EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 16, 2012

UNYAMA: Mtoto achomwa mikono yote

Mtoto huyo, Issa Hassan achomwa mikono yote
Unyama wa kutisha amefanyiwa mtoto mmoja wa miaka minane jijini Dar es Salaam baada ya mama yake mkubwa kumchoma moto mikono yote kutokana na kumtuhumu kumuibia Sh 500 za mauzo ya samaki.
Mtoto huyo, Issa Hassan anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Twiga, Mtoni Kijichi, amelazwa katika Hospitali ya Temeke baada ya hali yake kuelezwa kuwa mbaya baada ya kupata majeraha makubwa ya moto huo.

Akiongea kwa shida hospitalini hapo, mtoto huyo alisema unyama huo alifanyiwa majira ya saa 5:00 usiku eneo la Mtoni Kijichi na mama yake huyo aliyefahamika kwa jina la Fatuma Yusufu (52), ambapo imeelezwa kabla ya kuunguzwa kwa moto huo alilazimishwa kufanya mazoezi ya kushika masikio.
Taarifa kutoka katika eneo la tukio zinaeleza Issa alichukuliwa na mama yake mkubwa kutoka Mtwara akiwa bado mdogo kwa ajili ya kumlea baada ya mama yake mzazi kuugua maradhi ya akili kwa siku nyingi.
Alisema siku ya tukio mama yake alimfuata kwenye chumba anacholala na kumuuliza kama amechukua sh 500 za mauzo ya biashara yake ya samaki wa kukaanga. Hata hivyo, alimjibu hakuchukua pesa hiyo, lakini mama yake alipinga na kusisitiza kuzichukua.

"Alinisubiri wakati wa kulala alikuja na kuniuliza kama nilichukua Sh 500, nilikataa lakini alionekana kuwa mkali huku akisema nimechukua," alisema mtoto huyo.
Wakati wa majibizano hayo yakiendelea, Fatuma alimkamata na kumshurutisha kupiga magoti na ashike masikio kama moja ya mazoezi.

"Mama aliniambie nipige magoti nianze kufanya mazoezi ya kushika masikio, baadae aliniambia nikae chini na ninyooshe miguu yangu," aliendelea kusema.
Baada ya kutii amri hiyo alimkamata mikono yake na kumfunga matambaa na mifuko ya nailoni. Alipohakikisha hawezi yameenea mikono yote alichukua mafuta ya taa na kisha kumwagia kabla ya kumuwasha kwa kibiriti.

Moto ulivyokuwa ukiwaka mtoto huyo alilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali aliyokuwa akiyasikia, kitu ambacho kilisababisha majirani kujitokeza na kuanza kumuokoa mtoto huyo.
Kwa mujibu wa Aminajat Kilema ambaye amejitolea kumuuguza mtoto huyo hospitalini hapo, alisema kutokana na maelezo ya majirani walidai wakati wa kumuokoa mtoto huyo ilibidi watumie nguvu kutokana na mwanamke huyo kumng'ang'ania akitaka moto huo uendelee kumuunguza hadi uzimike wenyewe.
"Majirani walijitahidi kumuokoa kwa taabu sana, alikuwa mkali na ilibidi kutumia nguvu kubwa kumchukua mtoto na kuuzima moto, lakini tayari alikuwa ameungua vibaya," alisema.

Naye Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Amani Malima alisema walimpokea mtoto huyo juzi akiwa katika hali mbaya baada ya moto kuunguzwa mikono yake kwa asilimia hamisini. Hata hivyo baada ya kumpati matibabu hali yake imezidi kuimarika.
Taarifa zilizopatikana wakati Gazeti hili linakwenda mitamboni kutoka kwa Afisa Ustawi wa Jamii wa Manispaa ya Temeke Sultan Mziray alieleza idara yake kwa kushirikiana na jeshi la Polisi imemfikisha Fatuma katika Mahakama ya mfawidhi Wilaya ya Temeke kujibu tuhuma hizo.
Hata hivyo, imeelezwa licha ya mtoto huyo kupewa matibabu, anakabiliwa na matatizo kadhaa ikiwa pamoja na ukosefu wa mavazi na chakula baada ya kutokuwa na ndugu jijini.
Aidha kwa watu watakaoguswa na mkasa wa mtoto huyu na kutaka kutoa msaada wa haraka wanaombwa kufika ofisi ya Ustawi wa jamii Wilaya ya Temeke au wawasiliane kwa simu namba 0712481919.
                                               CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate