EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 26, 2013

CHOMBEZO: KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA.....SEHEMU YA...04.

Na Irene Mwamfupe Ndauka
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
“Umefunga geti kwa kufuli kweli wewe Fuko?”
“Ndiyo mama…”
“Haya pita, lakini sasa nina wasiwasi na
kitu kimoja…”
“Kipi tena mama..?”

“Mvua ni kubwa sana na mzee alisema
anasafiri, haiwezekani akaghairi kusafiri, akarudi..?”
“Mh! Lakini hataweza kuingia ndani hadi
afunguliwe geti…”
 
“Nitakwenda kufungua mimi,” alisema mlinzi…
“Sasa ukitoka si atasikia mlango huu
ukifunguliwa wakati wewe unatakiwa kukaa kwenye kijumba chako..?”
“Mama, atasikia na mvua hii, labda kama
itaacha kunyesha mama.”
Hapo, mlinzi alishaketi, mama Joy naye
aliketi lakini kwenye kochi jingine.
 
Walitulia kwa muda wakitazamana. Mama Joy
ndiye aliyekuwa akimwangalia kwa macho ya mahaba mlinzi wake huyo ambapo yeye
alikuwa akisikia aibu na kuangalia chini kila mara…
“Sasa?” aliuliza mama Joy…
 
“Sijui, si uliniita bosi ukasema una
mazungumzo muhimu na mimi.”
“Ee, ni kweli. Sasa nataka tukaongelee
chumbani kwani mambo yenyewe ni nyeti sana.”
Mlinzi alishtuka kusikia kauli hiyo mpaka
ikawa inajirudiarudia kichwani mwake…

“Ee,ni kweli. Sasa nataka tukaongelee chumbani kwani mambo yenyewe ni nyeti sana.”
“Sawa bosi,” alisema mlinzi. Moyoni alijua
hakuna cha mambo nyeti wala nini, bosi wake anataka kitu na boksi.
 
Mwanamke huyo ndiye aliyetangulia kusimama,
akamfuata mlinzi, akamshika mkono na kuanza kuondoka naye. Waliingia chumbani
ambapo kwa mara ya kwanza na aliamini pengine na ya mwisho kwa yeye kuingia
kwenye chumba cha tajiri yake.
 
Ni kweli alikuwa hafanani na chumba hicho
lakini alishatunukiwa na mama mwenye nyumba.
Nje mvua ilikazana kunyesha, kibaridi
kilikuwa kikali kiasi kwamba, chumbani hakukuwa na haja ya kuwasha ‘AC’ kama
inavyokuwaga wakati wa joto…
 
“Utaoga?” mama Joy alimuuliza mlinzi wake
huku mwili ukimnyevuanyevua kwa hisia za mahaba. Alitamani lisitokee hilo la
kwenda kuoga kwani dakika tano mbele kuanza pale kwake ilikuwa ni pigo la kiu
yake ya kufanya mapenzi…
 
“Kuna baridi sana bosi, siwezi kuoga.”
Mama Joy alimshika kwa fujo mlinzi wake na
kumwangushia kitandani na nguo zake zikiwa zimeloa mvua chapachapa, miguuni
matope, mpaka kinyaa.
 
Kisha na yeye akavua nguo haraka. Alivua
zote akabaki kama alivyozaliwa…
“Njoo baba njoo,” alimwita mlinzi huku yeye
akiwa anaelekea ukutani. Mlinzi alishangaa sana kwanini aitwe ukutani badala ya
kitandani. Kwanza alisita, ghafla mwanamke huyo akamfuata, akamshika mkono na
kumvuta.
 
Walikwenda hadi kwenye kona ya ukuta. Mama
Joy akamchojoa nguo zote huku akimtaka ajisikie yuko huru. Aliamini kama mlinzi
huyo atakuwa na wogawoga hatamtosheleza katika huduma ya mapenzi…
“Sawa.”
 
Mama Joy akaenda kitandani, akatoa godoro na
kuliburuza peke yake hadi kwenye kona. Kwa kuwa chumba kilikuwa kikubwa na
chenye nafasi ya kutosha, aliliweka pembeni kabisa, akarudia mashuka mawili.
Alitandika mwenyewe shuka moja, jingine
akalitupia juu ya godoro kwa ajili ya kujifunuka.
 
Alimvuta mlinzi, naye akaangukia hapo.
Shughuli ilianza. Mama Joy alimwingiza mlinzi wake kwenye shuka na kumwanzishia
mechi huku akijisisimua mwenyewe.
Mlinzi alibadilika moyo, akawa kama mwanaume
mwingine. Alianza kumchezesha mchakamchaka bosi wake huku wakiwa gubigubi ndani
ya shuka zito.
 
Bosi alikubali, alilalamika sana na
kumuahidi mlinzi wake hiyo mabo kibao…
“Fuko…nitahakikisha unaongezewa mshahara…nitahakikisha
unabadilishiwa kazi, uje kufanya kazi za huku ndani…nitakuwa nakununulia nguo…”
“Nitashukuru sana mama,” alisema Fuko…
“Kwa sasa sitisha kuniita mama, niiite
mkeo…”
 
“Haya mke wangu…”
“Eee, hapo sawa sasa…”
Mvua ilizidi kunyesha mpaka wenyewe ndani
wakaogopa mle chumbani…
 
“Mh! Mvua kubwa sana mke wangu,” mlinzi
alisema bila woga wala kumung’unya maneno kwenye kinywa chake chenye harufu ya
sigara…
“Nikumbatie zaidi, mi naogopa mume wangu,”
alisema mama Joy huku na yeye mwenyewe akimkumbatia sana mlinzi wake huyo.
 
Fuko alitii agizo, aliongeza kumbana
mwanamke huyo mpaka mwisho wa uwezo wake. Mama Joy alitangaza kuvunjia dafu
lake hapo lakini wakati akijilegeza kwa zoezi hilo simu yake ikaita na kumtoa
kwenye stimu…
“Siyo baba Joy huyo kweli?” alisema mama Joy
huku akikurupuka kwa fujo pale kwenye godoro…

Aliifuata simu na kuiweka sikioni, lakibi
ilikata. Alipoangalia namba na mpigaji ni mumewe, alipompigia ikawa haipatikani
tena…
“Khaa! Sasa huyu mbona ananiweka katika
wakati mgumu sana,” alisema mama Joy.
Mlinzi alimfuata na kumdaka, akamrejesha
kwenye godoro chini huku akimtaka kumtendea haki kwani ‘gari’ lake
lilishaongeza spidi lenyewe…
 
“Mke wangu nina hali mbaya,” alisema mlinzi…
“Jamani mbona hata mimi mwenyewe,” mama Joy
alisema akijiweka sawa. Mpambano mwingine ukaendelea ambapo mwanamke huyo
hakuchelewa akatangaza dafu linavunjika, mlinzi naye akapasua la kwake sambamba
na mama Joy.
 
Walibaki kimya kwa muda, kila mmoja alikuwa
akihema kwa kasi, wakati mwingine walitazamana kama waliotaka kuchekeana,
lakini mama mlinzi aliona aibu.
Simu ya mama Joy iliita tena, akaiwahi,
akaiweka sikioni…
“Baba Joy,” aliipokea kwa sauti ya chini
kama vile alikuwa hataki mtu mwingine asikie…
 
“Nimelala ndiyo, umesafiri na mvua hii..?”
“Ooo, pole sana. Basi safari njema,” kusema
‘basi safari njema’, mama Joy alitoa sauti ya juu kuliko alipopokea simu.
Aliweka simu kwenye meza, akamfuata mlinzi
na kumwangukia kwa furaha…
“Mume wangu, leo tufaidi mpaka wenyewe
tuseme basi.”
 
“Bosi ameamua kusafiri na mvua?”
“Anasema anakaribia Kibaha Maili Moja.”
Walicheka, wakakumbatiana. Mama Joy akamtoa
mlinzi kwenye godoro na kumsimamisha kisha yeye akabeba godoro na kuliweka
kitandani…
 
“Haya! Tulale kwa raha zetu sasa,” alisema
mama Joy. Alitangulia kupanda yeye, akamwita mlinzi, lakini naye kabla
hajapanda, mama Joy alishuka na kwenda kwenye kabati kubwa la nguo lililomo
chumbani humo na kutoa pajama pea moja... 
 
“Vaa hii ya mista, usiku wa leo kuna baridi
sana, sawa?” Mlinzi aliidaka pajama hiyo na kuitumbukiza mwilini mwake kisha
akapanda kitandani kulala.
Ulikuwa usiku wenye historia kwao, walitumia
muda mwingi kukumbatiana ndani ya shuka moja na kila ‘walipochaji’ walicheza
‘mechi’.
Mpaka saa saba usiku, walikuwa wamecheza
mechi nne, mama Joy alianza kuwa hoi, lakini mlinzi alitaka kupasha mazoezi ili
mechi ziendelee.
 
“Mume wangu tutaendelea kesho, mimi sasa
nimechoka sana,” alisema mama Joy kwa sauti ya tabu. Ni kweli alichoka. Hakuna
siku amewahi kuchezeshwa mechi mfululizo kama usiku huo.
 
Mpaka jua linataoka, wawili hao walikuwa
wamelala fofofo, hawajitambui.
Mfanyakazi wa ndani ndiye aliyetangulia
kushtuka kwamba, mama mwenye nyumba siku hiyo alikuwa amepitiliza kulala. Na
aliligundua hilo baada ya geti kubwa kugongwa kwa nguvu…
 
“Nani huyo? Halagu mbona mama hajaamka mpaka
muda huu?”
Alitoka kwenda getini ambapo alishangaa
kutomwona mlinzi huku geti limefungwa kwa kufuli kwa ndani…
“Mh! Pana usalama kweli hapa..?” aliwaza
mfanyakazi huyo huku moyo ukianza kupata wasiwasi hasa alipokumbuka kesi nyingi
za walinzi kufanya uhalifu na kukimbia.
 
Alikimbilia ndani, akagonga mlango wa chumba
cha bosi wake huyo huku wasiwasi ukizidi kumpanda…
 
“Lazima kuna tatizo, kwanza mlinzi hayupo
halafu mama naye hajaamka, pengine hayupo pia. Si kawaida yake kuwa kimya
asubuhi, lazima angefungulia redio,” alisema moyoni.
 
“Ngo ngo ngooo…” alizidi kugonga, lakini
geti kubwa nje nalo liliendelea kugongwa kwa nguvu vilevile.
Mfanyakazi huyo alianza kuamini tajiri yake
yupo baada ya kusikia mlio wa simu, akategemea kusikia ikipokelewa na ‘haloo’
lakini ikawa sivyo, ukimya ulitawala.
Alishika kitasa na kukitingisha kwa nguvu
huku akiita…
“Bosi…”
 
“Bosi kuna mgeni…”
Kwa mbali, mama Joy alisikia kutingishwa kwa
kitasa cha mlango, akashtuka. Alifikicha macho, akabaini jua lilishaanza
kuchomoza, akakurupuka kitandani…
“We Fuko…” mwenye nyumba alimwamsha kwa
fujo…
 
Mlinzi huyo alikurupuka naye huku akifikicha
macho kwa nguvu…
“Ha! Jua limetoka, mama yangu. Kama wamekuja
wageni nje itakuwaje?”
“Bosi,” aliendelea kuita yule mfanyakazi…
“Kuna nini?” mama Joy alihoji, wakati huohuo
simu yake iliita tena, akachanganyikiwa zaidi…
 
“Mungu wangu…atakuwa nani huyo..?”
Fuko alivaa nguo zake na kufungua mlango ili
atoke mbio, akakutana na macho ya mfanyakazi wa ndani…
“Ha!” alihamaki mfanyakazi…
“Ooosh,” mlinzi naye alishutuka akarudi
chumbani…
 
“Sasa wewe unatokaje bila kuniambia, je
ukikutana na huyo mama wa kazi itakuwaje?” alihoji mama Joy…
“Siyo nikikutana naye, nimekutana naye kweli,
amesimama hapo mlangoni…”
“Kweli..?”
Na Muandishi wako IRENE MWAMFUPE NDAUKA Usikose sehemu ya 05 Siku ya jumatano ya wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate