EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, May 25, 2015

UBONGO WA KAJALA WAPATA TATIZO

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Maskini Kajala! Ndivyo unavyoweza kusema ukisikia mkasa wa staa wa kiwango cha juu kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’, ambaye anadaiwa kwa hivi sasa hayuko sawa kiafya baada ya kupigwa chupa kichwani akiwa katika shoo ya kumchangia mke wa msanii Mabeste iliyofanyika New Maisha Club, Masaki jijini Dar.
Kajala Masanja akionekana na jeraha usoni kipindi ambacho alikua amepigwa chupa.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Kajala kimeliambia Ijumaa Wikienda kwamba, tangu staa huyo akumbwe na sekeseke hilo amekuwa katika kipindi kigumu kwani amekuwa akipata maumivu makali sehemu ya kichwani huku akianguka mara kwa mara.
Kajala Masanja.
Kilidai kwamba, pia Kajala amekuwa akipata kizunguzungu kikali hivyo kujiona yupo kwenye hatari kubwa hasa ikitokea akaanguka vibaya kwani anaweza kupoteza maisha.
 ASHINDWA KUENDESHA GARI
Mpashaji wetu huyo aliweka wazi kuwa tangu Kajala akumbane na mkasa huo mzito uliomsababishia kushonwa nyuzi mbili juu ya jicho, amekuwa hayuko vizuri na kuna wakati hawezi hata kuendesha gari hivyo kukwamisha shughuli zake za kila siku.
“Kiukweli Kajala hayupo vizuri kabisa,  amekuwa kwenye kipindi kigumu mno tangu alipopigwa chupa klabu.
“Amekuwa akianguka mara kwa mara kutokana na kizunguzungu kikali anachopata akisimama au kutembea,” kilisema chanzo hicho.
 CT-SCAN;mfano wa mashine ambayo Kajala amefanyiwa vipimo.
ATINGA HOSPITALINI
Habari zilizidi kumiminika kuwa, baada ya kuona hivyo Kajala alikwenda kwenye Hospitali ya Regency iliyopo Upanga jijini Dar kwa ajili ya kufanya vipimo.
 AFANYIWA CT-SCAN
Kilisema kuwa alipofika hospitalini hapo alifanyiwa kipimo cha CT-SCAN kichwani ambapo majibu yalipotoka aliambiwa kuwa kinachomsumbua ni damu iliyoganda sehemu aliyopigwa chupa.
 MAJIBU YA DAKTARI
“Daktari alimpa majibu ya kushangaza maana alimwambia kama angezembea, tatizo lingekuwa kubwa sana kwenye ubongo na lingeleta shida zaidi,” kilisema chanzo hicho.
 HUYU HAPA KAJALA
Baada ya kunyetishiwa mkasa huo wa kusikitisha, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Kajala ili kuthibitisha tatizo hilo alilokuwa nalo ambapo alikiri kuwa alikuwa akihisi kizunguzungu kikali cha mara kwa mara lakini hakuwa amegundua kama alikuwa na tatizo la kuvilia damu kichwani.
“Lakini kwa sasa namshukuru Mungu niko sawa kidogo. Ukweli nilikuwa napata shida sana kila nikiinuka, napata shida ya kizunguzungu kikali sana,” alisema Kajala.
 TUJIKUMBUSHE TUKIO
Wakati Kajala akitoka Klabu ya New Maisha hivi karibuni, akiwa anashuka kwenye ngazi, ghafla alishangaa kurushiwa chupa kichwani iliyosababisha kuanguka kutoka kwenye ngazi hadi chini na kusaidiwa na wasamaria wema waliompeleka katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar ambapo alishonwa jeraha alilolipata.
Katika sakata hilo, Kajala alisema kuwa mtu aliyempiga chupa ni mwanaume na tayari yupo mikononi mwa polisi japo kabla ya tukio hilo alikuwa  hamjui na wala alikuwa hajawahi kumuona.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate