EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 7, 2012

Majambazi yapora magunia ya fedha Benki, Dar es Salaam


Na Raymond Kaminyoge Zaina Malongo, gazeti la Mwananchi - Dar es Salaam -- WATU wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamevamia na kutumia mbinu za uhalifu wa hali ya juu na kupora magunia ya fedha kutoka Benki ya  Biashara ya Afrika (CBA), iliyopo  barabara ya Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo linaloweza kufananishwa na filamu za kimafia, lilitokea jana kati ya saa 2.30 na saa 2.45 asubuhi. Waliondoka na magunia hayo wakiwa wameyapakia kwenye magari yao ya kifahari, bila kuua wala kujeruhi mtu. 

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alithibitisha tukio hilo na kusema fedha walizoiba zinakadiriwa kuwa zaidi ya Shilingi Milioni 400, “Hatufahamu kiasi kamili lakini, tulivyowahoji maofisa wa benki wanasema ni zaidi ya Sh400 milioni ambazo zimeibiwa,” alisema Kova na kwamba  tayari meneja wa benki, msaidizi wake na mlinzi aliyekuwa zamu wanashikiliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema watuhumiwa hao wa ujambazi, waliingia kwenye benki hiyo, huku wakiwa wamevalia vitambusho vya benki kujifafanisha na wafanyakazi wa benki hiyo, mbinu ambayo iliwahadaa  watu waliokuwa kwenye eneo hilo wasishtuke kwa lolote. Vitambulisho hivyo viliwafanya walinzi wa benki hiyo kutokuwa na wasiwasi na watuhumiwa hao, jambo lilitoa fursa kwao kutekeleza uhalifu katika mazingira ya urahisi zaidi. Baada ya kuingia ndani ya benki, majambazi hao wakiwa na bastola yaliwaweka chini ya ulinzi walinzi wa benki hiyo. 

Wakati hayo yakitokea mmoja wa majambazi hao aliamuru wafanyakazi wa benki hiyo kuendelea kuwakaribisha wateja wao na kila aliyekuwa akiingia aliwekwa chini ya ulinzi. Mtuhumiwa mwingine wa ujambazi akiwa na bastola, alimfuata  mtunza funguo wa chumba maalum cha kuhifadhia fedha na chumba cha Mashine za Kutolea Fedha (ATM) na kumwambia, atoe funguo, “Tena jambazi huyo alimtaja kwa jina mtunza funguo huku akisema naomba funguo za strong room tumekuja kuchukua fedha zetu,” alisema mmoja wa mashuhuda akimkariri jambazi huyo na kusema alipewa funguo bila kizuizi. 

Baadaye majambazi hao walifanikiwa kufungua kwenye vyumba hivyo na kuchukua fedha zote na, kuzihifadhi kwenye magunia manne. Wakati shughuli hiyo ikiendelea majambazi wengine waliharibu mitambo ya kamera zinazoonyesha watu wanaoingia na kutoka kwenye benki hiyo, “Tunajua mnaturekodi kwenye kamera zenu na sisi tunaifahamu vizuri teknolojia hii, ndiyo maana tunalazimika kuharibu mtandao mzima,” mmoja wa jambazi alikaririwa akisema huku akifungua mtambo wa kamera.

Baada ya kumaliza kuharibu mitambo ya kamera, waliondoka na maguni ya fedha na kwenda walikoegesha magari yao ya kifahari na kupakia.

Walioshuhudia walisema, majambazi hao walikuwa wakitumia magari matatu ya aina ya Toyota Land Cruiser, Nissan Patrol na Toyota Noah na kwamba, wakati wakitekeleza ujambazi huo madereva wote walikuwa wamebaki kwenye magari hayo yaliyokuwa yameegeshwa karibu na benki hiyo. Baada ya magari hayo kupakia magunia hayo, madereva hao waliyaondoa magari hayo kwa kasi kuelekea eneo la katikati ya jiji. Wameendelea kusema kwamba wakati majambazi hayo yanaondoka katika eneo hilo mnamo  saa 2.45 asubuhi, hakukuwa na msongamano wa magari katika barabara ya Nyerere kama kawaida, “Unafahamu muda huu eneo hili huwa na msongamano wa magari lakini, tunashangaa wakati tukio hili linatokea hakukuwa na magari hadi tukadhani labda kuna msafara wa viongozi,” alisema mmoja wa mashuhuda.

Baada ya tukio hilo kumalizika maofisa wa Jeshi la Polisi walifika katika benki hiyo iliyopo kwenye jengo la Jamana wakiongozwa na Kamanda wa Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova.


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate