EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 8, 2015

MWANAMKE ASUTWA KWEUPE!

MSUTO! Mwanamke aliyetajwa kwa jina la Sina, mkazi wa Kawe jijini Dar amejikuta akisutwa mchana kweupe baada kumvujishia taarifa rafiki yake aitwaye Cheka Komba Mbegere kuwa wanawake wanaojiita Cash Money wanakwenda kumsuta, Risasi Mchanganyiko lilifuatilia hatua kwa hatua.Mwanamke aliyetajwa kwa jina la Sina (mwenye nguo nyekundu mbele kushoto), mkazi wa Kawe jijini Dar akisutwa mchana kweupe  na wanawake wanaojiita Cash Money wanakwenda kumsuta.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo Cash Money walichoshwa na tabia ya umbea wa Cheka ambaye ni memba wa kundi hilo, ndipo walipoamua kumfungia kazi lakini akanusurika baada ya kutonywa na Sina ndipo wamama hao waliobeba ngoma za vidumu vya maji walipomsuta Sina kwa niaba ya Cheka.
Kwa mujibu wa Jamila ambaye naye ni memba wa Cash Money, Cheka alimgombanisha yeye na Sheila kwa kumwaambia kuwa wanatembea na bwana mmoja aitwaye Bubu pasipo kujijua.“Huyu mama amenifanyia kitu mbaya sana, alikuwa anakwenda kumwambia Sheila kuwa mimi natembea na mume wake ambapo tulikuwa tukigombana mara kwa mara na mwisho ndiyo hiyo juzi aliponivamia na kunipiga wakati nimelewa.

Majibizano yakendelea.
“Kwenye ule ugomvi Cheka naye alikuja kunichangia, kesho yake nilipozinduka nilikwenda kituo cha polisi Kawe na kushtaki, asivyo na haya akamuandikia SMS Sheila akimwambia waende kwa mganga ili eti waifute kesi,” alisema Jamila.

Baada ya kuona mambo yameshindakana kwa mganga, Sheila akaona bora amuombe msamaha Jamila ndipo walipomjua ‘mchawi’ wao ni Cheka kisha wakaungana kwenda kumsuta.
“Nilipoona mambo yamenifika shingoni nikaona nirudi kwa mwenzangu nimuombe msamaha tupatane, ndiyo nikamweleza mtu aliyekuwa akituchonganisha tukapanga siku ya kumsuta ambayo ndio leo lakini bahati yake akawa ametonywa akakimbia, tulichunguza tukabaini ametonywa na Sina ndipo naye tukamsuta barabara,” alisema Sheila.
Paparazi wetu aliwashuhudia Cash Money wakimuimbia Sina nyimbo za kumsuta huku wakipiga ngoma za vidumu vya maji kwa takriban nusu saa ambapo Sina alileta vurugu kali ya kutaka kujinasua lakini hakufanikiwa.
“Hii ndiyo kiboko ya wambeya, kwa aliyeona fedheha hii kamwe hawezi kufanya umbeya wa aina yoyote,” alisikika shuhuda  mmoja.
Baada ya kumalizika kwa tukio hilo, paparazi wetu alimvutia waya Cheka ili kumuuliza kama ni kweli alihusika kuwagombanisha Jamila na Sheila na sababu za yeye kutimka nyumbani hapo siku ya tukio.“Mimi nilikimbia kwa sababu walisema eti wamewaita waandishi waje wanisute lakini ukweli ni kwamba mimi sijawahi kuwachonganisha ila walipopigana nilikwenda kuwasuluhisha.
“Hata hivyo wale hawanipendi kwa sababu nimejitoa kwenye kundi lao na ninawadai hela zangu ndio maana wananichafua,” alisema Cheka.   Hata hivyo, Cash Money waliahidi kufanya msuto ‘party two’ muda wowote watakapomtia mikononi Cheka wakidai wamechoshwa na tabia yake ya kuwagombanisha watu.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate