EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 23, 2015

GONJWA LA AJABU LAMKUMBA BAADA YA KUPATA UJAUZITO, MWANAUME AMKIMBIA!

Na Makongoro Oging’
MAAJABU ya Mungu! Ukisema wewe unaumwa sana, inawezekana hujawaona wagonjwa wengine! Faiza Masaka Paga (23)(pichani), mkazi wa Chanika –Msumbiji, Ilala jijini Dar amekumbwa na gonjwa la ajabu ambalo mpaka sasa madaktari hawajajua ni nini kwani sehemu ya kiuno na kalio upande wa kushoto imevimba na kumfanya aonekane ana kama nundu kubwa ya kutisha!
Faiza Masaka mkazi wa Chanika akionyesha jinsi uvimbe huo ulivyo kwenye mwili wake.
Akizungumza na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa mfadhili anayeishi naye huko Chanika, Faiza alisema tatizo hilo lilimuanza mara tu baada ya kupata ujauzito, Mei mwaka jana.

 
.......akionyesha jinsi uvimbe huo ulivyomkubwa na unavyomsumbua.
MSIKIE MWENYEWE
“Ilikuwa mwaka jana, nikiwa mjamzito wa huyu mwanangu (aliyempakata pichani mbele). Sehemu hii ilianza kwa kuvimba kitu kama kipele, baadaye kikawa kinakua kwa kasi mpaka nikaogopa sana.
“Labda nianze kwa kusema hivi, kabla ya kuupata ugonjwa huu wa kushangaza, nilipitia mambo magumu na mazito, kumbe ilikuwa ni salamu kwa ajili ya tatizo hili.
“Nikiwa darasa la pili, Shule ya Msingi Mnazi Mmoja (Dar) baba aliugua, akawa haendi kazini. Maisha yakawa magumu. Ilibidi mama aanze biashara ya kuuza mahindi ya kuchemsha mitaani. Kuna wakati yakawa hayauziki na akirudi nayo ndiyo tuliyageuza chakula cha usiku. Nilipofika darasa la tatu, baba alizidiwa, akafariki dunia.
 
......akionyesha kwa upande wa nyuma jinsi uvimbe huo unavyoonekana kwenye mwili wake.
WAFUKUZWA KWENYE NYUMBA
“Nyumba tuliyopanga ikaisha kodi, mwenye nyumba akabaini kwamba mama hana huwezo wa kulipia tena, akatutimua. Tukawa hatuna pa kwenda. Ilibidi tuondoke Dar kwenda Tanga kwa bibi na babu wazaa mama. Walitukaribisha ingawa kulikuwa na mzigo mkubwa wa maisha.
 BABU AFARIKI DUNIA
“Kabla hatujakaa sawasawa, babu aliugua ghafla, akafariki dunia. Tukawa tunaishi kwa shida na bibi, hata kusoma kwangu kukawa kwa shida.”

......akiwa anamnyonyesha mtoto wake ambapo alipata uvimbe huo mara baada tu yakushika mimba yake.
MAMA, BIBI WAFARIKI DUNIA
Bado nikiwa katika mawazo ya maisha yangu ya baadaye hasa kuhusu elimu, mama naye aliugua akafariki dunia. Nikabaki na bibi tu.”
“Tukawa tunaishi kwa shida sana. Nilijitahidi kwenda shule ingawa wakati fulani nilikuwa nikishinda njaa. Lakini nilijua elimu ndiyo mkombozi wangu wa pekee baadaye. Mwaka 2012 bibi alipatwa na presha, akafariki dunia. Nikabaki peke yangu pale nyumbani.”
“Nilijua ndiyo mwisho wa maisha yangu kwa vile niliamini sitasoma tena. Hapo sikuwa na wazo kwamba kuna kubwa zaidi linaningoja mbele, yaani hili la huu ugonjwa wa ajabu.”
 MWANAUME AJITOKEZA
“Mwaka 2014, nikiwa mtu wa kutangatanga kulekule Tanga, alitokea kijana mmoja, akanirubuni nikaishi naye kwake ili anioe. Nilimkubalia, sikuwa na jinsi. Nikiwa ndani ya uhusiano, nikapata mimba. Lakini mimba hiyo ikaenda sambamba na uvimbe. Ukawa unakua kwa kasi.
“Kuona hivyo, yule kijana aliondoka nyumbani. Nikawa sina mtu wa kunipeleka hospitali, sina pesa ya matibabu wala chakula.”
 MWANAUME HAPOKEI SIMU
“Siku moja niliamua kumpigia simu, akapokea lakini akaniambia hawezi kurudi nyumbani, nitafute pa kwenda. Nilikonda sana. Nikaanza kuomba nauli kwa watu, nilipopata nikaja Dar kwa rafiki wa mama anayeishi Chanika.
“Yule mama aliponiona na uvimbe alitokwa machozi. Pia  kutokana na afya yangu kwani nilikuwa na mimba kubwa huku uvimbe nao ukikua sana. Niliishi kama mnyama asiyepata matibabu.
“Sasa uvimbe ulikua kiasi kwamba, nilishindwa kuvaa suruali, magauni nayo yakawa yanatoa kinundu. Watu walianza kunishangaa. Usiku nashindwa kulala kwa maumivu makali.
 APELEKWA MUHIMBILI
“Rafiki wa mama anajishughulisha na biashara ya kuuza karanga kwa kufunga za miamia. Mume wake hana kazi, lakini alinichukua na kunipeleka Muhimbili. Walinichunguza na kuniambia inabidi nijifungue kwanza ndipo mambo mengine yaendelee.
“Februari 6, mwaka huu nikajifungua kwa njia ya upasuaji. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya kiafya. Madaktari wakaniambia nisimnyonyeshe mtoto. Ikawa gharama nyingine, kununua maziwa, pesa hamna kwani kuna wakati karanga hazinunuliwi.
“Mpaka sasa hivi nasubiri kama nitapatiwa matibabu na madaktari. Ingawa hata nikibahatika kupata matibabu sijui nitaishi vipi. Naumwa sana Watanzania wenzangu, naomba mnisaidie. Maisha yangu nayakabidhi mikononi mwenu,” alifunga kusema Faiza huku machozi yakimbubujika.
 BABA MLEZI ANENA
Baba mlezi wa Faiza, Mohamed Mrisho ambaye mke wake alimpokea Faiza, kwa upande wake alisema kwamba siku binti huyo alipofika kwake akitokea Tanga yeye hakuwepo nyumbani. Aliporudi alikuta ugeni huo huku binti akiwa amechoka na mwenye maumivu makali.
“Hamna jinsi, inabidi nikae naye ingawa na sisi hapa uwezo wetu kimaisha si mzuri. Mgonjwa huyu anahitaji mambo mengi ukizingatia ana mtoto mdogo ambaye anahitaji matumizi, pia mama yake anahitaji fedha ya matibabu. Nawaomba wasamaria wema wamsaidie kwa hali na mali,” alisema baba mlezi huyo.
 KUTOA NI MOYO
Kwa yeyote mwenye huruma na moyo wa kumsaidia Faiza, anaweza kutuma chochote kwa kupitia njia ya simu kwa namba; 0787 853153, 0654 187240 au 0717 260769.

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate