Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akitoa hotuba wakati wa kuzindua Kampeni ya Uhamasishaji wa Matibabu ya Fistula Tanzania ambapo pamoja na mambo mengine amesema mradi wa Fistula unalenga kumaliza tatizo la Fistula hapa nchini ambapo inakadiriwa wastani wa Wanawake Wapya 2500 hadi 3000 hupata ugonjwa huo wakati wanapojifungua. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa CCBRT Bw. Erwin Telemans na Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya CCBRT Dkt. Wilbrod Slaa.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam katika uzinduzi wa Kampeni ya Uhamasishaji wa matibabu ya Fistula Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa CCBRT Bw. Erwin Telemans akizungumza katika uzinduzi huo ambapo amewataka Wanawake kujitokeza kupatiwa matibabu kwa kuwa tunataka Tanzania bila FISTULA na kusisitiza tuwe mfano wa kuigwa na nchi zingine katika kutokemeza ugonjwa huu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Bw. Michael John akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo ambapo amesema Serikali ya Tanzania iko bega kwa bega na CCBRT pamoja na wadau wengine katika kuhakikisha lengo la kutokomeza Ugonjwa wa FISTULA linatimia.

Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete (wa pili kulia) akipitia hotuba huku Mkurugenzi Mkuu wa CCBRT Bw. Erwin Telemans (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya CCBRT Dkt. Wilbrod Slaa. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema.

Shuhuda Beatrice Ramadhani na mumewe Hosea Wilson Sanga akisimulia jinsi alivyopatwa na ugonjwa wa FISTULA na kupoteza mtoto wa kwanza lakini alipopata taarifa kuwa ugonjwa huo unatibika alifika katika Hospitali ya CCBRT na kupatiwa matibabu bure na sasa amepona kabisa na kufanikiwa kupata mtoto.

Bw. Hosea Wilson Sanga akizungumza ambapo amewaasa kina baba kutowatenga wake zao wanapokuwa na ugonjwa wa FISTULA na badala yake ni kuwapa moyo na kwapeleka Hospitali kwa ajili ya matibabu.

Mama Salma Kikwete akimpongeza Shuhuda Beatrice Ramadhani kwa ujasiri wa kujitokeza na kuwa mfano kwa wanawake wengine.

Wasanii wa Kikundi cha Mjomba Bendi wakionyesha igizo lenye fundisho kwa wanaume kutowafukuza wake zao majumbani wanapougua ugonjwa wa FISTULA kwa kuwa Ugonjwa huo husababisha Mwanamke kushindwa kudhibiti haja ndogo na kubwa.

Msanii wa kughani mashairi Mrisho Mpoto akiwasilisha Ujumbe kwa jamii nini cha kufanya pindi wanapoona mwanajamii mwenzao anaugua ugonjwa wa FISTULA.

Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akielekea kujumuika kuserebuka na wananchi sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema (kulia).



Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete (kulia) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kampeni ya Uhamasishaji wa Matibabu ya FISTULA itakayoendeshwa nchi nzima ambapo wanawake wanaougua Ugonjwa huo watapata matibabu Bure. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Mipango ya Kijamii wa CCBRT Brenda Msangi (katikati) na Meneja Mawasiliano wa CCBRT Bw. Abdul Kajumulo.

Dkt. Willbrod Slaa akitoa neno la Shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wake katika kuhakikisha kampeni hii inafanikiwa.

Mama Salma Kikwete akimsikiliza kwa umakini Mwenyekiti wa Bodi ya CCBRT Dkt. Wilbrod Slaa (hayupo pichani).
Pichani Juu na Chini ni  baadhi ya Wafanyakazi wa CCBRT na Wananchi waliofika viwanja vya Mnazi Mmoja kushuhudia uzinduzi huo.
Bw. Abdul Kajumulo (kushoto) akiwa na Wafanyakazi wenzake wakihakikisha zoezi zima linakwenda sawa. 
Wanawake kote nchini wanaosumbuliwa na ugonjwa wa Fistula wametakiwa kutojificha kwa kuogopa aibu, badala yake wajitokeze na wafike hosptali kupatiwa matibabu kwa kuwa ugonjwa huo unatibika.

Rai hiyo imetolewa leo na Mama Salma Kikwete wakati akizindua Kampeni ya Uhamasishaji wa Matibabu ya Fistula ambapo amesema miongoni mwa athari za ugonjwa huo ni mama kupoteza kichanga wakati wa kujifungua, kupoteza uwezo wa kudhibiti haja ndogo na/au kubwa na kutokwa na haja ndogo na kubwa kwa wakati mmoja, kupitia njia moja.

Mama Salma amesema ugonjwa huo ni moja ya changamoto katika sekta ya afya hapa nchini na hivyo akatoa wito kwa taasisi binafsi na mashirika na wadau wa maendeleo na wananchi kwa ujumla kujitoa kusaidia juhudi za kutokomeza tatizo hili la Fistula.
                                Chanzo cha habari Na.MO BLOG TEAM