EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, May 26, 2015

‘NIMEKUMISS’ YA MWANAMKE, ‘NIMEKUMISS’ YA MWANAUME, TOFAUTI

NIJumanne tena! Tunakutana katika mada hii ya maisha na mapenzi. Ni somo ambalo litaweza kukusaidia katika kubadilika hususan kama wewe ni mwanandoa au upo katika uhusiano!
Leo katika makala haya nazungumzia neno maalum kabisa katika uhusiano linaloitwa miss! Miss yaani kosa, pia ‘kosana’ hutumiwa zaidi na watu wenye uhusiano wowote ule, iwe ndugu, wapenzi na hata marafiki walioshibana.
MATUMIZI YAKE
Ni neno la Kiingereza ambapo watumiaji wanapaswa kuwa Waingereza wenyewe lakini pia wasio Waingereza ambao wanajua maana yake.
Hutumika kwa watu waliopotezana kwa muda ambao mhusika amehisi kumkumbuka mwenzake kwa maana ya kuonana naye laivu.
“Shoga, upo?”
“Nipo shoga yangu, niambie, mzima?”
“Mi mzima tu, nimekumisi ‘miss’ ile mbaya.”
“Nimekumisi pia shoga yangu.”
Maneno hayo ni watu wawili walioshibana ambapo wamepotezana au hawajaonana kwa siku kadhaa. Idadi ya siku za ‘kumisiana’ hutegemea mtu na mtu na si kwamba ni kiwango cha kimataifa kuwa lazima ziwe siku mia moja!

MATUMIZI MENGINE
Matumizi mengine ya neno hili limekuja kujikita kwa watu walio kwenye uhusiano wa kimapenzi. Walio wengi wanapokuwa kwenye mapenzi, hufika wakati kila mmoja akatamani kuwa na mwenzake ‘laivu’ kwa maana ya kukaa pamoja na kuzungumza au kuonana tu pia kunashibisha hamu ya upendo.
Wapenzi walio wengi, iwe mke na mume au wachumba na hata wasiokuwa na vyeo vyote viwili hulitumia neno kumisi kama ishara ya kukumbukana kwa maana kuonana laivu.
MFANO MZURI NI HUU
Mfano mzuri, wapenzi wawili, mmoja amesafiri hivyo kuwa mbali na mwenzake, sasa yeyote yule anaweza kumkosa mwenzake kama ilivyo mazoea yao. Hivyo ni rahisi kumsikia mmoja akianza:
“Baby nimekumisi sana.”
“Hata mimi nimekumisi pia mpenzi wangu.”
“Unarudi lini baby?”
“Wiki ijayo baada ya kumaliza hii kazi.”
“Poa baby, nakutakia kila la kheri.”
“Asante baby.”
Hawa wawili wamemisiana kwa kutoonana laivu kutokana na mmoja kuwa mbali na mwenzake tofauti na mazoea yao.

LAKINI SASA
Pamoja na yote hayo, uchunguzi wa kawaida nilioufanya nimebaini kuwa, neno nimekumisi limekwenda mbele zaidi na kutumika katika uhitaji wa tendo la ndoa, hasa kwa wanawake!
Kivipi? Wapenzi, baadhi yao tena kwa sehemu kubwa wamekuwa wakilitumia neno hili kwa maana ya kutaka kukutana kwa tendo la ndoa.
Unaweza ukakuta wapenzi wanaishi mbalimbali, wamekutana asubuhi lakini jioni, mmoja anamtumia meseji mwenzake ya kumwambia amemmisi sana.
Nilijaribu kutafuta maana yake nini, je ni kumisi kwa maana ya kumuona laivu nikajua si hivyo, nimekumisi hii ni ya kutaka kukutana kwa tendo la ndoa.
TOFAUTI YA MWANAMKE NA MWANAUME!
Ila sasa, kuna tofauti kubwa ya misi ya mwanamke na misi ya mwanaume! Katika wanawake kumi, nane hulitumia neno hili kwa maana ya kutaka kukutana kwa tendo la ndoa tofauti na misi ya mwanaume ambao karibu wote hulitumia kwa kutaka kuonana laivu.
Kama wewe ni mwanaume, una mpenzi wako, tena mkeo kabisa, mko nyumba moja, kitanda kimoja, unaweza kuwa kazini akakutumia meseji kukwambia amekumisi lakini yenye maana ya tendo la ndoa.
Kama wewe ni mwanamke, una mpenzi wako, ni mumeo, ukiwa mbali naye kwa siku nzima, anaweza kukutumia meseji ya hivyo akimaanisha kutokukuona laivu.
WAPENZI, WACHUMBA
Kundi hili ndilo linathibitisha matumizi hayo. Kwamba, wapenzi, wachumba wanaweza kukutana saa kumi jioni, wakiachana usiku, msichana akatuma meseji ya misi akimaanisha kukutana kimwili.
Mara nyingi sana, wanawake hulitumia neno hilo kwa maana hiyo. Nimefanya utafiti na kubaini hilo. Hata wapenzi wanapokuwa hawajakutana kimwili kwa siku kibao, mwanamke akijisikia anakuwa mgumu sana kusema wazi kwamba anahitaji tendo hilo, njia yake kubwa ni kusema ‘baby nimekumisi’ wakati mwanaume huenda moja kwa moja.
Kwa hiyo nathibitisha kwamba, nimekumisi ya mwanamke na nimekumisi ya mwanaume tofauti! Hivyo wanaume mnapaswa kulijua hilo badala ya kudhani ni ile ya kutokuonana na wewe ukajibu ‘na mimi pia’.
Tukutane wiki ijayo katika mada nyingine.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate