EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 26, 2012

Wezi waiba kompyuta, nyaraka TCU

Watu wanaodaiwa kuwa wezi wamevamia ofisi za Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na kuwalewesha kwa chakula kinachodaiwa kuchanganywa na dawa za kulevya walinzi wa kampuni ya Bulwark waliokuwa wakilinda na kisha kuvunja milango na kupora nyaraka na vitu mbalimbali vya mamilioni ya fedha zikiwemo dola za Marekani 6,000.

Kamanda wa mkoa kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela, akizungumza na NIPASHE alisema tukio hilo limetokea jana Juni 25 mwaka huu majira ya saa 12:30 asubuhi.

Alivitaja vitu vilivyoibwa kuwa ni pamoja na Kompyuta 11 aina ya Dell na HP, funguo za magari, fomu za wanafunzi wanaoomba mikopo, luninga aina ya Sumsung na dola za Marekani 6,000.

Alisema walinzi wa kampuni ya ulinzi ya Bulwark ambao walikuwa wakilinda ofisi hizo walikutwa wamelala fofofo wakiwa hawajitambui baada ya kula chakula kilichosadikiwa kuchanganywa na dawa za kulevya ambao ni Japhet James (34) mkazi wa Magomeni Kagera na Shaban Simba (60) mkazi wa Manzese.

Kamanda Kenyela alisema walinzi hao wamepelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu na wataendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi hadi watakapopata fahamu ambapo watatakiwa kutoa maelezo ya mazingira ya tukio hilo na ikibainika kulikuwa na uzembe hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Alisema kufuatia tukio hilo, polisi waliimarisha ulinzi katika wilaya zote za jiji la Dar es Salaam na kufanikiwa kupata baadhi ya vitu vilivyoibwa katika eneo la Temeke ambavyo ni fomu za maombi ya mikopo, funguo za magari na luninga ya Samsung.

Kamanda Kenyela alisema vitu hivyo vimepatikana baada ya kuwakurupusha wezi waliohusika katika tukio hilo ambao walivitelekeza na kwamba msako mkali umeimarishwa kuhakikisha waliohusika na wizi huo wanatiwa mbaroni pamoja na vitu vingine ambavyo havijapatikana.

Aliwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi watuhumiwa wa makosa mbalimbali wawe wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria kwani hali hii ikiachwa kuendelea itahatarisha usalama wa nchi.

Kadhalika, alitoa tahadhari kwa viongozi wa makampuni binafsi ya ulinzi kuhakikisha wanajenga utamaduni wa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika malindo wanayolinda walinzi wao kwani ni dhahiri kumekuwa na uzembe kwa baadhi ya walinzi wa makampuni hayo.

Alisema vitendo vya wizi katika malindo yanayolindwa na walinzi wa makampuni binafsi yamekuwa yakitokea mara kadhaa kutokana na walinzi hao kuwa na udhaifu kwa kupenda kupewa vyakula, vinywaji na zawadi mbalimbali ambavyo vinakuwa vimechanganywa na madawa ya kulevya na hivyo kujikuta malindo yao yakiibiwa kirahisi.

“Kuna uzembe mkubwa kwa walinzi wa makampuni binafsi ya ulinzi, tutaanza kuishawishi serikali iyafutie usajili, mfano walinzi wa kampuni ya Bulwark inaonesha kabisa kulikuwa na uzembe mkubwa, walinzi wa kampuni hii walikuwa na silaha aina ya Short gun lakini hawakuitumia kukabiliana na wezi hao na bahati nzuri tumeikuta,” alisema Kenyela.
                                                  CHANZO:GAZETI LA NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate