EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 16, 2012

SAKATA LA USAJILI WA YONDANI: SIMBA YAIANDIKIA BARUA KALI TFF KWA SABABU YA KELVIN YONDA


Simba Sports Club imesikitishwa na hatua ya Katibu Mkuu wa TFF kujichukulia mamlaka ya Kamati ya Katiba na Sheria na kuamua mustakabari wa suala la Kelvin Yondani kwa barua yenye kumb namba TFF/TECH/GC.12/62 ikijibu pingamizi la Simba Sports Club lililokuwa likitaka mgogoro huo uamuliwe na chombo husika.

Masikitiko hayo ya Simba Sports Club yanatokana na jinsi haki  na misingi bora ya uendeshaji wa mpira inavyoonekana kupindishwa waziwazi kwani Simba Sports Club imeshaandika barua nyingine mbili kwa Rais Tenga moja ya terehe 7/6/2012 yenye Kumb na SSC/5/6/02 ikilalamika juu ya uendeshwaji wa sakata zima la udanganyifu wa usajili wa mchezaji wa Simba Kelvin Yondani ambayo Rais alitoa maagizo kwa Katibu Mkuu na nakala kuja kwa Simba SC kwa barua pepe ya tarehe 8/6/2012 lakini baada ya kutofanyika utekelezaji wowote na badala yake watendaji wa TFF kuendelea kuongea katika vyombo vya habari wakisema mchezaji huyo ni mchezaji huru, Simba Sports Club iliandika barua nyingine kwa Rais Tenga juu ya kukosa imani na sekretarieti ya TFF  kwa barua ya tarehe 23/6/2012 yenye kumb na. SSC/24/6/02 jambo ambalo limeonekana wazi kwamba sekretarieti ya TFF haitendi haki kwa Simba kwa jinsi  ambavyo haikufanyia kazi barua mbili lakini Katibu Mkuu wa TFF amekuwa mwepesi wa kujibu pingamizi wakati si kazi yake ili mradi timu yake ya Yanga mabayo yeye ni mwanachama ifanikiwe jambo lake.

Katika barua ya pingamizi dhidi ya mchezaji Kelvin Yondani kutumiwa na klabu ya Yanga katika michezo ya kirafiki na ile ya CECAFA  ya tarehe 11/7/2012 yenye kumb namba SSC/1/7/02 Simba Sports Club iliomba suala la mchezaji huyo lipelekwe katika kikao cha kamati ya katiba na sheria ambayo muda wake wa kukaa bado kwani kamati hiyo inaweza kukaa baada ya wiki mbili za kufunga usajili na kupokea pingamizi mbalimbali lakini taarifa za uhakika ni kwamba kamati hiyo ilijaribu kuitishwa haraka haraka ili kulitolea suala hili uamuzi lakini corum haikutimia hivyo ikashindwa kutoa maamuzi lakini kwa ubabe Katibu Mkuu akaamua kujichukulia mamlaka yasiyokuwa yake na kumpa leseni ya Yanga Kelvin Yondani huku Simba ikipokea majibu tarehe 14/7/2012 kwa barua uwanja wa Taifa wakati mechi kati ya Yanga na Atletico imeshaanza na ipo dakika ya 18.

Katika barua yake ya kumuidhinisha Kelvin Yondani katibu mkuu kakiri kuwepo kwa mkataba wa Yondani na Simba unaoisha mei 31, 2012 na kakiri pia kupokea nyaraka ya makubaliano ya Simba SC na Kelvin Yondani lakini kwa sababu yeye si mwanasheria na ndio maana kazi hiyo ni ya kamati ya katiba na sheria amezitafsilia pande mbili za mkataba yaani Simba Sports Club na Kelvin Yondani nia yao wakati wanaingia mkataba kwamba mkataba utaanza tarehe 23 december 2012 na kuweka kiambatanisho cha sehemu ya kusaini ya Simba Sports Club ambayo kwa sababu za kibinadamu ilikosewa na inasomeka tarehe 23 december 2012.

Katibu Mkuu wa TFF ameshindwa/amejikataza kuusoma mkataba tangu mwanzo na kuona nia za pande za mkataba ni zipi kwani katika ukurasa wa kwanza mkataba unasoma kwamba umesainiwa tarehe 23/12/2011, pia mkataba unatambua uwepo wa mkataba wa pande hizo mbili unaoisha tarehe 31/5/2012 na pande husika katika mkataba zimeonyesha nia ya kuongeza mkataba mara tu ule wa awali unapoisha.

Katika kipengele cha kwanza mkataba umeshuhudia pande zikitamka waziwazi kwamba mkataba umeongezwa kuanzia (effective) tarehe 1/6/2012 mara tu mkataba wa awali unapoisha sasa inashangaza Katibu Mkuu anazitafsiria pande nia zao kwamba mkataba utaanza tarehe 23/12/2012 wakati mkataba umetamka waziwazi.

Pia sehemu aliposaini mchezaji Kelvin Yondani imeonyeshwa waziwazi kwamba kasaini tarehe 23/12/2011 hivyo kuacha hitimisho lisilo na shaka kwamba Katibu Mkuu wa TFF amekiuka na kujivika mamlaka yasiyo yake ili kutekeleza unazi wake wa Yanga.

Simba Sports Club inakusudia kuyakatia rufaa maamuzi haya ya Katibu Mkuu wa TFF na ipo  tayari kufuata mikondo yote ya sheria mpaka haki ipatikane kwani itatumia taasisi za TFF kwanza na isiporidhishwa na maamuzi itapeleka suala hili CAF mpaka FIFA na jambo la kushukuru ni kwamba Shirikisho la TFF limeanza kujibu barua za Simba SC suala ambalo linaanza kutoa mwanga wa nia ya kutotenda haki lakini barua hizo zitasaidia kuwaonyesha watu wa nje kama tukifika huko jinsi mpira wa Tanzania unavyoendeshwa kinazi na viongozi wa Shirikisho.

Imetolewa na
Simba Sports Club

VIELELEZO VYA SIMBA 



No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate