EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 21, 2012

Mbunge ahukumiwa kifungo au kulipa faini baada ya kukutikana na hatia

Mbunge wa Maswa Mashariki, Sylvester Kasulumbai (CHADEMA), na kada wa chama hicho, Robert William, wamehukumiwa kifungo cha miezi saba jela au kulipa faini ya sh 250,000 baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili ya jinai.

Adhabu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Tabora, Thomas Simba, muda mfupi baada ya kumwachilia huru mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho, Suzan Kiwanga, na mwanachama mwingine, Anwaryn Kashaga.

Kasulumbai na mwenzake walifungwa pingu na kupelekwa katika mahabusu ya mahakama kitendo ambacho kililalamikiwa na wakili Mbogolo kwamba ni cha udhalilishaji na uvunjaji wa haki za binadamu.

“Unakifurahia kitendo unachokifanya? Alisikika Kasulumbai akimuuliza askari polisi aliyemvika pingu mara baada ya hukumu hiyo kutolewa.

Akisoma hukumu ya kesi hiyo, hakimu Simba alisema kuwa hii ni sawa na kesi nyingine zinazowakabili watu wengine kwamba mbunge huyo atakwenda jela miezi mitatu kwa kutoa lugha ya matusi au kulipa faini ya sh 50,000.

Pia aliwahukumu washtakiwa hao kwenda jela miezi minne au kulipa faini ya sh 100,000 baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la shambulio liletalo madhara mwilini.

Hakimu Simba vile vile aliwataka washtakiwa hao kumlipa fidia ya sh 2,000,000 mlalamikaji Fatuma Kimario, ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga.

Washtakiwa wote walilipa faini hiyo na kuachiliwa huru huku wakibaki kusubiri kulipa fidia hiyo ya sh milioni moja kila mmoja.

Awali upande wa mashtaka ulidai kuwa washtakiwa wote walitenda makosa hayo Septamba 15 mwaka jana, katika Kijiji cha Isakamaliwa wilaya ya Igunga.

Mara baada ya kuachiliwa huru, Kiwanga na Kashaga walitoka nje na kutimua mbio jambo lililowafanya watu waliokuwepo mahakamani hapo kuwashangaa.

Mapema wakili wa utetezi, Edson Mbogolo, aliiomba mahakama itoe adhabu ndogo kwa wateja wake kwa vile ni wakosaji wa mara ya kwanza na kwamba Kasulumbai (62) ana watoto 27 na wake watatu wanaomtegemea.

“Mahakama izingatie kwamba Kasulumbai ni mwakilishi wa wananchi na endapo akipewa adhabu ya kifungo, jimbo lake litakuwa wazi na hivyo litaigharimu serikali kuitisha upya uchaguzi,” alisema Mbogolo.

Makosa mengine yaliyokuwa yakiwakabili washtakiwa hao ni kumweka chini ya ulinzi isivyo halali kwa mujibu wa sheria Mkuu huyo wa Wilaya, huku kosa la nne ni wizi kutoka maungoni ambalo halikuweza kuthibitishwa na hivyo kufutwa na mahakama.

via gazeti la Tanzania Daima.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate