EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 22, 2012

Wananchi wa Mgodi wa Buhemba kuishitaki Serikali Jumuia za Kimataifa

Diwani wa kata ya Buhemba Boniphace Masero akifafanua jambo kwa waandishi wa habari

Augustine Mgendi, BUHEMBA
WANANCHI vijiji Vitatu wanaozungukwa na Mgodi wa Buhemba  wilaya ya Butiama mkoani Mara wanakusudia kuishitaki Serikali ya Tanzania katika Taasisi za Umoja waMataifa zinazohusika na haki za binadamu ikiwa ni shinikizo la kulipwa fidia ya shilingi Bilioni 30.

Mbali na kusudio hilo la kuelekea umoja wa Mataifalakini pia wananchi hao wamesema kuwa wanakusudia kumuona Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania Jakaya Kikwete kumueleza madhara yaliyosababishwa na Mgodihuo ambao ulidaiwa kumilikiwa na Serikali kupitia Kampuni ya Meremeta.

Wananchi hao kutoka vijiji vyaTarani,Biatika na Magunga huku wakiomba Wabunge kuungana na kutoipitisha Bajetiya Wizara ya Nishati na Madini had hapo Serikali itakapo wafidia.  

Akiongeana waandishi habari katika eneo hilo la Buhemba,Diwani wa kata ya BuhembaBoniphace Masero amesema kuwa Mgodi huo umeachia athari kubwa kutokana namachimbo yaliyoachwa kuleta athari kubwa huku Ardhi yao ikiwa haina rutuba kutokanana Kemikali zilizomwagwa katika eneo hilo

Amesema athari zingine zilizoletwa na Mgodi huo nipamoja na Shule iliyokuwa katika eneo hilo kubomolewa lakini walishindwakuijenga kama walivyokuwa wameahidi wahuska hao wa mgodi huku miundombinu yabarabara nao ikiwa haifai kutumika.

“Huu Mgodi umetuachia madhara makubwa sana maanaMashimo hayakufukiwa,Milima inaleta uchafuzi wa Mazingira,shule iliyokuwaimejengwa hapa ilibomolewa,Nyumba zikabomoka kutokana na Baruti za mgodi,katikahili sisi tunakusudia kumuona Rais ili tumueleze haya Manyanyaso tunayoyapata”alisema diwani huyo

Diwani Masero ameongeza kuwa athari nyingine nipamoja na baadhi nyumba za wakazi wa eneo hilo kubomoka kutokana na barutizilizokuwa zikipigwa katika Mgodi huo lakini mpaka sasa hawajalipwa fidia nahivyo wanawaomba Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniakutoipitisha Bajeti ya wizara ya Nishati na Madini mpaka walipwe fidia yao

Aidha Pasta wa Kanisa la Anglikana SamweliNyakarungu alisema kuwa mgodi huo wa Buhemba ulikuwa ni Mgodi wa kitapeliambapo wahusika hao wamechuma raslimali za Taifa na kushindwa kufanya shughuliza Maendeleo katika Jamii.

Pasta Nyakarungu alisema kuwa mbali na wawekezajihao wa Kitapeli kuiba mali ya Watanzania lakini pia wamesababisha madharamakubwa kwa jamii ya Buhemba kwa kushindwa kujenga miundombinu ya barabara,kujengashule kama inavyotakiwa.

Kutoka na adha hiyo Pasta huyo alisema kuwa Serikaliimeshindwa kuwajali wananchi wake na hivyo wanawaomba Wabunge wa Bunge laJamhuri ya Muungano kutoipitisha Wizara ya nishati na Madini mpaka hapowananchi wa eneo hilo watakapopata fidia yao.

  “Hawa wawekezajimimi naona hawakuja hapa kwa lengo la kumsaidia mtu wa Buhemba huu Mgodi naonaulikuwa wa Kitapeli kabisa,wamechuma raslimali za Taifa na kushindwa kumsaidiamtu anayezungukwa na mgodi na hata kurekebisha miundombinu huska na hiiinaonyesha jinsi Serikali isivyojali wananchi wake” alisema Pasta Nyakarungu

Naye Mwalimu mstaafu Sita Nyamhanga na bi HadjaYasini walisema kuwa mgodi huo umewaachia matatizo makubwa ikilinganishwawalivyokuwa wameahidiwa wakati wanaanza uchimbaji katika mgodi huo.

 “Tunavyojuani kwamba wawekezaji wanapowekeza eneo lolote lazima watu wanaozungukwa naMgodi ule wanufaike lakini hapa Buhemba sisi wananchi ndiyo tumepat tabu kabisakwani mpaka sasa hatuna shule,barabara inayopitika muda wote,eneo letu limebakiJangwa huku wakina mama wanapata tabu kutafuta maji kutokana na vyanzo vingivya maji kuchafuliwa na mgodi” alisema Mwalimu mstaafu huyo.

Kwa upande wake Bi Hadja Yasini alisema kuwawanapata tabu hata kutafuta kuni kutokana na eneo kubwa la Buhemba kubakiJangwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Kulingana na adha hiyo Bi Hadja alisema kuwa nivyema Waziri mwenye dhama huska akawasaidia watu wa Buhemba ili waweze kupatafidia zao kutokana na madhara waliyoyapata kutokana na mgodi huo.

Mgodi wa Buhemba ambao ulianza kuchimbwa mwaka 2002ni moja ya mgodi ambao ulikuwa ni mkubwa hapa nchini ukielezwa kumilikiwa naSerikali na kufungwa mwaka 2006 huku ukiacha eneo hilo la Buhemba kupotezarutuba yake

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate