EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 21, 2012

Askari wahukumiwa kunyongwa hadi kufa askari wawili wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na mmoja wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la kumuua kwa kusudia, Swetu Fundikira.

Na Happiness Katabazi na Betty Kangonga.
HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imewahukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa askari wawili wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na mmoja wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la kumuua kwa kusudia, Swetu Fundikira.
Askari hao MT 1900 Sajenti Roda Robert (42) wa JKT, Kikosi cha Mbweni, MT 75854 Koplo Ally Ngumbe (37) wa JWTZ, Kikosi cha Kunduchi na MT 85067 Koplo Mohamed Rashid wa JKT Mbweni.

Washitakiwa hao walidaiwa kumpiga na hatimaye kumuua kwa makusudi Fundira Januari 23, majira ya saa 7:30 usiku wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam na kufariki dunia usiku wa kuamkia Januari 24 mwaka 2010, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu.
Sweti Fundikira ni mtoto wa mdogo wa Mwanasiasa Maarufu nchini, marehemu Chifu Abdallah Fundikira.

Hukumu hiyo ambayo inaweza kukomesha vitendo vya askari kujichukulia sheria mkononi dhidi ya raia, ilitolewa jana na Jaji Zainabu Muruke.
Jaji Muruke alisema baada ya kusikiliza kesi hiyo, ameridhika na ushahidi uliotolewa na mawakili wa upande wa Serikali ambao ulidai kuwa washitakiwa walitenda kosa hilo la mauji kinyume na kifungu cha 196 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002.

Akisoma hukumu hiyo iliyovuta hisia za wengi mahakamani hapo, Jaji Muruke alisema ingawa hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonesha washtakiwa hao kuwa ndiyo waliomua marehemu (Fundikira), ushahidi mazingira unaonesha pasipo shaka walihusika na mauaji hayo.
“Sheria ipo wazi na inaanisha kuwa ukiondoka au ukionekana na mtu kwa mara ya mwisho na baadaye mtu huyo uliyeondoka naye akapata madhara au amekutwa amekufa, wewe uliyeondoka naye ndiyo utawajibika kisheria na madhara yaliyompata mtu huyo;

“Japo kuwa ushahidi uliotumiwa na upande wa mashitaka katika kesi hii ni wa mazingira, lakini umeweza kuthibitisha kesi yao, upande wa utetezi nao umeweza kutoa ushahidi wenye matundu mengi na unaokatika katika sana na ambao umeshindwa kuudhoofisha ushahidi uliotolewa na upande wa jamhuri dhidi ya washtakiwa, ’alisema jaji Mruke.

Aidha, alisema Jamhuri imeweza kuthibitisha kosa la mauaji, hivyo mahakama imewaona washtakiwa wote wana hatia ya kumuua Swetu Fundikira.
Hata hivyo, Jaji Muruke kabla ya kutoa adhabu hiyo alimpa nafasi wakili Karoli Muluge pamoja na washtakiwa kusema lolote kabla ya kuwapatia adhabu hiyo.
Wakili Muluge aliiomba Mahakama iwape adhabu ndogo kutokana na mazingira ya kesi hiyo, umri wa washtakiwa kwani bado ni vijana, nguvu kazi ya taifa na familia zao zinawategemea.

Naye mshtakiwa wa kwanza, Sajenti Robert aliiomba Mahakama impunguzie adhabu akidai kuwa mama yake ni mjane na anamtegemea, pia ana watoto wadogo.
Hata hivyo Jaji Muruke alilamuamuru mshtakiwa wa pili, Koplo Ngumbe kukaa chini baada kuanza kujitetea kuwa ametiwa hatiani kimakosa na anamwachia Mungu.

Kwa upande wake mshtakiwa wa tatu, Koplo Rashid aliiomba mahakama imuonee huruma na impunguzie adhabu akidai kuwa bado ni mdogo na hilo ni kosa lake la kwanza.
Akitoa adhabu, Jaji Muruke alisema ni kweli maombi ya mshtakiwa wa kwanza yanatia huruma na kwamba mshtakiwa wa tatu hata kumbukumbu zinaonesha bado ni mdogo, pia hilo ni kosa lake la kwanza, lakini alisema kuna roho iliyopotea.

“Sheria ipo wazi kabisa mshtakiwa yoyote anayepatikana na hatia adhabu yake ni moja tu ambayo ni kunyongwa hadi kufa na hakuna mbadala wa adhabu hiyo…hivyo mahakama hii kwa kauli moja inatamka kuwa washitakiwa wote wa tatu mahakama hii imewahukumu adhabu ya kifo hivyo, mtanyongwa hadi kufa,” alisema Jaji Muruke:

Baada ya kutoa adhabu hiyo Jaji Muruke alitoka katika chumba cha mahakama na ghafla ndugu wa marehemu Fundikira waliangua vilio ndani ya ukumbi wa mahakama, kama vile walikuwa msibani.
Ndugu wawili wa marehemu, Mwasiti Fundikira ambaye ni Dada wa marehemu na Shelina Hamisi (mpwa wa marehemu) walianguka chini na kuzirai kwa muda hali iliyowalazimu watumishi wa mahakama kuwapatia huduma ya kwanza kwa kuwapepea hadi waliporejea katika hali ya kawaida.

Mke wa marehemu, aliyejitambulisha kwa jina la Lucy ambaye aliachwa akiwa mjamzito, alisema hakuamini kama haki ingetendeka kwani mpendwa wao aliuwawa kinyama.
Hata hivyo wakili wa washitakiwa hao, Muluge alisema hakuridhika na hukumu hiyo na kwamba atakata rufaa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate