EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 11, 2015

MIMBA YA ZARI SI YA DIAMOND

OHOOO! Wakati Nasibu Abdul ‘Diamond’ akijinadi kwa mbwembwe kuwa anategemea kiumbe kutoka kwa mwandani wake Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’, ubuyu mpya wa mjini unadai kuwa mimba aliyobeba mrembo huyo si ya Diamond, Amani limemeza sababu za kutosha.
Mwandani wa mbongo fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho karibu na Diamond anayesumbua kwa sasa na wimbo wake wa Nana, tangu habari ya ujauzito wa mlimbwende huyo mwenye asili ya Uganda ianze kupamba vyombo mbalimbali vya habari, watu walio karibu na staa huyo hawakuziamini.
“Hatukuamini sababu kwanza muda ambao Diamond alikutana na Zari ulikuwa mchache ukilinganisha na miezi mitatu ambayo mimba ilibainika. Watu wa karibu tulikuwa tunajua lakini tulikuwa tunashindwa pa kuanzia kusema.
MITANDAO YAWASAIDIA
“Sijui bwana nani alivujisha hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii ndiyo maana hata sisi sasa tukawa radhi kufunguka. Tena imeeleza mambo ya ukweli tupu ambayo sisi tulikuwa tunayajua,” kilisema chanzo chetu.
IMESEMAJE MITANDAO?
Watumiaji mbalimbali wa mitandao ya kijamii wametoa maoni kuwa, kwa asilimia 90 mimba ya Zari si ya Diamond na kuna uwezekano ana tatizo la uzazi kwani hata mpenzi wake wa zamani, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ aliwahi kukaririwa akisema Diamond hajampa ujauzito kama yeye alivyokuwa akijisifia kuwa amempa halafu ukatoka.
Diamond akibusu tumbo la Zari.
ANA TATIZO?
“Yawezekana ana matatizo. Haiwezekani aseme amempa mimba Jokate akaitoa halafu mwenyewe akatae. Kama mnakumbuka hata alipomwagana na Penny (Penniel Mungilwa), alisema ametoa mimba yake kitu ambacho mrembo huyo alikikanusha na kumtaka kama kweli ana ushahidi wa hospitali aliyoitumia kutoa mimba ampe,” alieleza mdau mtandaoni.

MWINGINE AKUMBUSHIA YA MUME WA ZARI
Kama hiyo haitoshi, mchangiaji mwingine katika mitandao hiyo ya kijamii alishibisha hoja ya mimba ya Zari si ya Diamond kwa kukumbushia suala la aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwaga kufunguka kuwa kamwe Zari hawezi kumzalia Diamond.
“Mume wa Zari alikuwa anaujua ukweli wa mimba ya Zari (huenda ni yake) ndiyo maana alinukuliwa katika vyombo mbalimbali vya habari pasipokuwa na shaka yoyote, kama hamuamini, akijifungua kipimo cha DNA kitamaliza ubishi,” alichangia mtu huyo.
Zari akiwa na Katunzi.
KATUNZI ATAJWA
Ushahidi wa mimba hiyo kuwa si ya Diamond ulizidi kumwagwa mtandaoni kuwa Diamond hakuwa mtu wa kwanza kuonana Zari kwani alitanguliwa na mfanyabishara maarufu Bongo, Mzamili Katunzi ambaye inasemekana ndiye aliyemfata Bongo kisha baadaye akakutana na Diamond.
“Mtu akiniambia hiyo mimba ni ya Katunzi naweza nikakubali sababu ndiyo mtu wa kwanza kukutana na Zari lakini Diamond hana chake pale, si unakumbuka Global (Kampuni ya Global Publishers) waliwahi kutoa picha ya zamani ya Katunzi akiwa na Zari? Tujiongeze,” alichangia mchangiaji mwingine mtandaoni.
KATUNZI ANASEMAJE?
Mwanahabari wetu alimtafuta Katunzi kujua anazungumziaje kutajwa kwenye ujauzito huo ambapo alijibu kwa kifupi:
“Nani kawaambia? Hivi si mnajua mimi nina familia yangu? Kwa nini msimuulize mama kijacho mwenyewe (Zari). Mama mtoto ndiye anayejua ukweli wote.”
DIAMOND SASA
Kwa upande wake Diamond alipotafutwa na mwanahabari wetu juu ya habari hiyo, alisema maneno kwamba mimba si yake si mageni lakini hayatilii maanani sababu hayana ukweli wowote.“Watu tu wenye roho mbaya ndiyo wanaongea maneno hayo, ninavyojua mimi tumbo lile linanihusu kwa asilimia mia moja,” alisema Diamond.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate