EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 19, 2015

Lulu amchokonoa Zari

lulu-na-diamondMwandishi Wetu
UCHOKOZI! Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ëLuluí anatengeneza kichwa cha habari kwa mara nyingine baada ya kudaiwa ‘kujibebisha’ kwa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ëDiamond Platnumzí, kitendo kilichotafsiriwa kuwa ni kumchokonoa mwandani wa jamaa huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
Tukio hilo lilijiri usiku mnene Jumapili iliyopita kwenye Ukumbi wa House Club uliopo Masaki, Dar ambapo kulikuwa na sherehe ya ëbethdeií ya DJ wa Diamond, Rommy Jones.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyeweka kambi ukumbini humo, Lulu, bila kujali kwamba, Diamond alimwacha Zari nyumbani akimnyonyesha ‘baby girl’ wao, Latifah Nasibu a.k.a ‘Princess Tiffah’, alionekana akijiachia naye kimahaba huku akionesha ‘kummisi’ kinoma jamaa huyo.
rommmmILIANZA HIVI
Lulu, alikuwa wa mwishomwisho kuingia ukumbini ambapo baada ya kuzunguka kusalimiana na mastaa wengine alitua kwenye sofa alilokuwa amekaa Diamond ambapo walianza kufanya yao bila kujali ëwavimba machoí waliokuwa wakiwakodolea.
Kwa kuwa Diamond alikuwa host (mwendeshaji) wa shughuli hiyo, Lulu alikuwa akimwaga mauno huku akimshangilia Diamond kufuatia muziki wake wa nguvu uliokuwa unarindima ukumbini humo.

Kutokana na hali hiyo, Lulu aliendelea kucheza zaidi kwa madai kwamba anaupenda mno muziki wa Diamond hasa ulipodondoshwa ule wa Mdogomdogo.
mondandzarinewWAONESHANA MAHABA
Ilifika wakati Diamond alionekana akimpiga Lulu busu mdomoni huku watu wakishangilia ëoyoooí lakini wao hawakuwa wakijali chochote kwani waliendelea kufanya yao.
Kuna wakati walikuwa wakitaniana na kucheka huku wakigongesha glasi zao za mvinyo na kukumbushana mambo mbalimbali ya siku za nyuma.
Baadhi ya watu walisikika wakisema kwamba, Lulu anamchokonoa mama Tiffah ‘Zari’ kwani kwa usiku huo yeye alikuwa tu nyumbani akinyonyesha wakati baba mtoto wake akijiachia na kimwana huyo.
“Naona Lulu anatafuta matatizo kwa Zari kwani mahaba wanayooneshana hapa ukumbini siyo ya kawaida, yaani hawa mastaa wetu mbona majangaaa,” alisikika mmoja wa wahudhuriaji wa shughuli hiyo iliyokuwa ya kistaa kwani hakukuwa na ‘watoto wa mbwa’.
SHETTA AMWAGA FEDHA
Katika sherehe hiyo ilipambwa na mastaa kibao wa fani mbalimbali na mapedeshee wa mjini, walimmwagia Rommy mvua ya fedha huku mwanamuziki, Nurdin Bilal ‘Shetta’ akimzawadia fedha taslimu Sh. milioni moja ambapo shughuli iliendelea hadi majogoo.
Wakati hayo yakitendeka mmoja wa marafiki wa karibu wa Zari alimtumia ujumbe mfupi wa maneno (sms) kumfahamisha juu ya tukio hilo.
MASTAA KIBAO
Ukiacha Lulu na Shetta, baadhi ya mastaa wengine waliojiachia vya kutosha ni pamoja na Aunt Ezekiel na baba mtoto wake, Moses Iyobo, dada wa Diamond, Mwajuma Abdul ‘Queen Darleen’, Khaleed Mohamed ‘TID Mnyama’, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ sambamba na Juma Musa ‘Jux’, Hamad Ally ‘Madee’, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na wengine kibao.
LULU ANASEMAJE?
Akizungumzia hali hiyo, Lulu alisema kuwa ilikuwa ni pati na kupiga picha na Diamond haikuwa ishu kubwa kwani ni watu wengi waliopiga naye picha.
“Siamini wala sihisi kama Zari anaweza ‘kumaindi’ ishu kama hiyo. Kama akimaindi atakuwa na lake jambo,” alisema Lulu.
TUJIKUMBUSHE
Kabla ya tukio hilo, Lulu aliwahi kudaiwa kutoka na Diamond lakini alikanusha vikali ishu hiyo huku akionesha kuwa jamaa huyo hana ubavu wa kumsogelea wala kufaidi penzi lake.

CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate