EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 7, 2015

WA 3 WALIOFUNGIWA NDANI MIAKA 10 NA MAMA YAO MMOJA AFARIKI DUNIA


Na Haruni Sanchawa
Katika Gazeti la Uwazi Toleo Na. 893 wiki iliyopita, kuliandikwa habari ya kusikitisha yenye kichwa kisemacho; MAMA AWAFUNGIA NDANI WANAYE 3 KWA MIAKA 10. Ni habari ambayo ilizua gumzo kubwa nchini kutokana na mazingira yake kuwa ya kushtua.
Marehemu Ally Juma enzi za uhai wake.
Baada ya habari hiyo kutoka ambayo ilikuwa na lengo la kuisaidia familia hiyo, sasa habari mpya ni kwamba, mmoja wa watoto hao, Ally Juma amefariki dunia ghafla.
Marehemu Ally aliaga dunia bila kuugua usiku wa kuamkia Aprili 4, mwaka huu na kuzikwa Jumamosi iliyopita majira ya alasiri mazishi ambayo yalihudhuriwa na mamia ya wakazi wa Kijiji cha Kanga, Wilaya ya Mafia mkoani Pwani.

ALLY NI NANI?
Marehemu Ally ni miongoni mwa watoto watatu, wakiwemo Muhadia (wa kike) na Mzee ambaye alidaiwa kumpa ujauzito Muhadia ambaye ni dada yake kwa kuzaliwa.Uwazi lilifanikiwa kupata taarifa za kifo cha  Ally na kushiriki msiba huo ambapo  umati mkubwa wa wanakijiji walijitokeza, lakini cha kushangaza wengi walisema hawakuwa na taarifa za kufungiwa kwa watoto hao ndani kwa muda wa miaka 10.
Mwili wa Ally Juma ukipelekwa eneo la kaburi kwa ajili ya kuzikwa.
MAMA ASIMULIA
Mama wa watoto hao, Mwasiti Ally alipohojiwa juu ya kifo cha Ally alisema: “Huwa nina tabia ya kwenda kuwaangalia kila siku  usiku kabla ya kulala ili kujua wanaendeleaje  maana silali nao nyumba moja.
“Nilipofika nilimkuta Ally ametulia kama mtu aliyekata roho. Kwanza nilijua amelala, lakini nilipomwita na kumwona haitiki nikaanza kuingiwa na wasiwasi.
“Nilitoka kwenda kumtafuta jirani mmoja  na kumwambia kuhusiana na hali niliyomkuta nayo Ally. Tulikwenda wote. Ilikuwa kama saa 8 usiku. Kufika tukakuta amekata roho kweli. Ikabidi tuanze kutoa taarifa kwa majirani wengine.”
AMEKUFA KWA MAZINGIRA MAGUMU
Baadhi ya wanakijiiji walisema kuwa, kwa vile mama mtu anasema marehemu hakuonesha dalili zozote za kuumwa, wanaamini  kifo chake kilisababishwa na mazingira magumu, hasa ya kufungiwa ndani ya chumba kwa miaka mingi hivyo kukosa hewa safi, mionzi ya jua na kugusana na wadudu watambaao kila siku.
Muhadia ambaye ni dada'ke Ally.
WANACHOJUA WANAKIJIJI
Ally Makame mmoja wa wanakijiji hicho cha Kanga alisema kuwa watoto hao walianza kuteseka kwa miaka mingi lakini watu walipokuwa hawawaoni waliamini mama yao aliwasafirisha kwenda kuishi sehemu nyingine maana kikubwa kilichotawala dhidi ya matatizo yao ni imani za kishirikina.
“Kusema kweli wanakijiji wengi hatujui kama hawa watoto walikuwa wamefungiwa ndani kwa miaka yote hiyo mpaka tuliposoma kwenye Gazeti la Uwazi na hiki kifo kilipotokea.“Sisi tulipoacha kuwaona tuliamini mama yao aliwapeleka sehemu nyingine kuishi maana matatizo yao ushirikina ndiyo ulikuwa ukitajwa sana. Si unajua watoto watatu wa familia moja kuwa na matatizo ya akili haiingii akilini?
“Halafu watu wenyewe licha ya kuwa wagonjwa wa akili lakini walikuwa hawana ugomvi na mtu, ila sema ile tabia yao ya kutembeatembea ndiyo ilikuwa hatari kwa uhai wao,” alisema Makame.
HALI YA DADA NI TETE
Hali ya Muhadia ni mbaya huku watu wakihofia hatima yake, Mzee yeye kidogo ana nguvu na afya kiasi kwamba, muda mwingi hukimbia akiona watu kwa kuhofia kukamatwa.
Mzee Juma, anayedaiwa kumpa mimba dada yake wa kuzaliwa, Muhadia aliyejifungua mtoto akafariki.
UWAZI LAENDELEA KUKATA MBUGA.
Gazeti la Uwazi lilifanya jitihada za kumtafuta Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Dk. Nasoro Hamid ili aweza kutoa ufafanuzi juu ya familia hiyo ambapo alisema kuwa habari hiyo ameisoma kwenye mtandao na kutoa pongezi kubwa kwa Gazeti la Uwazi kwa kuiibua.
“Ndugu mwandishi ninachotaka kusema  ninatoa shukurani nyingi sana  kwa Kampuni ya Global Publishers kutuma mwandishi na kuweza kutoa habari kama  hiyo. “Kwanza  ni habari ambayo imekaa kipekee sana na mwandishi huyo bila kukata tamaa alifika katika kijiji hicho na kufanikiwa kupata  mahojiano na familia,” alisema mkuu huyo wa wilaya.
Ndugu jamaa na marafiki wakiwa na majonzi wakati wa msiba wa Ally.
Baada ya mahojiana na mwandishi wetu, DC huyo alisema amemwagiza Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Mafia kufika katika kijiji hicho ili aweze kupata maelezo ya kutosha kisha kutafuta namna ya kuisaidia familia hiyo.
Uwazi pia lilifika ngazi ya juu ambapo mwandishi wetu aliongea na Msemaji Mkuu wa Wizara ya Afya,  Nsachris Mwamwaja ambapo awali alilipongeza  Gazeti la Uwazi.“Gazeti nimeliona na habari yenyewe nimeisoma, ninampa ‘Big Up’ mwandishi kwa kufumua tukio kama hilo. Mafia ina serikali kamili hivyohivyo nina imani tatizo la familia ile litashughulikiwa kikamilifu na haraka iwezekanavyo,” alisema Mwamwaja.   

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate