EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 16, 2012

‘Madee’ kamtimua Dogo Janja Bongo

Na Musa Mateja
Wiki hii haikuwa njema kwa rapa mdogo wa Kibongo, Aboubakar Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ baada ya Rais wa Manzese ambaye ni kiongozi wa Kruu ya Tip Top Connection aliyekuwa akimlea, Hamad Ally ‘Madee’ kumtimua Bongo, Risasi Jumamosi linakudondoshea ilivyokuwa.
Tukio hilo lililotokea Juni 13, mwaka huu baada ya Madee kupokea malalamiko kuwa Dogo Janja ameacha shule akiwa kidato cha pili katika Sekondari ya Makongo, Dar huku akidai kuwa anataka kwenda kusoma mkoani Arusha alikokulia.

Mbali na kukacha skonga, Madee alisema Dogo Janja alikuwa akijihusisha na mambo mabaya kinyume na makubaliano na wazazi wake waliomkabidhi amlee.
Dogo Janja alionekana akipunga mkono kwa mashabiki wake kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo, Dar akiwaaga kwa kusema: “Kwa heri Bongo, naenda zangu Ngarenaro (Arusha) kunywa chai na karoti lakini muda siyo mrefu nitawaibukia.”
Wakati akielekea kwao Arusha, Dogo Janja aliandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa BBM:
“Madee kweli kanisaidia kwa namna moja au nyingine kunileta Bongo ila kuna mapungufu ambayo pia kwake hawezi kuyafahamu na anakoelekea nahisi si pazuri, ilifikia kipindi hadi akawa ananinyang’anya simu na kutumia watu meseji za kunichonganisha.

“Nahisi uvumilivu kunishinda kutokana na habari zinazoongelewa na kaka yangu Madee, maana anachosema mimi nikisema kwa watu ataumbuka tu.
“Tangu anichukue kwetu na kuanza muziki sijawahi kupewa fedha taslimu zaidi ya Sh. laki 3 na siku zingine kuishia elfu 50.

“Madee alikuwa hana nia nzuri na mimi na nimegundua alikuwa ananisaidia kimuziki ili afaidike yeye, maana hapa naenda Arusha, akaunti yangu ina elfu 25 tu, halafu huwezi kuamini Madee katoa elfu 20 tu ya nauli, yaani kaniangusha sana na wala sikutegemea atanifanyia hivyo.”
Dogo Janja aliyewika na ngoma ya Anajua huku kukiwa na madai kuwa anataka kujiunga kwenye kundi fulani la muziki Bongo, aliwahi kuripotiwa kutoroshwa na mademu usiku jambo lililomkasirisha Madee lakini baadaye walimalizana.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate