzikwa leo mjini Dodoma, mitandao mbalimbali ya kijamii imempa kashfa staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa kumtaja kuwa alikuwa na uhusiano wa ‘kimalovee’ na marehemu huyo, Ijumaa Wikienda linakujuza.
Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Seki ambaye alikuwa na urafiki mkubwa na mastaa mbalimbali wa Bongo Movies, alifariki dunia baada ya kuanguka nyumbani kwake Madale jijini Dar ikidaiwa kuwa alikuwa akitaka kumuokoa mwanaye aliyekuwa akianguka ndipo yeye akaangukia meza ya kioo na kumchana tumboni.
ALIKUFA AKIKIMBIZWA HOSPITALI
Hata hivyo, wakati akikimbizwa hospitalini jijini Dar, alivuja damu nyingi hali ambayo ilimsababishia umauti kabla ya kupatiwa huduma ya kwanza.

LULU AANZA KUTAJWA
Saa chache baada ya kifo hicho kutokea, mitandao tofauti ya kijamii ilianza kumtaja Lulu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na bilionea huyo kwa kumpa pole pasipo kuwa na uhakika kama ni kweli au la!
“Mh! Pole Lulu kwa kufiwa na mtu wako, jamani huyu mtoto ana bahati mbaya sana sijui ni nini,” alichangia mdau mmoja katika mtandao wa Instagram.
POLE ZAZIDI KUMIMINIKA
Kadiri muda ulivyozidi kwenda ndivyo wafuasi wengi wa mitandao ya kijamii walivyozidi kummwagia pole nyingi Lulu huku wengine wakikemea suala la kumhusisha Lulu na bilionea huyo bila kuwa na ushahidi.“Jamani mna uhakika gani kama Lulu na huyo marehemu walikuwa na uhusiano? Mnamchafua bure mtoto wa watu,” alichangia mdau mmoja mtandaoni.
LULU AJIONDOA INSTAGRAM
Wakati watu wakiendelea kumhusisha kimapenzi na bilionea huyo kwa namna tofauti mtandaoni, ghafla Lulu alifuta akaunti yake ya Istagram hivyo kuwafanya wafuasi wa mtandao huo kushindwa kuona mwigizaji huyo ametoa tamko gani kuhusiana na kifo hicho.
Marehemu Lusekelo Samson Mwandenga ‘Seki’ enzi za uhai.
BETHIDEI YA LULU YAYEYUKA
Kama hiyo haitoshi, siku hiyo ya msiba (Alhamisi), Lulu alikuwa akiadhimisha sherehe ya kuzaliwa kwake ambapo angetimiza miaka 20 lakini kutokana na sababu ambazo hazikuweza kufahamika mara moja, hakufanya sherehe hiyo.
LULU ANASEMAJE?
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Lulu kwa njia ya simu kutaka kujua taarifa za yeye kuhusishwa na bilionea huyo pamoja na mambo mengine, Lulu alijibu kwa kifupi:Ijumaa Wikienda: “Lulu kwanza tumesikia unaumwa na umelazwa, ni kweli?”
Lulu: “Siyo kweli, mimi mbona nipo tu hapa nyumbani.”
Ijumaa Wikienda: “Kuna manenomaneno kuhusu kifo cha Seki, watu wanakusema vibaya mitandaoni. Je, unatoa tamkoa gani?”Lulu: “Sina tamko lolote.”
Ijumaa Wikienda: “Lakini ni mtu uliyekuwa unamfahamu au alikuwa mpenzi wako?”
Lulu: “Sina cha kusema mimi na sina tamko lolote.”Ijumaa Wikienda lilipojaribu kumbana kwa maswali zaidi kuhusiana kuwa na uhusiano na bilionea huyo, kutofanyika kwa bethidei yake na kufuta akaunti ya Instagram, Lulu hakuwa tayari kujibu lolote.
Marehemu Seki ambaye alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa madini, Arusha na Dar ameacha mke na watoto wawili.
Mwili wake ulitarajiwa kuagwa jana katika Kanisa la KKT, Wazo-Hill jijini Dar na kusafirishwa mjini Dodoma kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika leo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate