EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 23, 2015

BABA ANAYEDAIWA KUMCHINJA MWANAYE HUYU HAPA

Shani Ramadhani na Mayasa Mariwata
MAPYA yameibuka! Kwamba baba mzazi anayedaiwa kumchinja mwanaye hivi karibuni maeneo ya Mabibo Luhanga jijini Dar, Maneno William Kasuga (50) (pichani),  kuwa kabla hajafanya unyama huo aliomba atumiwe pesa na mzazi mwenzie ndipo  amrudishe mtoto.
Baba aliyefahamika kwa jina la William Kasuga akionekana katika picha na mwanae aliyemchinja.
Akizungumza na waandishi wetu bibi wa marehemu William,  Mwanaidi Hassan alidai kabla ya tukio, baba mzazi aliomba arushiwe pesa na mzazi mwenzie halafu ndiyo amrudishe mtoto huku akitoa onyo kali.

“Mtoto alikuwa na baba yake tangu saa mbili asubuhi wakati huo mama yake alikuwa akimpikia uji na baada ya uji kuiva alimpigia simu mumewe ili amrudishe mtoto anywe uji halafu ndiyo aondoke naye, yule baba alisema kuwa anataka atumiwe shilingi elfu hamsini kwanza halafu ndiyo aonyeshe mtoto alipo.
“Mwanangu alijua ni utani akapiga tena kwa mara nyingine akaambiwa tena kauli ileile, akaona atushirikishe sisi na baadaye akaamua kwenda katika Kituo cha Polisi Mabibo Luhanga na kutoa taarifa lakini polisi walipouliza wakaambiwa mtoto yuko na baba yake hawakushtuka wakasema huenda anatania hivyo yeye arudi nyumbani na mtoto atarudi tu,” alisema bibi wa marehemu.
Alidai baba mzazi huyo hakuishia hapo, alipiga tena simu kwa mara nyingine huku akimuamuru mzazi mwenziye atume pesa haraka iwezekanavyo na kama atashindwa basi atakuwa amemkosa mtoto kabisa.
“Mimi nilijua hivyo kuwa atarudi tu kwa sababu huwa anamchukua na kumrudisha lakini nikashangaa alipopiga simu kwa mara nyingine tena huku akisema nimtumie hiyo pesa haraka ndani ya saa moja na kama nitachelewa basi yeye atamchinja mtoto na mimi nitakuwa nimemkosa kwa uzembe wangu.
“Nikawapigia rafiki zake na kuwaeleza kuhusu hilo wakashangaa na kuniambia huenda alikuwa amechanganyikiwa kwa sababu hata mimi ndugu zangu walianza kunijia juu na kuniambia kama alinipa hizo shilingi elfu hamsini nimrudishie nikawaambia hakunipa ndiyo nikajaribu kupiga simu ikawa haipatikani na ndipo nilipoanza kusikia minong’ono huko nje kuwa kuna mtoto amechinjwa kwenye Msitu wa Njia ya Miti uliopo pembezoni mwa Shule ya Sekondari Loyola,” alisema mama mzazi wa mtoto huyo, Amina Hassan.
Habari hii iliandikwa katika gazeti hili toleo lililopita likiwa na kichwa cha habari: ‘Baba mzazi amchinja mwanae wa kumzaa.’

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate