EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 8, 2012

MAJONZI BONGO MOVIES


 
Marehemu Rose enzi za uhai wake.
Odama (katikati) akiaga mwili wa marehemu.
Wolper (wa nne kulia) na jamaa wengine wakiwa msibani hapo.
Hashim Kambi (kushoto) nae akiwa msibani hapo.
Na Erick Evarist
KAMBI ya wasanii wa filamu nchini maarufu kama Bongo Movies imepata pigo zito baada ya kiungo muhimu katika tasnia hiyo, Rose Thomas Maguzo kuaga dunia.
Marehemu Rose aliyefariki Agosti 03, mwaka huu, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikuwa ni mtaalamu wa make up (vipodozi) kwa wasanii mbalimbali nchini.
Taarifa kutoka kwa msemaji wa familia hiyo ilieleza kwamba, marehemu Rose alifariki baada ya kuugua ugonjwa wa homa ya mapafu.
MKANGANYIKO WA MAZIKO
Awali ilielezwa kuwa, marehemu Rose angeagwa Agosti 5, mwaka huu, Muhimbili kabla ya kupelekwa kuzikwa katika eneo ambalo lingetangazwa hapo hapo Muhimbili.
Ndugu, jamaa, marafiki na mastaa wengi wa filamu walifika hospitalini hapo mapema ili kutoa heshima za mwisho kwa mwenzao lakini wakiwa hapo wakaelezwa kwamba mwili utaagwa katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mabibo – External kwenye misa ya mazishi.

KANISANI HOLA!
Hata hivyo, inaelezwa kuwa baada ya watu kufika kanisani walipoelekezwa hapakuwa na dalili zozote za kuwepo kwa ibada ya mazishi jambo lililowashangaza.
“Unajua tukiwa Muhimbili, mjomba wa Rose (marehemu) alituambia twende kanisani, lakini tukiwa hapo tukasikia tena si hapo, bali msiba unafanyika nyumbani kwa baba wa marehemu Mabibo - Garage, ikabidi tugeuze tena kwenda huko,” alisema mmoja wa wasanii wa filamu ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.
Akaongeza: “Tulipofika nyumbani kwa baba yake tulikuta taratibu za kuaga zinaendelea, lakini kuna baadhi ya wasanii hawakuweza kupata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kutokana na kuchelewa.”

MASTAA KIBAO
Baadhi ya mastaa waliohudhuria kwenye mazishi ni pamoja na Jacob ‘JB’ Steven, Single ‘Richie’ Mtambalike, Jacqueline Wolper, Yusuph ‘Angelo’ Mlela na Ruth ‘Mainda’ Suka.
Wengine ni Jenifer ‘Odama’ Kyaka, Rachel ‘Recho’ Haule, Hashim ‘Wingo’ Kambi na wengine wengi ambao walionesha ushirikiano mkubwa katika shughuli hiyo ya kumpumzisha Rose.
Rose alipuzishwa katika nyumba yake ya milele, alasiri ya Jumapili, Agosti 05, mwaka huu, katika Makaburi ya Mabibo.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe – Amina.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate