EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 10, 2015

PENZI LA NAY, SHAMSA SIWEMA, MUME WA SHAMSA VILIO

Musa mateja na imelda mtema
Penzi matata linalowanyima usingizi baadhi ya watu mjini kwa sasa kati ya mwigizaji wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford na mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ limeibua tafrani kubwa huku waliokuwa wapenzi wa mastaa hao wakijikuta wakiangua vilio kweupe, Ijumaa limesheheni.
Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego na Shamsa Ford wakipozi kimahaba.
TATIZO MAHABA NIUE
Mara baada ya wawili hao kutangazwa rasmi kuwa sasa ni mahaba niue huku picha za ushahidi zikimwagwa, aliyekuwa mwandani wa Nay, Siwema a.k.a Wemalicious na aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’ wanadaiwa kujikuta kwenye hali mbaya kiasi cha kumwaga machozi.
TUJIUNGE NA CHANZO KWA SIWEMA
Habari kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa Siwema jijini Mwanza zilidai kwamba, mara baada ya picha za wawili hao kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii aliumia roho hasa alipomuona Shamsa akijiachia kwenye nyumba ambayo alishirikiana na Nay kuijenga.
“Yaani Siwema ameumia hadi akajikuta akiangua kilio kwa uchungu. Sikukuu ya Pasaka ilikuwa mbaya kupita kiasi kwa Siwema. “Kinachomuuma zaidi ni kwamba hata nguo zake za mtoko Shamsa anavaa ‘gym’ na kufanyia mazoezi. Jamani kuna dharau zaidi ya hiyo? “Ukweli roho inamuuma vibaya mno,” kilisema chanzo hicho kwa ombi la kutochorwa jina gazetini.
Ney na Shamsa wakifuatilia jambo kwenye simu.
Kabla ya kuhamia kwa chanzo cha mume wa Shamsa ili kupata ubuyu kamili, gazeti hili lilimsaka Siwema ili kujua anachukuliaje jambo hilo ambapo alifunguka ya moyoni.
SIWEMA AANIKA MAZITO
Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Siwema mwenye mvuto wa kuvunja midume shingo alianika mazito kwamba, kitendo cha Nay kumuacha na muda si mrefu kwenda kwa Shamsa ni upuuzi.

Siwema alifunguka kwamba, kinachomshangaza ni kitendo cha Shamsa kuvaa nguo zake na kufanyia mazoezi.
Mwanamama huyo alisema watu watamtukana kwa kuwa hawajui tabia ya Nay kwani hata Shamsa atamshindwa tu.
“Nilivumilia vitu vingi sana. Maumivu nayajua mimi, nyumba tuliyojenga wote, anaingia mwanamke mwingine. Namhurumia sana Shamsa kwani hajui tabia za Nay,” alifunguka mtoto mweupe, Siwema kwa uchungu.
KUMBE SIWEMA ALIJUA
Habari zilieleza kwamba, Siwema alijua muda mrefu kuwa Nay anatembea na Shamsa lakini alipomuuliza staa huyo anayetamba na Ngoma ya Akadumba alimwambia walishaachana.
Siwema.
NAY ANASEMAJE?
Akizungumzia ishu hiyo, Nay alisema kuwa yeye yupo na Shamsa na kwamba anamshangaa huyo Siwema kwani alishaachana naye.
TUJIUNGE NA CHANZO KWA MUME WA SHAMSA
Kwa mujibu wa chanzo makini, naye kama Siwema, baada ya penzi la Shamsa na Nay kuwa ndiyo habari ya mjini huku wakitupia picha za malovee mtandaoni, mume wa Shamsa, Dick alipaniki kiasi cha kutokwa machozi huku akitafuta namna ya kupooza machungu.
JB AOMBWA AOKOE JAHAZI
Habari zilidai kwamba, Dick alikimbilia kwa staa wa sinema za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’ na kwenda kumuomba aokoe jahazi akimshitakia Shamsa kuwa ameamua kumwacha na kuamua kutembea na Nay, jambo ambalo analiona kuwa ni udhalilishaji kwani ni mkewe ambaye amezaa naye mtoto mmoja wa kiume, Terry.
Mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Ilidaiwa kuwa, baada ya Dick kufika nyumbani kwa JB maeneo ya Ubungo-Kibangu, Dar na kumweleza hayo, mwigizaji huyo alimpigia simu Shamsa ambaye humwita Daddy na kumuuliza juu ya suala hilo ambapo alimweleza kuwa alishaachana na Dick hivyo kila mmoja ana maisha yake.
Katika hali hiyo, JB aliwataka kukaa chini na kuyamaliza kiutu uzima kuliko kuwekeana kinyongo.
SHAMSA ANASEMAJE?
Baada ya kusikia kilichopo upande wa mume wa Shamsa, gazeti hili lilimgeukia Shamsa na kumwelezea kila kitu kilichopo ambapo alionesha kumshangaa Dick kwa kuwa alishamalizana naye tangu Oktoba, mwaka jana.
“Kwanza namshangaa kwa nini anawaka wakati kila mtu ana maisha yake?“Tulishaachana tangu mwaka jana so kila mtu ana maisha yake,” alisema Shamsa ambaye kwa sasa amehamishia moyo wake kwa Nay.
Aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’.
DIAMOND ACHAFUA HALI YA HEWA
Wakati sakata la Shamsa na Nay likishika kasi mithili ya moto wa kifuu, mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amechafua hali ya hewa baada ya kutundika mtandaoni picha ya mahaba ya wapenzi hao iliyosababisha tafrani zaidi.
Diamond ambaye ni swahiba wa Nay ndiye aliyekuwa wa kwanza kuweka picha iliyomuonesha Nay ‘akibusiana’ na Shamsa kupitia ukurasa wake wa Instagram hivyo kuwapandisha hasira Siwema na Dick kwani alionekana kufurahishwa na ‘pea’ hiyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate