EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 22, 2012

Watoto wawaburuza wazazi wao Polisi kwa kuwatelekeza na kusababisha waishi mitaani

Watoto watatu wa familia moja wamewafikisha wazazi wao katika Kituo Kikuu cha Polisi mjini Musoma , Kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto wakidai kutelekezwa na kuwafanya kuishi maisha ya kutangatanga mitaani ilhali wazazi wao wakiendelea na maisha yao bila ya kuwajali.

Wakizungumza nje ya kituo hicho cha Polisi, mmoja wa watoto hao aliyejitambulisha kwa jina la Justine Kichere alisema baba yao mzazi kwa kushirikiana na mama yao wa kambo ambaye hawakuweza kumtaja jina lake, waliwafukuza nyumbani kwa kuwatupia nguo zao kwa kile walichokieleza kudaiwa kuwa 'machokoraa’, yaani watoto wa mitaani.

Wakielezea chanzo cha tukio hilo la kufukuzwa nyumbani, Justine (14) anayesoma darasa la saba katika Shule ya Msingi Rwamlimi A katika Manispaa ya Musoma, alisema waliitwa na mama yao wa kambo akiwa na wadogo zake, James (13) na Gerald (12) na kuelezwa kuwa mama yao anaumwa na amelazwa Hospitali ya Mkoa, hivyo waende kumjulia hali.

Aliongeza kuwa, wakiwa njiani kuelekea hospitalini huku wakiwa hawapajui waliomba msaada katika gari moja na kueleza wanakwenda hospitali ya Mkoa na kupandishwa kisha kuelekea wasipokujua na walipofika na kuuliza waliambiwa wapo maeneo ya Ramadi.

Alidai baada ya kudaiwa kupotea, waliomba msaada wa kurudi nyumbani Musoma na kusaidiwa lakini mara baada ya kufika nyumbani bila kuulizwa kilichowasibu walitupiwa nguo zao nje na kutakiwa kuondoka nyumbani na watafute mahala pengine pa kuishi.

Justine alisema baada ya kufukuzwa na baba yao pamoja na mama yao wa kambo waliamua kwenda kwa mama yao ambaye alitengana na baba yao anayeishi maeneo ya Baruti na kukaa kwa muda wa siku mbili kisha mama yao kuwataka kurudi kwa baba yao kwa kuwaeleza kuwa, hana pesa ya kuwalisha wote watatu.

Kwamba, baada ya kuona hawana pa kwenda, waliamua kuishi mtaani kwa takribani wiki moja huku wakiwa wakilala katika jumba bovu eneo la Nyakato, lakini baada ya kuona maisha yakiendelea kuwa magumu, waliamua kwenda kituo cha Polisi ili kuweza kupata msaada zaidi.

Mtoto huyo aliongeza kuwa hilo sio tukio la kwanza kwa baba yao Kichere Sangi aliyemueleza kuwa ni mfanyabiashara wa duka la rejareja katika maeneo ya Kigera kufanya hivyo kwa kuwa alishawahi kumfukuza kaka yao, Geofrey Kichere aliyekuwa akisoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Bweri ambaye mpaka sasa hajulikani halipo.

Aidha watoto hao walisema lengo la kwenda katika kituo cha Polisi ni kutaka kupata msaada kwa kuwa maisha wanayoishi mtaani ni magumu na wameshindwa kwenda shuleni huku mmoja wao akiwa anakabiliwa na mtihani wa darasa la saba

Mwandishi wa habari hizi alifika katika ofisi ya dawati la jinsia na watoto katika kituo cha Polisi Musoma kutaka kujua hatima ya watoto hao na kuelezwa kuwa wanazo taarifa hizo na hatua waliyochukua ni kundika barua wa wito kwa wazazi ili kuelezea madai ya watoto hao.

HabariLeo

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate