EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, November 5, 2012

Mwanachuo wa Musoma Utalii achomwa kisu kwa wivu wa mapenzi.

Habari hii imeandikwa na Pascal Michael, Musoma, na imeshirikishwa kwetu na Magiri Paul wa wotepamoja.com

Mwanachuo wa Musoma Utalii aitwaye Rose Kanyambo  (21), alishambuliwa kwa visu mgongoni na ubavuni na mtu anayedaiwa  kuwa ni mpenzi wake ambaye pia ni mwanachuo, baada ya kukataliwa kuendeleza urafiki.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Mara, Irege Ngaregeza ametibitisha kumpokea mgonjwa huyo siku ya Ijumaa, Novemba 2, mwaka huu ambapo binti huyo alikuwa na jeraha la kuchomwa kisu mgongoni na ubavuni alifika hospitali hapo katika hali mbaya lakini juhudi za madaktari za kuokoa maisha yake zilifanikisha hali yake kuimarika.


Akizungumza na waandishi wa habari kwa taabu wodini, Rose alisema kuwa siku ya Ijumaa majira ya saa mbili asubuhi akiwa chuoni maeneo ya Kamunyonge katika Manispaa ya Musoma, ghafla kijana aitwaye John Ogolla alitokea  chuoni hapo na kuanza kumshambulia kwa kumchoma kisu mgongoni mara mbili  na ubavuni na kutokwa na damu nyingi. 

Rose anasema alifanikiwa kukimbia hadi alipokuwa anaishi, umbali mchache kutoka chuoni na kisha kudondoka chini baada ya nguvu kumuishia. Anasema majirani walipomsaidia na kufanya jitihada za kumpeleka hospitalini.

Binti huyo alieleza chanzo cha kuchomwa kisu ni kumkataa kijana huyo kuhusiana na uhusiano wa kimapenzi. Kijana huyo amekuwa akimlazimisha mara kwa mara kuwa na uhusiano wa kimapenzi lakini yeye hakutana na ndipo alipomjeruhi.

Hata hivyo, baadhi ya majirani na wanachuo  walisema kuwa  Rose na John walikuwa na mahusiano ya muda mrefu na kijana huyo amekuwa akimsaidia  mambo mengi sana lakini ghafla mpenzi huyo alibadilika na kumkataa bila sababu za msingi.


Inasemekana Ogolla baada ya kutekeleza tukio hilo, “alikuwa ameandaa barua ambayo aliandika ya ama kufa yeye au Rose Kanyambo na pia alichukua picha ambayo walipiga pamoja na kuichora alama ya X kwa kutumia marker pen” alisema shuhuda mmoja.
Jeshi la polisi linamshikilia John Ogolla kuhusiana na tukio mara baada ya upelelezi kukamilika atapandishwa kizimbani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate