EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, May 26, 2015

IMAMU: NIMEMWAGIWA TINDIKALI KUTETEA MALI ZA MSIKITI


CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
UNYAMA wa kutisha! Bwana mmoja ambaye ni imamu, aliyefahamika kwa jina la Mustafa Omar Mustafa, mkazi wa Ghana, Kata ya Nyamanoro jijini Mwanza, amefanyiwa unyama wa hali ya juu kwa kumwagiwa tindikili na watu wanaosadikiwa kuwa ni waumini wenzake, kisa kulinda mali za msikiti wao uliopo katika mtaa huo wa Ghana. Uwazi linakupa habari kamili.
Mustafa Omar Mustafa, anayedaiwa kumwagiwa tindikali.
ILIKUAJE?
Akizungumza na mwandishi wetu kwa masikitiko Mustafa alisema kuwa, tukio hilo la kinyama alifanyiwa majira ya saa mbili kasorobo usiku, Jumapili ya Agosti 31, mwaka jana akiwa nyumbani kwake Ghana.
“Nilikuwa katika hali ya furaha na familia yangu, sikuhisi kabisa hatari ambayo ilikuwa inakuja kutokea katika maisha yangu. Tukiwa hatuna hili wala lile, tulishitukia kundi la watu likivamia nyumba yangu ndipo waliponitendea unyama huu na kutoweka,” alisema.

AKIMBIZWA HOSPITALI YA MKOA SEKOU-TOURE
 “Baada ya unyama huo familia yangu na jamaa wa karibu kwa haraka walinikimbiza katika kituo kidogo cha polisi cha kata hiyo ambapo nilipata kibali cha matibabu (PF3) na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza, Sekou-toure, ambapo nilipokelewa na kuingizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.“Katika chumba hicho nilikaa kwa muda wa siku sita nikahamishiwa katika chumba cha wodi za kawaida.”
Mustafa akionyesha jeraha alilolipata mkononi.
MATIBABU YASHINDIKANA AHAMISHIWA CCBRT
“Baada ya hali yangu kuzidi kuwa mbaya, madaktari wa hospitali hiyo walinishauri kufanya utaratibu wa kwenda kupata matibabu zaidi katika Hospitali ya CCBRT Dar ambayo inasifika kwa kutoa huduma nzuri ya matibabu ya macho.
“Kama unavyoona sehemu kubwa niliyoathirika na tindikali ni usoni, kifuani na mgongoni! Mwanzoni kabisa macho yote hayakuwa yanaona ndipo nilipohamia CCBRT, ambapo angalau nimeweza kupata matibabu, namshukuru Mungu sasa jicho moja la kulia linaweza kuona kwa mbali.
KISA CHA KUMWAGIWA TINDIKALI
 “Kabla ya tukio hilo katika msikiti wetu kulikuwa na mgogoro kati ya waumini na viongozi wa msikiti.
Hatukuwa tunawataka ambapo baada ya mvutano wa muda mrefu uliosababisha kufikishwa  mahakamani baadhi ya watu, uchaguzi wa viongozi wengine ulifanyika chini ya uangalizi maalumu wa mahakama, baada ya kupatikana viongozi wapya nilipendekezwa kuwa imamu na nikawa naongoza sala za asubuhi.
Jeraha la kifuani.
“Kadiri siku zilivyozidi kusonga mbele, nilianza kujihusisha na shughuli mbalimbali za msikiti ikiwemo kufanya usafi wa mazingira  na kutunza baadhi ya rasilimali jambo ambalo lilionekana kutolifurahisha kundi la baadhi ya watu ambao hawakuwa wanaupenda huo uongozi mpya, ambapo kwa kile walichokiita kunikomesha ndipo walipoamua kunimwagia tindikali.
MSAADA
“Kutokana na hali mbaya ya kiuchumi niliyonayo, nawaomba Watanzania watakaoguswa na matatizo yangu kunisaidia ili niweze kupata huduma ya matibabu zaidi kwani hali yangu kiuchumi kwa sasa ni mbaya sana.
“Nawashukuru sana wote ambao wamenisaidia mpaka angalau nimekuwa katika hali hii, japo hali yangu bado haijawa vizuri sana hasa kimaisha, maana nimeshatumia fedha zangu zote kwa ajili ya matibabu na leo hii nafikia hatua ya kuomba kwa kuwa familia inanitegemea na haina namna tena, mtaji wangu wote umeishia katika matibabu.
“Kabla ya kufanyiwa unyama huu nilikuwa wakala wa mitandao ya simu na sasa changamoto yangu kubwa ni hali ya hewa ya jijini Dar es Salaam kuwa ya joto sana, hivyo napata maumivu sana kwenye majeraha yangu.
Jeraha la mgongoni.
MACHO
 “Hivi sasa matibabu ya macho bado yanaendelea ingawa nimeambiwa nirudi tena mwezi ujao (Juni) ambapo nimepewa uhamisho kwenda katika Hospitali ya Ocean Road kwa ajili ya kushughulikia tatizo la ngozi ambayo nayo imeharibika vibaya.
“Nilikwenda katika hospitali hiyo nikaambiwa kumuona daktari tu, natakiwa kutoa shilingi elfu hamsini, kiasi ambacho kwa sasa ni kikubwa sana kwangu maana nakosa hata shilingi mia mfukoni.“Ninayoyasema hapa ni rahisi kwa asiye jua hali yangu kuona kama natania ila ukweli ni kwamba hata fedha ya kwenda hospitali kumuona huyo daktari sina.
“Nawaomba Watanzania wanisaidie ili niweze kumuona daktari kisha nipate nauli ya kurudi Mwanza kukaa na familia yangu japokuwa siwezi kuihudumia. Changamoto ni kwamba baada ya mwezi natakiwa kurudi Dar kwa matibabu ya macho na ngozi.
“Nampongeza sana Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo kwa kuwa nami bega kwa bega tangu nipate tatizo hili na hakika yeye ni mtu mwenye upendo wa dhati, pia nawashukuru wote ambao wanaendelea kunijulia hali,” alisema Mustafa huku akilengwalengwa na machozi.
 Aliyeguswa na habari hii awasiliane naye kwa namba 0752 362 221, kutoa ni moyo.
Ili kupata mahojiano kamili tembelea tovuti ya www.globaltvtz.com au
www.globalpublishers.info

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate