EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 18, 2015

HATIMAYE WEMA AMWANGUKIA KAJALA

wema (8)
Staa wa filamu za bongo, Wema Sepetu ‘Madam’.
Musa mateja
HAKUNA mwanzo usiyokuwa na mwisho! Huu ni usemi pekee ambao umejidhihirisha kwa Mkurugenzi wa Endless Fame Production na mbunge mtarajiwa wa Viti Maalum mkoani Singida kwa leseni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wema Isaac Sepetu baada ya kumwangukia aliyekuwa shostito wake, Kajala Masanja ‘Kay’.
MWISHO WA MATUSI?
Wema na Kajala wamekuwa na bifu zito lililokuwa likichukua sura mpya kila kukicha kufuatia wawili hao kutokusameheana, kutukanana na kukashifiana ambapo Wema alifikia hatua ya kumwita mwenzake ‘bogasi’ na yeye (Kajala) akamwita chizi.
Tukio la Wema kujishusha na kutoa kauli ya kusema yuko tayari kumsamehe Kajala aliitoa mbele ya mwandishi wetu, Julai 15, mwaka huu ndani ya Ofisi za gazeti hili, Bamaga-Mwenge jijini Dar.

masanja1Kajala Masanja ‘Kay’.
WEMA AFUNGUKA
Wema alifunguka hayo baada ya kuulizwa hatima ya bifu lake na Kajala  ambapo alisema kwa sasa yupo tayari kabisa kumsamehe Kajala ambapo aliapa kwamba hata ikitokea wakutane popote hawezi kumuonyeshea kinyongo cha aina yoyote.
Alisema pamoja na kushindwa kukutana na Kajala kwa muda mrefu lakini nafsi yake imeshamsamehe na imemuongoza kufanya hivyo.
Wema alisema kuwa kila jambo lina mwisho wake, hivyo amekaa chini na kufikia uamuzi huo ambao anaamini kabisa hapa duniani hakuna mtu asiyekuwa na moyo wa huruma.
Aliongeza kuwa pamoja na yote yaliyotokea awali, hana budi kuyapuuzia kwa sasa, hivyo yuko tayari kukutana na kukaa na Kajala  kwani moyoni hana kinyongo chochote.
wemanakajalaKajala na Wema wakipozi pamoja.
SINA TATIZO NA KAJALA
“Kiukweli kabisa nimeshamsamehe Kajala, sina tatizo naye, hivyo muda wowote akinihitaji kwa lolote sina kinyongo kabisa.
“Nimefikiria kwa kina, nikaona sina sababu ya kuendelea kuwa na chuki naye na kupitia hilo namuomba Mungu aendelee kuniongoza ili nifute kabisa hilo wazo la chuki moyoni.
“Nipo radhi kukutana naye mahali popote pale endapo atanihitaji au mimi nitakapomuhitaji nitamtafuta,” alifunguka staa huyo na kuongeza:
KUTOKA MOYONI
“Najua itakuwa ngumu sana kwa watu kuniamini kwa sababu hapo nyuma kulikuwa na mambo mengi kati yetu, naendelea kuwatoa wasiwasi kwa kuwaambia tena kuwa tayari moyo wangu umeshamsamehe Kajala na nimejishusha kwa kila hali kwake.
“Nipo radhi kukutana naye mahali popote tukaongee ili wale wanaohisi sijamsamehe waamini hilo.”
Baada ya paparazi wetu kuhakikishiwa taarifa hiyo na Wema kwa kauli za kumsamehe zaidi ya mara moja huku akionyesha unyenyekevu na kujishusha kwa asilimia mia, alimtafuta Kajala ili kujua moyoni mwake ana nini juu  ya Wema.
KAJALA ROHO KWATU
“Kwanza nashukuru kusikia hivyo, binafsi sina tatizo na hilo, kikubwa namshukuru maana nimekuwa nikimuomba Wema kupitia sehemu mbalimbali ili tumalize tofauti zetu lakini alikuwa akikataa, ila kama mwenyewe anasema yupo tayari tuyamalize, kwangu ni furaha.
“Nimekuwa nikipigania hilo kila kukicha, sasa naamini Mungu atakuwa amesikia kilio changu kwa mara nyingine, napenda kusema sina tatizo lolote katika hilo,” alisema Kajala.
WEMA ACHUKUA FOMU YA UBUNGE
Msamaha huo umekuja siku moja kabla ya Wema kuchukua fomu ya kuwania Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Mjini kupitia CCM ambapo juzi Julai 15, mwaka huu alichukua fomu na anatarajia kuirejesha kesho Jumapili.


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate