EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 22, 2012

SPIDER MAN HATARINI KUWAKOSA MAFUNZO, NIZAR HATA JEZI HAVAI KESHO, BERKO, CHUJI, KIIZA NAO NJE NDANI



Said Bahanuzi 'Spider Man'
MSHAMBULIAJI tegemeo wa Yanga, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ yuko hatarini kuikosa mechi ya Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kesho dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar, kutokana na maumivu ya mgongo, wakat kiungo Nizar Khalfan yeye kwa asilimia 100 hatacheza kutokana na maumivu ya nyonga.
 
Kocha wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet amesema mchana huu kwamba, Nizar hatacheza kabisa, lakini wachezaji wengine watatu, Bahanuzi,  kipa Yaw Berko anayesumbuliwa na goti, kiungo Athumani Iddi ‘Chuji’ na Hamisi Kiiza wanaosumbuliwa na quadriceps wako kwenye hatihati kucheza.
Mtakatifu Tom amesema kwamba, 
Daktari wa Yanga, Sufiani Juma anaendelea kufuatilia afya za Bahanuzi, Kiiza, Berko na Chuji ili kuhakikisha wanakuwa fiti kwa ajili ya mechi ya kesho, lakini kwa Nizar kocha huyo wa zamani wa Namibia na Ethiopia, amekwishakata tamaa kumtumia kwenye mechi na Mafunzo.
 
Amesema sababu ya wachezaji wake kuumia mara kwa mara ni kutokana na kucheza mechi mfululizo na kulingana na kanuni za mashindano hayo, hawezi kutumia wachezaji zaidi ya 20, hivyo hana namna nyingine zaidi ya kupambana na hali hiyo.
Bahanuzi ndiye kinara wa mabao wa Yanga hivi sasa, hadi sasa akiwa amekwishaifungia timu hiyo mabao manne, hivyo kuingia kwenye mbio za kuwania kiatu cha dhahabu cha mashindano hayo, ambayo tayari kwenye kabati la Yanga kuna mataji manne yamehifadhiwa.
 
Mshambuliaji huyo mpya kutoka Mtibwa Sugar ya Morogoro, juzi alikaribia kuondoka na mpira uwanjani, kama si refa Dennis Batte kutoka Uganda kukataa bao lake moja siku ambayo alifunga mawili yaliyokubaliwa dhidi ya APR ya Rwanda, Yanga ikishinda 2-0, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
 
Katika mchezo huo, Kocha Tom alimpumzisha Bahanuzi dakika ya 72 na nafasi yake ikachukuliwa na Jerry Tegete, wakati Nizar Khalfan kabla ya hapo alimpisha Juma Seif ‘Kijiko’.
Wakati huo huo: Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), leo limesema kwamba mechi ya Yanga kesho itakuwa ya pili, kama ambavyo itakuwa kwa Simba keshokutwa.

RATIBA ROBO FAINALI
Julai 23, 2012
URA vs APR (Saa 8:00 mchana)
Mafunzo vs Yanga (Saa 10:00 jioni)
Julai 24, July
Atletico vs AS Vita (Saa 8:00 mchana)
Azam vs Simba SC (Saa 10:000 jioni)
Via Bin Zuberiblog.com

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate