EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 8, 2015

WASTARA AANDIKA HISTORIA

Waandishi Wetu
AJABU! Staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma usiku wa kuamkia Jumatatu aliandika historia ya aina yake ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, Dar kwa kuonesha shoo ya nguvu jukwaani hivyo kuwafanya mashabiki kibao waliohudhuria ukumbini hapo kupigwa butwaa wasiamini kama ni yeye.
Staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma akicheza kwa hisia.
Katika shoo hiyo ya Sikukuu ya Pasaka iliyotambulika kwa jina la Mwana Dar Live, wasanii, Msaga Sumu, Ali Kiba na Isha Mashauzi walitumbuiza, lakini Wastara alihudhuria maalum kwa ajili ya  Ali Kiba.
ATINGA NA TIMU KIBA
Wakati jukwaani akiimba msanii wa muziki wa Vigodoro, Msaga Sumu, kundi kubwa lililojulikana kama ‘Team Kiba’ likiwa na watu zaidi ya kumi lilitinga ukumbini hapo likiongozwa na Ali Kiba mwenyewe huku Wastara akiwa miongoni mwao.
AJIWEKA KARIBU NA DADA KIBA
Katika hali ya kushangaza, punde baada ya kundi hilo kutinga ukumbini hapo, Ali Kiba alipanda jukwaani na kumuacha Wastara akiwa sanjari na dada wa Kiba aitwaye Zabibu Kiba huku muda wote akionekana kucheka na kurusha mikono kwa shangwe.

Kudhihirisha kuwa amekuja kama Team Kiba, staa huyo alionekana kukongwa na nyimbo zilizokuwa zikiimbwa na Kiba kiasi cha kuanza kuserebuka hadharani huku Zabibu akimpa sapoti kwa kuibiaibia kiaina.

Kitendo cha kuendelea kuserebuka nyuma ya jukwaa kiliwashangaza baadhi ya watu huku wengine wakiwa hawaamini kama ni Wastara wanayemjua wao.
“Jamani kweli huyu ni Wastara tunayemjua au? Mh! Mimi sijawahi kumwona akisakata muziki kama hivi. Ama kweli Dar Live ndiyo kiwanja cha burudani, ingekuwa viwanja vingine sidhani kama angejiachia,” ilisikika sauti ya shabiki mmoja wa muziki baada ya kukosa uzalendo kwa kumuangalia Wastara.
WATU WAPIGWA BUTWAA
Baada ya kusakata mauno nyuma ya jukwaa kumnogea na kusababisha kuzua minong’ono ya hapa na pale, mdada mmoja alionekana kuvutiwa na staa huyo na kuamua kumshika mkono kwa kumtaka apande jukwaani ili akawadhihirishie mashabiki wote kuwa, anayaweza kama si kuyamudu!
Awali, Wastara alionekana kukataa katakata na kugeuza kichwa huku na kule kwa aibu lakini dakika kama tatu mbele, ghafla aliibukia jukwaani ambapo Ali Kiba pamoja na mdogo wake, Abdu Kiba walikuwa wakiimba pamoja wimbo wa Chekecha Cheketua na kuwafanya mashabiki kupigwa butwaa.
ATUMIA ZAIDI YA DAKIKA TATU
Wastara aliyevaa suruali nyesi na juu kitop cha jinzi, akiwa jukwaani hapo, bila kupepesa macho alianza kwa kuwanyooshea mkono mashabiki wake kisha akawageuzia mgongo na kuanza kuyakata mauno kwa staili ya Chekecha Cheketua huku baadhi ya mashabiki hao wakiwa hawaamini kwa kile alichokuwa akikifanya, wengine walitamani kupanda jukwani wakajirushe naye.
Pale jukwaani, Wastara alitumia zaidi ya dakika tatu kiasi cha kuwafanya Ali na Abdu kushusha vipaza sauti vyao na kumuangalia staa huyo akiwafundisha mashabiki staili ya wimbo huo wa Cheketua.
Hadi anaondoka kwenye jukwaa hilo la kisasa, mashabiki walikuwa wakimshangilia staa huyo wengine wakisema kumbe ni fundi wa kucheketua!
“Loo! Wastara bwana! Leo amenifanya nimpende zaidi, kumbe anayaweza, huwezi amini kabisa. Ama kweli Mungu kila mtu kampa kipawa chake,” alisema shabiki mmoja huku macho yake yakimsindikiza Wastara wakati anaondoka.
TUJIKUMBUSHE
Wastara alifunga ndoa Juni 6. 2009 na msanii mwenzake, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ (sasa marehemu). Wakiwa wachumba wawili hao walipata ajali mbaya ya bodaboda maeneo ya Tabata jijini Dar ambapo Wastara alivunjika mguu na baadaye kukatwa kabisa hivyo kumfanya awekewe mguu wa bandia.
Katika kipindi chote hicho na hasa baada ya kifo cha Sajuki, Wastara amekuwa akiishi katika mazingira ya kidini na hakuwahi kuonekana akicheza muziki hadharani kama vile, hivyo alichokifanya usiku huo kwake ni kuandika historia mpya ya maisha yake ya ustaa.Kwa kilichotokea kwenye upande wa burudani usiku huo, nenda Ukurasa wa 8&9.Imeandaliwa na Andrew Carlos, Mayasa Mariwata, Deogratius Mongela na Shani Ramadhani.
CHANZO-GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate