EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 26, 2012

Lulu bado njia panda

SERIKALI imezidi kumweka katika wakati mgumu msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael Lulu, anayekabiliwa na kesi ya tuhuma za mauaji ya msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Hatua hiyo inatokana na hatua ya upande wa mashitaka kukwamisha usikilizwaji wa kesi hiyo kwa kuwasilisha Mahakama ya Rufani maombi ya kupitiwa upya uamuzi wa Mahakama Kuu wa kukubali kufanya uchunguzi wa umri sahihi wa mshitakiwa huyo.

Umri wa Lulu umeibua utata wa kisheria baada ya upande wa utetezi kusema mteja wao ana miaka 17 na si 18 kama Hati ya Mashitaka inavyoonyesha, hivyo unadai kisheria anapaswa kushitakiwa katika Mahakama ya Watoto huku ule wa mashitaka ukipinga hoja hiyo.

Kufutia hali hiyo, mshitakiwa huyo aliyefika Mahakama Kuu jana Jumatatu kusikiliza shauri la utata huo wa umri wake, alishindwa kujizuia na kumwaga machozi baada ya mahakama hiyo kusimamisha shauri hilo.

Katika kesi yake ya msingi iliyoko Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Lulu anatuhumiwa kumuua Kanumba usiku wa Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu, Sinza, jijini Dar es Salaam.

Utata wa umri wa Lulu ulitarajiwa kusikilizwa hiyo jana Jumatatu na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Juni 11, 2012 Mahakama Kuu iliamua kufanya uchunguzi wa usahihi wa umri wa msanii huyo kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea.

Lakini jana Jumatatu, Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, asema mahakamani hapo kuwa upande wa Jamhuri tayari imewasilisha maombi Mahakama ya Rufani kuomba uamuzi huo wa Mahakama Kuu uliotolewana Jaji Dk. Fauz Twaib ufanyiwe marejeo.

Jaji Dk. Twaib alikubaliana na maombi haya Jamhuri na kusimamishwa usikilizwaji huo hadi Julai 9, 2012, ikiwa Mahakama ya Rufani itakuwa imemaliza kushughulikia maombi hayo ya Serikali.

Kabla ya mahakama kufikia uamuzi huo, mawakili wa Lulu, Kennedy Fungamtama na Peter Kibatala, walipinga maombi ya serikali wakidai ni mbinu ya kuchelewesha shauri hilo.

Fungamtama alidai kuwa hadi wakati huo mahakama ilipoanza hapa kuwa na amri yoyote ya Mahakama ya Rufani ya kusimamishwa usikilizwaji wa suala la utata wa umri wa mteja wao.
Hata kwenye maombi haya hakuna maombi yanayoelekeza kusimamishwa kwa usikilizwaji wa maombi haya, alisema Fungamtama.
Kinachofanywa hapa ni matumizi mabaya ya mamlaka ya Ofisi ya DDP (Mkurugenzi wa Mashtaka).

Kwa upande wake, Wakili Kibatala, alidai kuwa maombi hayo ya Jamhuri kwa Mahakama ya Rufani hayaoneshi mazingira ya kusimamishwa kwa usikilizwaji wa maombi hayo na kwamba hiyo inabaki kwa mamlaka ya Mahakama Kuu yenyewe.
Lakini kwa maslahi ya mshtakiwa ambaye anaendelea kuteseka mahabusu, tunaiomba mahakama hii iamuru usikilizwaji wa maombi haya (utata wa umri ) uendelee,alisisitiza Kibatala.

Lakini akijibu hoja hizo, Wakili Kaganda, alidai ofisi ya DPP inatambua matakwa ya haki na kwamba inatenda kwa matakwa ya haki haitumii vibaya mamlaka yake.

Lulu anaendelea kushikiliwa rumande kwa vile aina ya shitaka linalomkabili halina dhamana kisheria.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate