EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 21, 2012

KATIBU mkuu mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdullahman Kinana amesema kuwa wanachama na wafuasi wa chama hicho, wasitarajie miujiza CCM.

KATIBU mkuu mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdullahman Kinana amesema kuwa wanachama na wafuasi wa chama hicho, wasitarajie kwamba amekuja na miujiza katika kukabiliana na matatizo yaliyomo ndani ya chama hicho tawala.
Kinana alitoa kauli hiyo jana wakati akijibu maswali katika kipindi cha Jenerali On Mondey, kinachoongozwa na mwandishi wa habari nguli, Jenerali Ulimwengu, na kurushwa na kituo cha televisheni cha DTV cha jijini Dar es Salaam.

Alisema tangu ateuliwe kuwa Katibu Mkuu, amekuwa akipata salamu nyingi za pongezi kutoka kwa wanachama wa kada mbalimbali, wakiwemo waliokata tamaa na kumwambia sasa wanarudi kwenye chama baada ya yeye kushika nafasi hiyo.
“Wapo wanachama wengi waliokata tamaa na hata wale waliohamia upinzani, wamenipigia na kunipa pongezi na kusema kwamba sasa wako tayari kurudi CCM na wana matarajio makubwa sana kutoka kwangu.

Mimi nawaambia wasitarajie miujiza kwamba nimekuja na dawa ya matatizo yote ya CCM, lakini nawahakikishia nitasimamia utekelezaji wa maamuzi yote ya chama,” alisema Kinana.
Kada huyo maarufu ndani ya CCM alisisitiza kuwa hajaja na miujiza bali ataongoza kwa kufuata katiba na kubwa kuliko yote ni kusimamia utekelezaji wa maazimio ya vikao vya chama.
Akitolea mfano wa maazimio ya Mkutano Mkuu wa CCM uliomalizika hivi karibuni, Kinana alisema atahakikisha anasimamia utekelezaji wake.

Baadhi ya maazimio ya mkutano huo uliomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma ni pamoja na kuitaka Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kuendelea na zoezi la kuwabaini na kuwaondoa viongozi na watendaji wa chama wanaoenda kinyume na maadili ya viongozi-wanaokipaka chama matope.
Mkutano Mkuu huo, pia uliiagiza serikali kuwachukulia hatua kali na za haraka viongozi na watendaji wa serikali ambao ni wala rushwa, wabadhirifu na wanaotumia vibaya madaraka yao.
Katika kushughulia nidhamu na uwajibikaji wa viongozi wa chama, Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Philip Mangula, alisema juzi kuwa hawatasubiri uamuzi wa mahakama katika kushughulikia wala rushwa na mafisadi kwani chama kinaweza kuchukua hatua zake mara moja.

Sifa moja kubwa anayotajwa kuwa nayo Kinana ni msimamo mkali dhidi ya masuala ya ufisadi na kubwa zaidi anatajwa kuwa bingwa wa mikakati ya kisiasa ndani ya chama hicho.
Kinana ndiye aliyeongoza kampeni za Benjamin Mkapa mwaka 1995, dhidi ya Augustine Mrema, aliyekuwa mwanasiasa maarufu na aliyekubalika kwa wakati huo.
Tangu wakati huo, Kinana amekuwa akiongoza kampeni za urais na mtu anayependa kusimamia mawazo anayoamini ni sahihi, lakini akiwa tayari kuunga mkono hoja zenye lengo la kukijenga chama hicho.

Kuhusu kudhibiti makundi yanayotaka urais ambayo yamesababisha mpasuko mkubwa ndani ya chama, Kinana alisema uongozi mpya utadhibiti kasi ya wagombea na kwa sasa inawataka waache kuwapotezea wananchi muda kwa kufikiria urais mwaka 2015 badala ya kufikiria maendeleo.
“Kuna mambo mengi ya kufikiria kwa sasa hasa masuala ya uchumi na namna ya kuwakwamua wananchi kiuchumi, muda wa urais haujafika na wanaotaka kugombea wasubiri hadi Mei 2015,” alisema Kinana.

Katibu Mkuu huyo aliyerithi mikoba ya Wilson Mukama aliwataka wana CCM kushirikiana na kuvunja makundi hasa baada ya uchaguzi wa ndani kumalizika.
Pia alisema kuanzia leo, viongozi wapya wa sekretarieti wataanza kufanya ziara mikoani kuhimiza na kuimarisha uhai wa chama hicho ambacho katika siku za hivi karibuni, kimepoteza mvuto.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate