EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 23, 2015

Chadema yaja na mbinu mpya kudhibiti mamluki

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya Magomeni, Jijini Mwanza.
 Mbunge wa Kahama Mjini, James Lembeli (kushoto) akiwa na Ester Bulaya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mara
“Mwaka huu hakuna kupita bila kupingwa, wagombea wetu wote tutawasainisha mahakamani na wakishindwa kurudisha fomu, tutawashughulikia mahakamani,” amesema Dk. Slaa na kuongeza;
“Waliochukua fomu hatutaki kesho mmoja amejitoa, kama unataka kujitoa ondoka leo, ruksa.”
Mkutano huo umehudhuriwa na wabunge na viongozi mbalimbali wa chama hicho akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Makamu Mwenyekiti Bara, Prof. Abdallah Safari; Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA), Halima Mdee.
Katika mkutano huo, wanachama wapya kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) walitambulishwa, wanachama hao ni James Lembeli aliyekuwa Mbunge wa Kahama Mjini na Ester Bulaya ambaye alikuwa Mbunge Viti Maalum kutoka Mkoa wa Mara.
Kwenye mkutano huo Dk. Slaa amesema, sasa hivi Chadema ipo sehemu yote ya nchi hivyo hakuna mahali ambapo chama hicho kitashindwa kusimamisha mgombea na kwamba, Ijumaa wiki hii watamaliza uteuzi kwenye majimbo yote Tanzania.

“Leo tumeingia kila kona ya nchi, uchaguzi uliofanyika wiki hii ni wa Tanzania nzima, hakuna mahali ambapo Chadema haipo tena, hatuzungumzi kabila, hatuzungumzi Magufuli ni mkabila, sehemu zote tunazungumza Utanzania,” anasema Dk. Slaa.
Akizungumzia mahudhurio ya wananchi kwenye mkutano huo Dk. Slaa amesema, miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo hakuna aliyelipwa fedha wala kubebwa na magari kutolewa kule alikokuwa.
“Hakuna aliyebebwa, hakuna aliyelipwa pesa, mmekuja hapa kwa miguu yenu tangu asububi, asanteni sana na Mungu awabariki,” amesema Dk. Slaa.
Hata hivyo amesema, ukiumwa na nyoka hata utapoguswa na jani utalikimbia. Aliwafikirisha wananchi kwa kujiuliza, katika miaka 10 iliyopita, Watanzania walikuwa wanakunywa chai huku sukari ikiuzwa Sh. 500, je leo nani anaweza kunywa chai kwa sukari bei hiyo?
Pia aliwakumbusha kuwa, miaka 10 iliyopita ikiwemo wafugaji waliweza kula nyama, leo bado wanaweza kula kula kilo ya nyama?
Dk. Slaa amesema, mwaka 2005 wakati Rais Jakaya Kikwete akiwa mgombea urais kupitia CCM, aliwaahidi Watanzania Maisha Bora kwa Kila Mtanzania lakini sasa maisha yamekuwa magumu kwa kila Mtanzania.
Hata hivyo amesemea, mgomea wa CCM ni mzaliwa wa ukoo ule ule na kabila la CCM hivyo kuna kila sababu ya kuwaonda.
Pia amesema, “tumekuja leo ili tuwaeleze kwamba Chadema tupo makini, kazi za chama hazisimami, tupo kwenye utekelezaji wa kazi za chama.
Hata hivyo, amewaahidi wananchi kuwa, wakati utakapofika “tutadondosha nondo zetu.”
Dk. Slaa amewahahakikishia wananchi kuwa, chama hicho hakiwezi kumeguka wala kusambaratika licha ya kuwepo kwa taarifa kwamba, yeye na Freeman Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho hawasalimiani,
Kwa kujiamini kiongozi huyo amesema, wamejihakikishai kushika dola, “haya sio maneno wala utani.”
Msukumo mkubwa wa maisha Dk. Slaa amesema unatokana na mabadiliko ya uchumi ulio mbovu kwa miaka zaidi ya 50 baadaya Uhuru uliopatikana mwaka 1961.
Amefafanua kuwa, wakati wa Rais wa Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, uamuzi ulianza matawini kwenda juu lakini sasa CCM imebadilisha na kuwa uamuzi wa kundi la watu wachache dhidi ya wananchi walio wengi.
“La kwanza tunalolisimamia ni nchi irudi kwa wananchi, ukifanya hivyo yote yanaondoka; ufusadi, wizi rasilimali vyote vitakoma.
“Mkikabidhi nchi kwa wachache hiki ndicho kinatokea, mwaka 2015 ndio mwisho. Katiba inasema serikali itapata madaraka yake kutoka kwa wananchi, CCM imepoka,” amesema.
Akizungumzia ukombozi Dk. Slaa amesema, nchi inahitaji ukombozi na wananchi wapo tayari katika ukombozi na kuwa, Polisi, Wanajeshi na wengine ni watiifu na ndio maana wanawapenda na wanaungana nao katika safari ya ukombozi ambapo vyombo hivyo vitaendelea kuwepo, hofu kuwa upinzani unaleta vurugu haipo tena.
Katika mkutano huo, Mbowe amewatoa hofu wananchi kwamba, Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) uko imara, hadi atakapopatikana rais.
Aidha, Mbowe alianza hotuba yake fupi baada ya kuwakabidhi kadi za uanachana Bulaya na Lembeli.
“Hamtakiwi kuendelea kusikiliza maneno ya uzushi ambayo yanasemwa UKAWA umevunjika au kusambaratika, hayo sio kweli na kuhakikishieni hilo, hadi leo asubuhi nimewasiliana na viongozi wezetu wa UKAWA.”
Amesisitiza kuwa, wananchi hawatakiwi kusikiliza maneno ya nje bali wawasikilize viongozi wao, kwani umoja wao bado unalengo lile lile la kuiondoa CCM madaraka.
Amesema, UKAWA bado wanaendelea na mazungumzo ya amani na kwamba, bado wanamalizia mambao madogo ili wote waende sawa na kutoka na mgombea mmoja “Agosti 4 mwaka huu tutatoa taarifa ya nani rais.”
Hata hivyo amesema, jambo la kwanza ambalo UKAWA italishughulikia ni kurudisha viwanja vyote ambavyo ni mali ya wananchi na sasa vipo chini ya CCM.
Lakini pia amepiga marufuku mausula ya ukabila na kushangazwa katika Karne hii ya 21 kuwepo wapo kwa watu wanaozungumzia ukabila.
Akizungumzia ukabila, alijaribu kuiga sauti ya Mwl. Nyerere ambaye katika hotuba zake alizokuwa akizungumzia ubaya wa kuubeba ukabila katika nchi hii.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate