EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 9, 2012

Wafuasi wa Ponda waachiwa kwa dhamana.

Katibu wa Kamati ya kutetea haki za Waislamu,Sheikh Ponda Issa Ponda(katikati) na wenzake 49 wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu aliposomewa mashtaka ya uchochezi na kuvamia kiwanja kilichouzwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania(Bakwata) jijini Dar es salaam.
HATIMAYE washtakiwa wote katika kesi ya wizi na uchochezi inayomkabili Katibu  wa Jumuiya na Taasisi za  Kiislam  Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda wameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Wakati washtakiwa hao wakipewa dhamana, Sheikh Ponda ameendelea kubakia mahabusu kutokana na dhamana yake kufungwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP). Dhamana kwa washtakiwa hao ilitolewa baada ya wote kutimiza masharti .
Miongoni mwa masharti hayo, ni kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wanaotambulika, wenye vitambulisho na wote kusaini bondi ya dhamana ya Sh1 milioni.
Sambamba na masharti hayo, mahakama iliwapiga marufuku washtakiwa hao kwenda eneo la mgogoro uliowasababishia kesi hiyo (Markazi Chang’ombe) hadi kesi itakapokwisha.
Washtakiwa waliofikishwa mahakamani jana na kuachiwa kwa dhamana ni 30, ambao waliungana na wenzao 19 ambao walikuwa tayari wamepata dhamana kwa nyakati tofauti, baada kutimiza masharti hayo.
Sheikh Ponda na wenzake 49 walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Oktoba 18, mwaka huu chini ya ulinzi mkali na kusomewa mashtaka matano yakiwamo wizi na uchochezi.
Tuhuma zingine ni kula njama, kuingia kwa nguvu eneo lisilo mali yake kwa nia ya kutenda kosa, kujimilikisha ardhi kwa nguvu na kusababisha uvunjifu wa amani.
Mashtaka manne yanawahusu washtakiwa wote 50 isipokuwwa shtaka moja la uchochezi, ambalo linamhusu Sheikh Ponda pekee anadaiwa kuwashawishi  wafuasi wake kutenda makosa ya uhalifu.
Wakati kesi hiy ilipotajwa mahakamani hapo Novemba Mosi, mahakama ilikubali kuwapa dhamana washtakiwa wote isipokuwa Sheikh Ponda ambaye mahakama ilisema haina mamlaka ya kisheria kwa kuwa DPP aliwasilisha hati ya kuzuia dhamana yake.
Siku hiyo Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi (SSA), Tumaini Kweka alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Hivyo, Kwaka aliomba mahakama ipange tarehe ya usikilizaji wa awali (PH), washtakiwa hao watasomewa maelezo ya awali ya kesi inayowakabili na kutakiwa kubainisha mambo wanayokubaliana na wasiyokubaliana nayo.
Hata hivyo, Wakili wa washtakiwa hao, Juma Nassoro alikumbusha mahakama kuhusu dhamana ya washtakiwa hao, akidai kuwa wakati walipopandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza, maombi yao ya dhamana hayakushughulikiwa kwa kuwa hakimu aliyepangwa kusikiliza kesi hiyo hakuwapo.
Hakimu Nongwa alikubaliana na maombi hayo ya dhamana na kusema dhamana iko wazi kwa washtakiwa wote, isipokuwa Sheikh Ponda ambaye dhamana yake imefungwa na DPP.(CHANZO HABARI NI MWANANCHI )


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate