EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, October 30, 2012

CHADEMA: Tumeshinda.

WASEMA NAPE ANAPIGA VUVUZELA BILA TATHMINI.Habari na Shehe Semtawa
WAKATI Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akitambia ushindi mkubwa walioupata katika kata 22 kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika Jumapili, CHADEMA wamemtaka aache kuwa kama vuvuzela, wakidai wao ndio washindi.
Chama hicho kimesema kutokana na idadi kubwa ya kura walizopata katika kata zote hata zile ambazo hawakushinda ni dhahiri kuwa ngome yao inazidi kuimarika maeneo mengi nchini kiasi cha kuweza kuwanyang’anya CCM kata.
Kauli ya CHADEMA ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa (Bavicha), John Heche, wakati akijibu tambo za Nape na kudai kuwa kada huyo ni sawa na vuvuzela, kwani kama angekuwa anafanya tathmini angeweza kubaini ni kwanini wananchi wanazidi kuikataa CCM.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Mtaa wa Lumumba, Nape alisema kuwa idadi kubwa hiyo ya madiwani waliyopata ni ishara kwamba CCM bado kinakubalika kwa wananchi na kitaendelea kushinda katika chaguzi zijazo.
Kauli ya Nape inakuja ikiwa ni siku moja tangu kumalizika kwa uchaguzi huo mdogo kwenye kata 29, ambapo CCM iliweza kurejesha kata zake 22 na kupoteza tatu zilizochukuliwa na CHADEMA iliyoshinda kata tano na CUF ikipata kata moja.
Nape alisema ushindi huo umetokana na chama hicho kuhubiri amani mara kwa mara katika mikutano yake, tofauti na vyama vingine ambavyo sera zao ni za kumwaga damu, kitendo ambacho wananchi hawakikubali.
“Ushindi huu unadhihirisha kuwa hata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 chama chetu kitawashinda wapinzani,” alijigamba.

Nape aliponda opereshini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayoendeshwa na CHADEMA nchi mzima, akidai inaandamana na vurugu na kwamba haitakisaidia chama hicho.
Alisema operesheni hizo zimekuwa zikisababisha vurugu na vifo katika maeneo mbambali kilipopita chama hicho.
“Juhudi zote walizofanya Katibu Mkuu, Dk. Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, hazikuzaa matunda, hiyo inatokana na siasa chafu za vurugu, hivyo wananchi wameamua kukinyima ushindi,” alisema.
Nape pia alisema kuwa CCM inalaani vurugu zilizotokea katika baadhi ya maeneo kulikofanyika uchaguzi huo kwamba huo si utamaduni wa Watanzania.

Alisema kuwa uchaguzi ulifanyika katika kata 29 na kati ya hizo 27 zilikuwa za CCM na mbili za CHADEMA, hivyo wao waliweza kuzirejesha kata zao na kutwaa nyingine tatu.
“Nape aache kupiga kelele kama vuvuzela bali wakae chini na kujifanyia tathmini, wajiulize ni kwanini watu wanazidi kuwakataa. Sisi kwanza tumeweka historia tangu mfumo wa vyama vingi uanze kwa kusimamisha wagombea kwenye kata zote, tumeweza kutetea kata zetu mbili na kuchukua za CCM tatu,” alisema.
Katika kujibu hoja hizo, Heche alisema kuwa wanachokifanya CCM sasa ni sawa na kufiwa na watoto halafu ukajipongeza kwa wale waliobaki, huku akibainisha kuwa uchaguzi huo umewawezesha CHADEMA kufika katika vijiji 116 na kusimika matawi.

Kuhusu madai ya Nape kwamba Operesheni ya M4C haikufua dafu katika uchaguzi huo kwa vile inachochea vurugu, alisema kuwa taarifa za magazeti mengi ya jana zilieleza bayana kuwa vitendo vya vurugu kwenye uchaguzi vilisababishwa na CCM kwa kuwashambulia wafuasi wa CHADEMA.
“CCM ni chama cha rushwa na wamechaguana kwa rushwa hata Mwenyekiti wao Jakaya Kikwete amekemea hilo kwenye mikutano ya UVCCM na UWT, sasa kwa mantiki hiyo Nape apime mwenyewe nani kapoteza na kama anafikiri tunafanya mzaha, basi angoje mwaka 2015,” alisema.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate