EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 27, 2015

Siri 4 matusi ya Diamond kwa Diva


diva
Loveness Malinzi ‘Diva’
NI mtifuano! Agosti 24, mwaka huu ilikuwa siku mbaya kwa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah na mtangazaji anayekimbiza kwa sauti tamu hewani, Loveness Malinzi ‘Diva’ kufuatia kupishana lugha ndani ya studio za redio na hivyo, Diamond kumvurumishia matusi mwenzake.
Kupishana kauli huko kuliashiria kuwepo kwa uhasama wa siku nyingi kwa wawili hao huku kila mmoja akiwa anaamini mwenzake ana makosa na ndipo siri tano za Diamond kumtusi Diva zikajulikana.
MCHEZO ULIVYOANZA
Siku hiyo majira ya saa 9:00 alasiri, Diamond alitia timu kwenye studio za redio hiyo zilizopo Mikocheni, Dar kwa lengo la kumtambulisha msanii wake mpya kutoka studio yake ya Wasafi Records iliyopo Sinza-Mapambano, Dar.Mwanyeji wa Diamond alikuwa mtangazaji Hamis Mandi ‘B12’. Lakini ndani ya studio hiyo alikuwepo Diva.
platnumz
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah.
ALIANZA DIAMOND
Kabla Diamond hajaanza kumtambulisha msanii wake, alianza na Diva kwa kumsema kwamba amekuwa akimchoresha mitandaoni kwa kumchafua.
DIVA AKAJIBU
Diva alijibu kuwa, kisa cha yeye kumchoresha, aliwahi kumuita Diamond kwenye Kipindi cha Ala za Roho lakini staa huyo hakutokea wakati meneja wake, Salam alimpa taarifa, akakubali na yeye Diva akaanza kutangaza mitandaoni kuwa, siku moja atakuwa na Diamond hewani jambo lilimfanya wasikilizaji wake kusema aliwaongopea na wengine kuanza kumtusi mitandaoni.
DIAMOND ACHAFUA HALI YA HEWA
Baada ya maneno hayo ya Diva, ndipo Diamond apoonesha dalili ya kukasirika na kutoa lugha ya matusi ambayo haiandikiki gazetini lakini akimaanisha kuwa, kama Diva angewahi kuwa mpenzi wake, angemheshimu.
MANENO BILA MPANGILIO
Diva naye alijimjia juu Diamond kwa kumwambia kuwa, hana hadhi ya yeye kuwa mpenzi wake, maneno ambayo yalimchefua baba Tiffah na kuanza kutupiana maneno bila utaratibu hali iliyomlazimisha B12 kuingiza matangazo ili kuwatoa hewani wawili hao.
Baada ya sitofahamu hiyo, Amani lilichimba na kubahatika kuibuka na siri nne (4) zilizomfanya Diamond kumtukana Diva.
SIRI YA KWANZA
Kwanza inadaiwa kuwa, meseji za Diva kwenye mitandao kumsema Diamond kwa kitendo chake cha kutotokea kwenye Kipindi cha Ala za Roho zilimfanya mzazi mwezake, Diamond, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kumbana baba wa mtoto wake huyo akimtaka aseme ukweli kama kuna siri iliyofichika kati yao
“Diamond amekuwa akimkatalia Zari kuwa, hakuna siri wala uhusiano wake na Diva. Kwenye kipindi hicho kama Diamond angekwenda, ilikuwa aongozane na Zari maana alikuwa hajajifungua. Diamond akawa anamwona Diva kama ana lengo la kuvuruga mapenzi yao.
SIRI YA PILI
“Kitendo cha Diva kutumia mitandao kumshambulia, Diamond alikiweka moyoni na kuahidi siku wakikutana laivu atampasulia ya moyoni mwake liwalo na liwe. Hata alipokwenda studio jana (Jumatatu), hakujua kama angekutana na Diva.”
SIRI YA TATU
“Diamond aliamini kuwa, Diva kumshambulia mitandaoni alilenga kumshushia heshima mbele ya jamii ili kumuua kisanii. Maana yeye mwenyewe alisema anaamini maneno ya Diva kwenye mitandao kuna zaidi ya kitendo chake cha kutotokea studio,” kilidai chanzo chetu.
SIRI YA NNE
Kwa upande wake, Diamond alipozungumza na Amani alianika siri ya nne akisema:
“Yule Diva dizaini f’lani kama ananitaka vile lakini mimi simpi nafasi ndiyo maana anatengeneza bifu na mimi.”
DIAMOND ANAENDELEA
“Diva amekuwa akinisema mara kwa mara. Mimi nilikwenda pale kwa lengo lingine, yeye akaanza kuleta zake za kuleta. Kila nikiitafuta sababu siioni. Sijawahi kumkosea popote pale.”
DIVA TAYARI KWA MWANASHERIA WAKE
Amani lilimtafuta Diva juzi kwa lengo la kumsikia anasemaje kuhusiana na sakata hilo ambapo alisema:
“Hii ishu iko kwa wanasheria wangu (tayari kwa kumpeleka Diamond mahakamani). Amenidhalilisha sana kama mwanamke nisiyefaa katika jamii. Ushahidi upo kila kona kwenye mitandao.”
ATISHIWA KUPIGWA, MAISHA
“Akaenda mbali zaidi na kutaka kunipiga maana lugha ya matusi haikutosha. Amenitishia maisha jambo ambalo halitakiwi kisheria. Hakuna aliye juu ya sheria. Sitazungumza zaidi.”
Imeandaliwa na Musa Mateja na Nyemo Chilongani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate