EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 31, 2012

Wafanyakazi watangaza maandamano yatakayofanyika Dar es Salaam

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limetangaza maandamano ya amani yatakayofanyika Dar es Salaam wiki hii ili kupeleka malalamiko yake kwa Serikali ya kutokubaliana na sheria mpya ya mafao ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii (SSRA).

Sheria inayolalamikiwa na wafanyakazi inazuia wanachama wa mifuko hiyo kujitoa uanachama na kuchukua mafao yao mpaka wafikishe umri wa kustaafu kwa hiari wa kati ya miaka 55 na 59 na kwa lazima miaka 60 au wanapopata ulemavu wa kudumu.

Mratibu wa Kamati ya TUCTA ya Mkoa wa Dar es Salaam, Musa Mwakalinga jana alisema maandamano hayo yatafanyika Agosti 4 na yataanza saa 1.30 asubuhi katika ofisi za TUCTA makao makuu Mnazi Mmoja hadi ofisi za SSRA eneo la Makochi, Kinondoni barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Mwakalinga alisema maandamano hayo yatashirikisha wafanyakazi, wafanyabiashara na wakulima na kueleza kuwa wameshatoa taarifa Polisi kupata ulinzi ili kufikisha kilio chao, kwa kuwa mabadiliko hayo yataongeza umasikini kwa wafanyakazi pindi watakapoachishwa au kuacha kazi, “Sisi tunachofanya ni maandamano ya amani, hivyo hatuna haja ya kuomba kibali, ila tulichofanya ni kuwapa taarifa tu ili watupe ulinzi,” alisema Mwakalinga.

Katibu Mkuu wa TUCTA, Nicholaus Mgaya alisema wanabariki maandamano hayo na wanataka mabadiliko ya haraka yafanyike kwenye sheria hiyo ya hifadhi ya jamii, ili fao la kujitoa lirejeshwe.

Alisema wadau na TUCTA hawakuona kifungu hicho cha sheria kwa kuwa hakikujitokeza kwa uwazi kwenye muswada au kama ilivyoelezwa na SSRA, baada ya sheria kupita na kifungu pekee cha muswada kilichotaja suala la mafao ya kujitoa ni cha 107 kilichotoa mapendekezo ya kufuta fao la kujitoa kwa mfuko wa PPF.

Hivyo alisema wadau na vyama vya wafanyakazi walielewa kuwa kifungu hicho kinalenga kufuta fao la kujitoa kwa mfuko wa PPF tu, ambao ndio pekee uliokuwa na fao hilo na kwamba malipo ya kujitoa yangeendelea kutolewa kama ilivyokuwa ikifanyika kwa mifuko mingine.

Kutokana na hilo, alisema TUCTA inataka uandaliwe utaratibu mwafaka utakaohakikisha mwanachama anayeshindwa kuendelea na uanachama wa Mfuko anarejeshewa michango yake na ya mwajiri pamoja na riba mara tu anapokoma uanachama wa mifuko hiyo.

lisema TUCTA haitasita kuchukua hatua za kisheria, endapo mamlaka itaendelea kushikilia msimamo wake wa kubakiza kifungu hicho kinachomtaka mwanachama wa mfuko afikishe miaka 55 ndipo alipwe mafao.

Aidha, alisikitishwa na kushangazwa kuwahishwa kutangazwa kwa mabadiliko ya sheria ya hifadhi ya jamii, huku mchakato wake ukiwa haujakamilika baada ya kuridhiwa na Rais, kama vile kupita kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali, akisema huo ni ukiukwaji mkubwa wa taratibu, “Hali hii inatupa shaka kuwa huenda sheria hiyo ikawa na mabadiliko ambayo wadau hatukuyaridhia, jambo ambalo TUCTA kamwe hatutalikubali,” alisema.

Alisema TUCTA inataka SSRA kuchukua jukumu la kutoa elimu kwa wanachama kuhusu sheria hiyo mpya ili kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima.

via HabariLeo

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate