EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, September 22, 2012

Mganga Mkuu ajifungia baada ya ndugu kudai maiti ya ndugu yao .

ENEO la Hospitali ya Mwananyamala katika Manispaa ya Kinondoni, jana liligeuka la vurugu kwa muda, baada ya ndugu kuchachamaa wakitaka kukabidhiwa mwili wa mpendwa wao baada ya kuelezwa kuwa, umeshachukuliwa tayari kwa maziko mkoani Tanga.
Wanandugu hao wa jijini Dar es Salaam, waliwasili hospitalini hapo jana asubuhi kwa lengo la kukamilisha taratibu za kumzika ndugu yao kwenye makaburi ya Mikocheni, Manispaa ya Kinondoni.

Tukio hilo lililosababisha mtafaruku mkubwa kati ya wanandugu na madaktari katika hospitali hiyo na hata kuwalazimu polisi wa kituo cha Mwananyamala kuingilia kati, limethibitishwa na Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela na kuongeza kuwa, limechangiwa na uzembe wa mhudumu katika chumba cha kuhifadhia maiti.Aliongeza kuwa, juhudi za kuufuatilia mwili huo zinaendelea na kwamba, kama utakuwa umezikwa, kitaombwa kibali maalumu cha mahakama ili ufukuliwe na kisha ukabidhiwe kwa ndugu.
Awali, Fredrick Nkenzidyo ambaye ni kaka wa marehemu, alisema ilikuwa wauchukue na kuuzika mwili wa marehemu katika makaburi ya Mikocheni jana, lakini cha kushangazwa waliambiwa kuwa mwili huo haupo.lisema kuwa akiwa hospitalini hapo, alipewa taarifa kuwa kuna watu waliwasili asubuhi na kujitambulisha kuwa ni ndugu wa marehemu na kuondoka na mwili huo.Akizungumzia kuhusiana na marehemu alisema ndugu yao alikuwa akiitwa Ntimaruku Nkenzidyo na alikuwa mlinzi wa kampuni ya Group 7 Security na alikutwa na mauti kufuatia ajali ya gari iliyotokea Masaki, Dar es Salaam Septemba 17, mwaka huu.

Alisema kuwa baada ya ajali hiyo, mwili wake ulipelekwa hospitalini hapo kwa ajili ya kuhifadhiwa na hata walipokuwa wakifika kuangalia mwili walikuwa wakiukuta katika sare zake za kazi za kiuaskari.Akizungumza kwa jazba mbele ya polisi waliofika hospitalini hapo, alisema wameelezwa mwili wa ndugu yao umepelekwa Tanga na watu walisingizia kuwa ni ndugu yao na hatimaye kukabidhiwa mwili wa marehemu.Hata hivyo, baadaye ilibainika kuwa hakukuwa na ujanja wa kuusafirisha mwili huo, bali kulikuwa na makosa yaliyoanzia kwa wahudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti.

Hata hivyo, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dkt. Sophinias Ngonyani hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo, huku akionekana kuzunguka huku na huko kutafuta chanzo cha tukio hilo.Kufikia mchana, huku ndugu wakipaza sauti za kuutaka mwili wa ndugu yao kiasi cha kuwapa kazi ya ziada askari polisi, busara ilitumika kwa pande tatu, yaani uongozi wa hospitali, ndugu wa marehemu na polisi kuingia katika chumba maalumu kwa ajili ya majadiliano ambayo yalifikia mwafaka wa kusubiri juhudi za kuurudisha mwili kutoka Tanga.

via HabariLeo





No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate