EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 1, 2015

USTAA UMEWASHINDA,WAPO KAMA HAWAPO!!!


Na Hamida Hassan
Wapo mabinti ambao waliingia kwenye fani ya uigizaji kwa mbwembwe, wakawika sana kwenye vyombo vya habari na kuunyemelea ustaa lakini ghafla wakayeyuka.Walipoibukia kwenye fani walionekana watakuwa tishio na kuwafunika wale wakongwe waliokuwa wakionekana wao ndiyo wao. Sasa hivi hawajulikani wako wapi na wanafanya nini.
Skaina Ally
Skaina Ally
Huyu alikuwa tishio sana miaka ya nyuma. Umbo lake tata, uzuri wake vilimbeba, akawavutia baadhi ya wanamuziki ambao walimfanya kuwa Video Queen kwenye nyimbo zao kama vile Bob Junior aliyemtumia kwenye ‘kichupa’ chake cha Wimbo wa Kimbiji.

Aliigiza kwenye filamu mbalimbali kupitia Kampuni ya RJ. Hata hivyo, baadaye aliolewa kisha akaachika, mara akabeba ujauzito uliodaiwa ni wa mwanamuziki Nay wa Mitego. Baada ya kujifungua akawa kimya, mwanaye ni mkubwa lakini haijulikani sasa anafanya nini.
Zamda Salim
Huyu naye aliibuka miaka 2010 kwenye soko la filamu. Ana umbo zuri lililomfanya atumike kwenye filamu kadhaa.
 Naye alionekana kuja kuwafunika mastaa lakini cha kushangaza akaanza kufifia na mpaka sasa hata wewe msomaji unayefuatilia masuala ya burudani ukiulizwa yuko wapi na anafanya nini huwezi kuwa na jibu.Mara ya mwisho zilivuja picha akiwa amevaa shela, watu wakasema ameolewa lakini wengine wakadai ni filamu.
Zamda Salim
Ester Flaviana
Huyu ni mmoja wa maandagraundi walioibuka kwa kasi ya ajabu. Aling’ara kwenye magazeti, akaonekana kwenye filamu mbalimbali lakini naye mara ya mwisho zilivuja picha zake za utupu na mpaka leo hii haijulikani kajichimbia wapi.
Diana Kimaro
Diana Kimaro ni binti f’lani mcharuko. Mcharuko wake umeonekana kwenye filamu mbalimbali alizocheza kama vile Family Disaster. Aling’ara sana alipokuwa akiigiza kwenye filamu kama Pacha wa Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mara ya mwisho alikuwa akisoma Moshi kisha baadaye akaonekana kwenye filamu ya Msuto Daily na Kigodoro lakini hawiki kama anavyowika shoga yake Lulu.
Rehema Fabian.
Rehema Fabian
Aliibukia kwenye Shindano la Miss Kiswahili 2008, akapaa zaidi pale alipokuwa akitoka kwenye magazeti na skendo tofauti huku akionekana kwenye filamu mbalimbali.Mara ya mwisho alikimbilia nchini China ambapo alidai kuchumbiwa na mtoto wa kigogo wa Nigeria. Juzikati ilisemekana ni mjamzito, amekaa kimya haijajulikana anafanya nini.
Neema Chande
Huyu alitokea kwenye umiss, alivuma sana alipojiingiza kwenye masuala ya filamu na kufikia hatua ya kutoa filamu yake aliyoipa jina la Time Goes Around. Alipamba kurasa mbalimbali za magazeti kwa habari zake tofauti.
Staa huyu kwa sasa yupo nchini India, anaonekana kwenye mitandao tu ya kijamii, haijulikani anafanya nini huko lakini kwenye anga za mastaa amepotea kabisa.
Pendo wa Maisha Plus.
Pendo wa Maisha Plus
Jina lake kamili ni Upendo Mushi. Staa huyu aliibukia kwenye Shindano la Maisha Plus. Baada ya hapo alicheza kwenye filamu mbalimbali. Kuna kipindi ilidaiwa kutoka na marehemu Kanumba na Diamond Platnumz.
Lakini naye sasa hivi haijulikani anafanya nini. Wapo wanaosema anaigiza lakini habari zake zimekuwa ngumu kuzipata tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo alikuwa hakauki kwenye vyombo vya habari.
Amisuu Malick
Huyu naye alipamba kurasa za magazeti baada ya kuibukia kwenye umiss. Wapo wanaodai alichumbiwa ndiyo sababu ya kuwa kimya.Marafiki zake wa karibu wanasema kuwa ameamua kutulia na kufanya mambo yake ambayo si lazima yaanikwe hadharani.
Sharzy Sadry
Huyu naye ni staa ambaye alitoka na marehemu Steven Kanumba kwenye filamu ya ‘The Shock’. Alionekana kuwashtua mastaa wa Bongo kwani filamu hiyo aliicheza kwa umahiri.Wapo waliosema kuwa Kanumba alimchukua ili kuziba pengo la Wema kwani kwa wakati huo Wema na Kanumba walikuwa wameachana.
Halima Madiwa
Aliibukia kwenye uigizaji wa filamu. Waliomchezesha kwenye filamu waliamini kuwa angekuja kuwa tishio. Akawa hakauki kwenye magazeti lakini naye cha ajabu kapotea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate