EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, September 3, 2012

Kifo cha Daudi Mwangosi: Unyama huu hadi lini?

Taarifa kwa vyombo vya habari, Septemba 03, 2012

Sikika imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mwandishi wa habari wa kituo cha Channel Ten mkoani Iringa, Daudi Mwangosi.  Kwa mujibu wa vyombo vya habari, marehemu Mwangosi alikuwa kazini akitimiza wajibu wake wa kutafuta habari. Tumestushwa zaidi baada ya kuona picha za mnato zikionyesha jinsi ambavyo mtu anayedaiwa kuwa ni mwandishi huyo akishambuliwa na idadi kubwa ya askari polisi na baadae kupoteza maisha.

Katika siku za karibuni, tumeshuhudia ongezeko la matumizi ya nguvu kupita kiasi yanayofanywa na jeshi la polisi, ambayo siyo tu yanasababisha uharibifu mkubwa wa mali za wananchi bali pia baadhi yao kupoteza maisha. Mfano, mwezi uliopita, tuliarifiwa kuwa kijana aliyeuawa mkoani Morogoro alikuwa akiuza magazeti na wala hakuhusika katika vurugu kwa namna yoyote. Vivyo hivyo, marehemu Mwangosi alikuwa akitimiza wajibu wake wa uandishi wa habari.

Uhai ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania. Hivyo, ni jukumu la polisi kulinda maisha na uhai wa wananchi wote bila kujali itikadi au kazi zao. Hakuna sheria inayohalalisha kujeruhi, kutesa wala kuua mwananchi yeyote kwa sababu tu ati amekataa kutii amri ya polisi. Sikika inasikitishwa zaidi na utamaduni unaozoeleka ndani ya jeshi la polisi kwamba matukio ya kujeruhi, kutesa au  vifo ni halali iwapo wanasiasa au wananchi hawakutii amri.

Kwa mtazamo wetu, amri ya serikali au polisi haitakiwi kuwa juu ya Katiba inayolinda haki ya  kuishi. Hivyo, kisingizio cha kukiuka amri ya polisi hakitakiwi kuwa sababu ya kujeruhi wala kuua binadamu yeyote. Hata kama polisi watatoa maelezo kukanusha kuwa picha ya mtu anayeteswa si mwandishi, je wanayo haki ya kumjeruhi, kumtesa au kumdhalilisha mtanzania yeyote kama inavyoonekana kwenye picha hizo?

Tangu matukio haya ya kujeruhi, kutesa na hata kuua wananchi yalipoanza, hakuna hatua za dhati zilizochukuliwa na serikali wala jeshi la polisi. Vitendo hivi vinavyofanywa na polisi siyo tu vinapunguza imani ya jeshi hilo kwa wananchi, bali pia vinakiuka wajibu wa msingi wa jeshi hilo ambao ni kulinda usalama wa raia.

Ni matumaini yetu kwamba waliohusika na kifo cha Daudi Mwangosi na watanzania wengine waliopoteza maisha katika mazingira ya aina hii, watachukuliwa hatua stahiki. Pia, maaskari wanaoonekana katika picha hizo wakimtesa na kumnyanyasa raia wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ili iwe funzo kwa wengine.

Tunatoa pole nyingi kwa familia na ndugu wa marehemu Daudi Mwangosi pamoja na tasnia ya habari hapa nchini.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi, Amen.
Bw. Irenei Kiria

Mkurugenzi Mtendaji, Sikika, S. L. P 12183 Dar es Salaam,
Simu: +255 222 666355/57, Nukushi: 2668015, Barua pepe: info@sikika.or.tz, Tovuti: www.sikika.or.tz

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate