EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 4, 2015

SLAA NI SHUJAA WA TAIFA

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dokta Wilbroad Slaa.
Na Amran kaima
HOTUBA ya kwanza tangu ‘atoweke’ kwenye anga za siasa ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dokta Wilbroad Slaa, aliyoitoa juzi Jumanne juu ya kujiweka pembeni, imepokelewa kwa hisia tofauti huku wengi wakimuita kuwa ni shujaa wa taifa kutokana na ujasiri wake, Ijumaa lina kila kitu.
Katika mahojiano yaliyowahusisha wananchi na wachambuzi mbalimbali wa mambo ya kisiasa kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mara baada ya kiongozi huyo kukutana na waandishi wa habari, waliliambia Ijumaa kuwa, Dokta Slaa ni mtu wa aina yake ambaye taifa halijapata kuwa naye tangu kuondoka kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Mhe. Freeman Mbowe.
Ana msimamo
Wengi walionesha kufurahishwa na misimamo ya kiongozi huyo tangu ajiingize kwenye masuala ya siasa, kwani siku zote amekuwa mstari wa mbele kuwatetea wanyonge, kuanika maovu na kukemea kila analoliona lipo tofauti na anavyoamini.
“Kwa kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Dk. Slaa ni kati ya viongozi wenye msimamo asiyekubali kuyumbishwa. Amekuwa hivyo tangu nilivyomjua na hata hotuba yake aliyoitoa juzi, inadhihirisha hilo,” alisema Chande Juma wa Kinondoni jijini Dar.
Alisema kama mtu alifuatilia vizuri mazungumzo yake, ni wazi kuwa viongozi wenzake walikubali kubadili msimamo ili kumwezesha Lowassa aingie Chadema, lakini yeye akakataa licha ya kamati ndogo kuundwa ili imshawishi alegeze msimamo.
Mgombea urais kupitia Chadema(Ukawa) Edward Lowassa.
Rushwa ni adui mkubwa kwake
Mchambuzi mmoja wa habari za siasa aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema siku zote anamtambua Dk. Slaa kama mtu mwenye kuichukia rushwa, kwani anaamini hicho ndicho chanzo cha matatizo yote yanayosababisha kero za wananchi kutoisha, licha ya nchi kuwa na rasilimali za kutosha.

“Unampata wapi sasa hivi aina ya kiongozi ambaye anaweza kukataa rushwa ya shilingi milioni 500 akitetea masilahi ya wananchi masikini? Viongozi wetu wa sasa kila mtu anaweka mbele masilahi yake na familia yake, suala la kuwatetea wanyonge wanalifanya kama maigizo tu,” alisema mchambuzi huyo, akikumbushia jinsi mbunge huyo wa zamani wa Karatu alivyokataa kiasi hicho cha fedha ili ashiriki kuzuia ripoti ya Kamati ya Bunge juu ya sakata la Richmond isisomwe bungeni.
Maneno kama hayo yalisemwa pia na mkazi mmoja wa Sinza, Nicholaus John akirejea jinsi alivyokataa rushwa ya uongozi pale alipoahidiwa kazi nje ya nchi, ilimradi tu akubali kuachia ubunge wake katika Jimbo la Karatu.
Kwake ni taifa kwanza
Kitendo chake cha kueleza kuwa alitumia sehemu kubwa ya mshahara wake kumpa mkewe ili afanye ziara ya kuzunguka nchi nzima katika harakati za kukijenga chama, ni kielelezo kuwa kiongozi huyo anajali ustawi wa taifa kwa namna anavyoamini kuliko maisha binafsi ya familia yake.
“Slaa amekuwa akitanguliza masilahi ya taifa kwenye siasa zake, kama mtu anakubali yeye na familia yake wale mihogo na maharage ili kipato chao kitumike kwenye mambo ya siasa, unadhani ana uchungu kiasi gani na taifa hili?” alihoji Mama Saidi wa Mwananyamala jijini Dar.
Kuweka maisha yake rehani
Kitu kingine kinachofanya wananchi wengi kumuona Dk. Slaa kuwa ni shujaa wao ni kitendo chake cha kukubali kuweka maisha yake rehani, ilimradi tu mambo makubwa na muhimu ya nchi yanasemwa hadharani na kila mmoja ayasikie.
“Ni nani atakuwa tayari kufa kwa kuwataja watu majina kwenye uovu, tena watu hao ni vigogo wenye fedha na mamlaka ambao wanaweza kumfanya lolote. Fikiria kitendo chake cha kutaja majina ya mafisadi papa wakati ule. Huu ni ujasiri wa aina yake,” alisema Liffa Jason, mwenyeji wa Shinganya aliye Dar kibiashara.Walisema Dk. Slaa alifanya hivyo akijua yeye binafsi hafaidiki na lolote, lakini aliweza kuwataja ili kuwafunua wananchi wawajue watu wanaoitafuna nchi yao.
Hana tamaa
Kingine kilichoelezwa na watu hao ni kwamba kiongozi huyo hana tamaa ya fedha wala madaraka, kwani alikubali kuacha ubunge, wenye mshahara na marupurupu mengi na kwenda kufanya kazi ya kukijenga chama, kitu ambacho alifanikiwa kwa kiwango kikubwa.
Lakini kikubwa zaidi, wamedai kwamba Dk. Slaa angeweza kunyamaza kimya na kufanya kazi ya kumnadi Lowassa, kwani kwa vyovyote mwisho wa siku angepata kuteuliwa katika nafasi kubwa na nyeti serikalini.
“Kiukweli hana tamaa, naamini angekaa kimya na ukatibu mkuu wake wa chama, bado maisha yake yangekuwa mazuri, kaamua kujiweka pembeni bila kujali athari atakayoipata ili tu asikumbatie mafisadi ndani ya Chadema,” anasema Elika wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Apewe ulinzi
Kwa kuzingatia mambo yote yanayoendelea katika maisha yake ya kisiasa, wananchi waliozungumza suala hili walitaka kiongozi huyo ambaye sasa yuko nchini Italia kupewa ulinzi, kwani kazi yake kubwa kwa nchi inawakera watu wachache wanaoweza kumdhuru kwa namna yoyote.
“Unajua tangu siku alipoongea na kuwalipua viongozi wa Ukawa, ni lazima kutakuwa na vitisho, wengine wamemtukana na kudai kajidhalilisha, lakini ukweli unabaki palepale kuwa yeye ni shujaa na anastahili ulinzi ili wasitokee wa kumdhuru,” alisema Modesta George wa Oysterbay jijini Dar na kuongeza:
“Lakini pia kwa kila mwenye mapenzi na nchi ya Tanzania, anayechukia ufisadi, rushwa na uonevu ndani ya vyama vya siasa anayeona kuwa alichokifanya Slaa ni kitendo cha kishujaa, tuungane kumuombea ili Mungu amuepeshe na balaa.”
Aibomoa VIBAYA Ukawa, aacha majeraha
Kitendo chake cha kutoa maneno makali kwa viongozi wenzake wa Chadema na Ukawa, kimesababisha majeraha kwa umoja huo, kwani viongozi sasa wamegawanyika juu ya nani ni mkweli kati ya yanayosemwa kuhusiana na sakata zima la Dk. Slaa.
“Dk. Slaa ametuacha njia panda, sasa kama yeye alikataa kumkaribisha fisadi bila kutimiza masharti, lakini wenzake wakafanya ina maana sisi sasa tushike lipi?” alihoji Bruno Kei wa Tegeta Kibaoni.
Slaa vs Chadema, Lowassa
Siku moja baada ya Dk. Slaa kutoa hotuba yake hiyo iliyowasisimua mamilioni ya Watanzania wenye uchungu na nchi yao, baadhi ya viongozi wa chama chake wameibuka na kumtetea mgombea wao, Edward Lowassa wakisema kilichotokea katika kumkaribisha kiliridhiwa na pande zote, akiwemo katibu huyo.
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu akihojiwa na BBC, alisema Dk. Slaa ni mwongo, kwani kama kulikuwa na masharti yoyote ambayo yeye aliweka kwa ujio wa Lowassa, basi yeye alipaswa kushirikishwa kama mtu wa sheria, kitu ambacho hakikuwahi kufanyika.
Naye Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia akijibu madai ya Dk. Slaa, alidai kuwa alichokisema Dokta Slaa ni siasa nyepesi zinazoonyesha kushindwa.
“Tupambane kwa hoja badala ya uchochezi kwa sababu sisi sote tutapita ila nchi yetu itabaki, maneno yote ya Dk. Slaa yalijaa uchochezi ila kwa kifupi ni kwamba, sisi katika Ukawa tupo pamoja na tunamuunga mkono mgombea wetu.”

CHANZO; GLOBALPUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate