EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 23, 2012

MTOTO WA UWOYA, DUDE SARE SARE MAUA



 Uwoya akiwa na Krish.

Eva akiwa na Naima.

Hamad Ndikumana ‘Kataut’.

Kulwa Kikumba 'Dude'.
Na Erick Evarist
AMA kweli duniani wawiliwawili na kama huna mwana eleka jiwe! Watoto wazuri wa mastaa wakubwa wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya (Krish) na Kulwa Kikumba (Naima) wanafanana ileile, Ijumaa Wikienda limewakagua kuanzia nywele hadi kucha.
Awali ilikuwa vigumu kuwatathmini watoto hao kwa kuwa walikuwa wadogo lakini sasa wamekua hivyo wamependeza na ukibahatika kumuona mmoja halafu ukaletewa mwingine ni vigumu kuwatofautisha.
Baada ya kuwepo kwa habari za kufanana kwa watoto hao ambao wa Dude ana sura yenye mvuto ‘beautiful’ na wa Uwoya ‘handsome boy’, Ijumaa Wikienda lilizama kwenye makabrasha yake na kukagua picha moja baada ya nyingine ili kung’amua ukweli.
MAJIBU YA KUPERUZI
Katika kuperuzi na kuzidadisi picha za watoto hao, majibu yalionesha waziwazi kufanana kwao ambapo jamii inafahamu wazi ni wa uzao tofauti kabisa.
Uwoya alimzaa Krish na mumewe kipenzi ambaye ni msakata kabumbu wa Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ huku Dude akimzaa Naima na mkewe ‘Eva wa Dude’.
Viungo vingi vya miili yao vinafafa kiasi kwamba ukimuona wa Dude unaweza ukadhani ni wa Uwoya na ukimuona wa Uwoya ni ‘vaisivesa’. Wamefanana kuanzia nywele, midomo, mashavu, pua, macho, kucha, paji la uso na mikono yaani ni saresare maua.
NGOJA TUMTAFUTE DUDE
Baada ya kujiridhisha kufanana kwa Krish na Naima, paparazi wetu alimtafuta Dude (baba Naima) ambaye alikiri kuwepo marafiki zake wengi ambao wamekuwa wakimwambia na kumsifia kuwa mwanaye amefanana na Krish wa Uwoya.
“Kufanana ni kitu cha kawaida kabisa, mimi mwenyewe nimeshafananishwa sana na watu ambao wengine ukiambiwa unaweza kushangaa. Ni kweli mwanangu na wa Uwoya wanafanana.
“Wengi wamekuwa wakizungumzia sana kufanana kwa mashavu, midomo na viungo vingine, kitu ambacho mimi naamini kinaweza kutokea kwa mwanadamu yoyote,” alisema Dude.
RAFIKI WA DUDE
Staa mmoja mkubwa wa filamu ambaye ni rafiki wa Dude, alipofika kumtembelea hivi karibuni, nyumbani kwake Jeti Lumo jijini Dar, baada ya kumuona Naima na kwa kuwa anamfahamu Krish, alikiri kuwa kweli duniani wawiliwawili.
“Kusema kweli watoto hawa wa mastaa wamefanana kwa 150%, itapendeza sana kama siku moja nao watakuwa mastaa na ikiwezekana waje waoane kabisa,” alisema staa huyo.
MAMA KRISH YUPO WAPI?
Hata hivyo, jitihada za kumpata mama Krish ili kujua na yeye kama anaweza kutia neno lolote juu ya kufanana kwa watoto wao, hazikuzaa matunda, lakini akipatikana atawekwa hewani na mtazamo wake.
TUJIKUMBUSHE
Pamoja na kufanana kwa kupita maelezo, watoto hao wametofautiana siku ya kuzaliwa kwani Krish wa Uwoya alizaliwa Mei 8, 2011 huku Naima wa Dude akizaliwa Machi 14, mwaka huu.
KALAMU YA MHARIRI
Gazeti hili linatumia nafasi hii kuwapongeza mastaa wetu Uwoya na Dude kwa kujaliwa watoto wazuri na pia linawaombea wote afya njema wakue nao waje kuwa mastaa kama wazazi wao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate