EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 7, 2015

MAUAJI YA POLISI 2 MKOA WA PWANI UGAIDI UGAIDI


Makongoro Oging’ na Issa Mnally
HUKU watu wakisherehekea Sikukuu ya Pasaka kwa vifijo, shangwe na nderemo, kwa familia za polisi waliouawa Vikindu wilayani Mkuranga, Pwani,  Sajenti Michael Aaron Tuheri (49) na Koplo Francis Mkinga (53) ilikuwa ni huzuni kutokana na vifo vya wapendwa wao hao.


Marehemu Michael Aroni Tuheni enzi za uhai wake.
Mauaji ya polisi hayo yamewaacha ndugu na jeshi la polisi nchini katika hali ya huzuni huku yakifananishwa na yale yaliyotokea katika vituo mbalimbali vya polisi nchini yanayofananishwa na ugaidi.Tukio hilo lililotokea saa 1:30 usiku wa Machi 30, mwaka huu katika kizuizi cha barabarani kilichopo Kijiji cha Kipara, Kata ya Vikindu ni mfululizo wa utekaji wa askari na vituo vya polisi katika Mkoa wa Pwani.

Juni 11, 2014, watu wenye silaha za jadi walivamia Kituo cha Polisi cha Kimanzichana, Wilaya ya Mkuranga mkoani humo na kumuua kwa kumshambulia kwa mapanga Askari Joseph Ngonyani kisha kupora bunduki tatu aina ya SMG na risasi 50.
Januari 21, mwaka huu, watu wasiojulikana walivamia Kituo cha Polisi cha Ikwiriri, Rufiji mkoani humohumo na kuwaua askari wawili, Koplo Edgar na WP Judith na kupora silaha zilizokuwepo kituoni hapo.Katika tukio hilo la Vikindu, polisi hao walikuwa wanne ambapo wawili walikuwa wanakula huku wengine wakiwa barabarani.

Marehemu Francis P. Mkinga enzi za uhai wake.
Mara baada ya tukio hilo, timu ya waandishi wa habari za uchunguzi wa Gazeti la Uwazi ilitinga katika eneo hilo na kufanya mahojiano na wakazi wake ambao walikuwa na haya ya kusema:
“Mimi nilikuwa ninapita pale niliwaona watu kama kumi hivi wakielekea katika kizuizi walipokuwa polisi. Baada ya muda mfupi nilisikia kelele za mtu akilia, akisema ‘msiniue mnanikata, nimewakosea nini?’ Halafu ghafla nikasikia milio ya risasi, nilijua kuna uvamizi.
Miili ya polisi hao ikiagwa.
“Mimi na baadhi ya majirani tuliulizana lakini bila kupata majibu. Baadaye ndipo tukapata habari kwamba polisi wawili wameuawa na majambazi na mmoja wao (Sajenti Ali) amejeruhiwa.“Polisi hawakuchukua muda mrefu kufika lakini walikuta wahalifu hao wameshaishia zao.“Hawa watu ni wabaya sana, hivyo IGP Ernest Mangu asipochukua hatua haraka polisi watakuwa wanauawa na kunyang’anywa silaha kila kukicha.”
“Mimi naamini hawa watu wanakusanya silaha, naamini kuna jambo kubwa watalifanya huko mbele maana hata Boko Haramu walianza kidogokidogo na kwa sasa wanaisumbua serikali ya Nigeria.“Kuna haja ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) kushirikiana na polisi kukomesha hii hali, hatuna raha kuona vijana wetu wanatekwa na kuuawa kinyama kila kukicha bila hata hatua madhubuti kuchukuliwa. Huu ni ugaidi, ugaidi kwa sababu haiwezekani jambazi avamie, waue na kuchukua silaha za kivita.”Mkuu wa Mkoa wa Dara es salaam Meck Sadick akiaga mwili wa marehemu.
Vyanzo vyetu makini ndani ya jeshi la polisi vinadai kwamba wakati polisi hao wanavamiwa, Francis alishtukia kitu chenye makali kikiingia shingoni, aliishiwa nguvu, bunduki ikadondoka na kuchukuliwa na mmoja wa watu hao.
Michael yeye alipigwa risasi ya mgongoni na kutokea kifuani, wote wakafariki dunia papo hapo, wakati huo sajenti Ali alikimbia na bunduki iliyobakia huku akijeruhiwa na risasi mguuni.Taarifa toka kwa marafiki wa marehemu Francis zinadai kwamba, ni kama walijua watakufa kwani aliwahi kusema kuwa kwenye kizuizi wanapangwa wachache wakati kizuizi hicho kipo porini hivyo kuna siku wanaweza kuvamiwa kirahisi.
Baadhi ya maafisa wa jeshi la polisi wakiwa wamebeba jeneza.
Agnes Michael, mke wa marehemu Michael alipohojiwa na Uwazi juu ya kifo cha mumewe alisema:
“Ilikuwa saa 2:30 usiku wa kuamkia Jumanne ndipo nilipopata taarifa kutoka kwa afande mwenzake kwamba mume wangu ameuawa na watu wasiojulikana akiwa kazini.Nilipata mshtuko mkubwa sana kwani tulikuwa tukiishi vizuri. Ni mwaka juzi tu tulifunga ndoa,” machozi yakamtoka.

Moja ya jeneza likipakiwa kwenye gari.
IGP MANGU NAYE
Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Ernest Mangu (pichani) aliwataka askari kujipanga kwa sababu wanapambana na watu wanaotaka kuwapunguza nguvu za polisi.“Tutumie msiba huu kuhakikisha hawa watu tunawashinda. Pia tunawaomba wananchi watupe ushirikiano.” alisema Mangu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate