EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 21, 2015

Hali tete Bunda, viongozi Chadema wajiuzulu



bulaya
SIKU chache baada ya mgombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya kuteuliwa na chama hicho na kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo, hali ndani ya chama hicho wilayani  Bunda imekuwa tete.
Hatua hiyo inatokana na uamuzi wa aliyekuwa mpinzani wa Bulaya katika kura za maoni ndani ya chama hicho, Pius Masururi, kujitoa katika chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tayari Masururi ametangaza kumuunga mkono Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira katika mbio za ubunge huku viongozi 11 wa Chadema katika jimbo hilo wakisimamishwa uongozi.

Inaelezwa kuwa sababu ya kusimamishwa kwa viongozi hao kunatokana na kile kilichodaiwa kuwa kusimamisha wagombea mamluki katika nafasi ya ubunge na udiwani.
Akizungumza jana mjini hapa kupitia Redio ya Kijamii ya Mazingira FM,  Masururi alitangaza kujiunga na CCM jana muda mfupi kabla ya kuondoka na kurejea jijini Nairobi nchini Kenya.
Alisema Kamati Kuu haikutenda haki kwa kumteua  Esther Bulaya na kumwacha yeye ameshinda katika kura za maoni licha ya kushiriki kwake kukijenga chama hicho kwa kipindi cha miaka minne.
Kutokana na hali hiyo, Katibu wa Chadema Wilaya ya Bunda, Rita Ikandire kwa niaba ya viongozi wanzake wanaotuhumiwa kukihujumu chama hicho wametangaza kujiuzulu nafasi zao za uongozi huku wakidai ofisi ya katibu wa Mkoa wa Mara na Taifa wamevunja katiba ya chama hicho.
“Mimi pamoja na viongozi wa jimbo na kamati  ya utendaji Jimbo la Bunda tumejiuzulu baada ya kutoridhika na  uamuzi wa Kamati Kuu lakini pia baadhi ya makatibu na wenyeviti katika  kata 20 za jimbo hili wamejiuzulu na watabaki kuwa wanachama wa kawaida wa Chadema,” alisema Rita.
Waliotangaza kujiuzulu mbele ya waandishi wa habari ni pamoja na Alfred Imanani(Mwenyekiti wa Jimbo), Emmnuel Malibwa(Katibu Mwenezi),  Dickson Kujerwa(Mwenyekiti BAVICHA), David Abogast (Mjumbe Kamati  ya Utendaji), Mwenge Webiro (Katibu BAWACHA jimbo) na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa,  Juma Omari.

Wengine ni Ng’wena Mwita (Mwenyekiti Baraza la Wazee jimbo), Damas Kunju, Kibago Kibago(Red Brigedia Mkuu) ambao wote wamedai kujiuzulu na kubaki wanachama wa kawaida.
Wakati viongozi hao wakidai kujiuzulu, mmoja wa kiongozi wa Chadema, Kaunya Yohana, alisema viongozi 11 tu ndio wamesimishwa uongozi na chama baada ya kupandikiza wagombea wasiokuwa na sifa.
“Viongozi hao hawakujiuzulu kama wanavyodai isipokuwa wamesimamishwa uongozi mpaka mambo yatakapokuwa sawa tangu tarehe 15/8/2015,” alisema Yohana.
Alisema viongozi hao wamesimamishwa kwa barua yenye kumb. Na.C/HQ/ADM/KK/08 ya tarehe 19/08/2015 iliyosainiwa na Julius Mwita Katibu wa Vijana Taifa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Chadema Taifa.
Aliwataja  baadhi ya waliosimamishwa kuwa ni pamoja na Alfred Imanani, Rita Ikandiro, Emanuel Malibwa, Damas Kunju, Dickson Kujerwa, David Abogast, Matara Athumani na Noa Laurent.
Alisema wakati viongozi hao wakitumikia adhabu hiyo chama kimeunda nguvu kazi itakayosimamia shughuli zote za chama na kuratibu mchakato mzima wa uchaguzi katika majimbo matatu ya Bunda Vijijini, Bunda Mjini na Mwibara.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate