EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 7, 2012

Tendwa ni mkurupukaji wa siku nyingi sana - Prof. Lipumba


Baada ya Msajili wa vyama vya siasa Bwana John Tendwa juzi kusema kuwa vyama vya siasa vitakavyobainika kusababisha mauaji vitafutiwa usajili kutokana na kukiuka sheria, kanuni na utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za siasa nchini, MWENYEKITI wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba, amemjia juu Msajili wa Vyama Vya Siasa Nchini, John Tendwa na kusema kauli yake aliyoitoa dhidi ya vyama vya siasa ni ya kukurupuka.

Profesa Lipumba alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na gazeti la MTANZANIA jana kwa simu na kusema kuwa, kauli ya Tendwa ya kutishia kufuta vyama vya siasa imejaa vitisho.

“Tendwa ni mkurupukaji wa siku nyingi sana, anawezaje kusema atakifuta chama cha siasa wakati yeye hana chombo cha kufanya uchunguzi, suala la kifo ni suala la jinai yeye anasemaje anafuta chama? Ukiangalia vifo vingi au hiki kifo cha Mwandishi Daudi Mwangosi ni wazi polisi wamehusika kwa sababu bomu limehusika na lile bomu lilitoka kwa polisi na picha zimeonyesha kwamba polisi ndiyo wamehusika. Sasa kwa mazingira haya, yeye anawezaje kusema anakifuta chama kilichokuwa na shughuli zake katika eneo hilo?,” alihoji Profesa Lipumba.

Alisema kauli ya Tendwa ina lengo la kuhujumu shughuli za kisiasa hapa nchini na kwamba inapaswa kupingwa na vyama vyote vyenye lengo la kuimarisha demokrasia.

“Hii kauli yake ni ya kifisadi kwa sababu anataka watu wamuabudu, unapoona mtu anataka kuabudiwa basi ujue kabisa ana sifa zote za kifisadi kwa hiyo huyu ni fisadi hana tofauti na mafisadi wengine ambao wanadhuluma rasilimali za nchi. Huyu amekuwa mkurupukaji wa siku nyingi sana, hakuna asiyemjua na kauli yake hii ni kutaka kufinya demokrasia, yeye aache vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake, ili kufahamu ni nani amehusika katika matukio hayo ambayo yamesababisha vifo vya raia. Yeye afanye kazi yake ya kusajili vyama na si kuingilia masuala ya jinai, ambayo yana mamlaka husika na kufahamu kifo kimesababishwa na nani wala si kusema unafuta vyama vya siasa, hii ni kauli isiyokuwa na mashiko kabisa,” alisema Profesa Lipumba.

Juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Tendwa alisema atavifuta vyama vya siasa vinavyosababisha mauaji wakati wa shughuli zake za kisiasa.

Pamoja na mambo mengine, Tendwa alikuwa akizungumzia kifo cha Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel Ten, Daudi Mwangosi aliyefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa bomu na askari polisi katika kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa mwanzoni mwa wiki hii.

via Mtanzania


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate