Mkurugenzi
 Mtendaji wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka 
na wenzake wawili wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na mashtaka sita 
yakiwamo ya matumizi mabaya ya madaraka, kughushi na kuisababishia 
hasara Serikali kupitia ukodishaji wa ndege. 
Wakili
 Mkuu wa Serikali, Timon Vitalis akishirikiana na mawakili wa Takukuru, 
Joseph Kiula na Stanley Luoga waliwataja washtakiwa wengine 
wanaokabiliwa na kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage
 kuwa ni Ofisa Mtendaji Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi 
ya Umma (PPRA), Ramadhan Mlinga na Mwanasheria wa mamlaka hiyo, Bertha 
Soka.
Wakili
 Vitalis alidai kuwa Oktoba 9, 2007 katika ofisi za ATCL zilizopo 
wilayani Ilala, Mattaka alitumia vibaya madaraka kwa kutia saini mkataba
 wa ukodishaji wa ndege A320-214 iliyotengenezwa kwa namba 630 baina ya 
Wallis Trading Inc na ATCL. 
 
 
 
 
 
 
 

 
 Husna Maulid.
Husna Maulid. Hamisa Mobeto akiwa na Mkongo.
Hamisa Mobeto akiwa na Mkongo.