EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 22, 2012

CCM yapumulia mashine

•  Ajali ya mv Skagit, urais 2015 vyaitesa
UPEPO wa mabadiliko ya kisiasa uliozikumba nchi nyingi duniani, unaelekea kukiathiri Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho sasa kinahaha kujinusuru kung’oka madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Chama tawala hivi sasa kina msuguano mkubwa wa kiuongozi ambapo baadhi ya viongozi wake wamekuwa wakimshutumu Katibu Mkuu, Willison Mukama, kwa kukwamisha mikakati ya kujiimarisha na kurejesha matumiani yaliyofifia miongoni mwa wanachama wake.

Licha ya Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wiki hii kukanusha kutokuwa na msuguano na Mukama, makada wa chama hicho wamelidokeza Tanzania Daima Jumapili, kuwa vita ya makundi ya kuwania uongozi na ile ya ufisadi inakitesa chama hicho.
Mnyukano wa kisiasa unaonekana wazi hivi sasa ni baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, dhidi ya kundi linalomuunga mkono aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, anayetajwa kutaka kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wakati hali ya mambo ikionekana kutokuwa nzuri ndani ya chama hicho, nguvu kubwa sasa imehamishiwa kwenye Bunge kwa lengo la kuwadhibiti wabunge wa CHADEMA ambao wanaelezwa kutishia uhai wa chama hicho.
Makada wa CCM wamedokeza kuwa wamebaini wabunge wa CHADEMA mwaka 2005-2010 walilitumia vizuri Bunge kujenga hoja za msingi ambazo ziliwasaidia kujijenga na hatimaye kupata wabunge 22 wa majimbo kutoka watano.

Waliongeza kuwa kutokana na kubaini jambo hilo, chama hicho kimeamua ‘kuzishughulikia’ hoja zinazotolewa na CHADEMA bila kujali kama zina masilahi kwa taifa au la.
Inadaiwa kuwa viongozi wa Bunge nao wamepewa maelekezo ya kukisaidia chama chao hasa wanapoona kuna hoja zinazoelekea kuwapatia umaarufu wabunge wa CHADEMA.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa pamoja na maelekezo hayo baadhi ya viongozi wa Bunge wameonekana kushindwa kukisaidia chama tawala kwa sababu ya kutozijua ipasavyo kanuni, hivyo kutumia ubavu kukataa jambo linalotolewa na wapinzani, hivyo kuwaongezea umaarufu.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, anatuhumiwa kutoa fursa zaidi kwa wabunge wa CCM kurudia maneno ya dharau na lugha ya kuudhi dhidi ya wapinzani.
Kiongozi huyo pia juzi alionesha ‘ukada’ wake pale alipojifanya kukosea jina la Mbunge wa Viti Maalumu, Rose Kamili, kwa kumuita Rose Kamili Slaa, ilhali akijua mbunge huyo alishatarikiana na Dk. Slaa.

Hata hivyo CCM hivi sasa pia kinakabiliana na wakati mgumu wa kushutumiwa kushindwa kuwachukulia hatua watendaji wake wanaobainika kufanya uzembe katika shughuli zao za kila siku.
Ajali ya mv Spice Islanders iliyotokea mwaka jana na mv Skagit iliyotokea wiki iliyopita inadaiwa ilichangiwa na uzembe wa wataalamu kwa kushindwa kukagua ubora wake.
Serikali ya CCM pia inalaumiwa kwa kushindwa kuwa na vifaa vya kisasa vya uokoaji licha ya kila mara kukumbwa na matukio ya ajali za baharini na ziwani.

Katika ajali hizo mbili za majini zilizopoteza maisha ya Watanzania zaidi ya 400, serikali ya CCM inalaumiwa 
kwa kushindwa kusimamia sheria za usafiri wa majini na kuficha taarifa ya uchunguzi wa ajali ya awali.
Mmoja wa wabunge wa CCM ambaye jina lake limehifadhiwa, aliilaumu serikali kwa kuunda tume kuchunguza ajali ya mv Bukoba na Spice Islanders, lakini haikutoa matokeo ya uchunguzi huo.

“Serikali iliunda tume kuchunguza ajali ya awali ya mv Spice Islanders na mv Bukoba lakini ikaficha matokeo ya uchunguzi wake. Leo imetokea ajali nyingine na binafsi naamini kama matokeo ya uchunguzi wa awali yangetolewa, bila shaka ajali ya juzi ingeepukika,” alisema kada huyo.
Kufichwa kwa matokeo ya uchunguzi wa ajali za awali za majini, kumeelezwa kuwa ndiyo sababu ya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kuzima hoja za wabunge wa kambi ya upinzani walioungana na wabunge wote wa Zanzibar kutaka kujadili ajali ya mv Skagit iliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 150.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate