EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 30, 2013

Ikulu yatakiwa kufafanua kuhusu MwanaHalisi

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRD), umedai kupokea kwa mshangao taarifa zilizoandikwa na gazeti la serikali zikisema kuwa Rais Jakaya Kikwete amelizika rasmi gazeti la MwanaHalisi kwa uchochezi.
 
Kwamba habari hiyo imeupotosha umma kwa kiwango kikubwa, na hivyo wanaitaka 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu kutoa ufafanuzi, kutokana na kupotoshwa kwa kosa lililosababisha gazeti hilo kufungiwa.

Mtandao huo ambao ni mkusanyiko wa mashirika zaidi ya 60 ya watetezi wa haki za binadamu wakiwamo wanasheria, waandishi na watetezi wengine, ulisema kuwa habari hizo ni za upotoshaji kwa sababu zinamkariri Rais Kikwete akiwa mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Kwamba habari iliyochapishwa na gazeti hilo la HabariLeo ilidai kuwa MwanaHalisi lilifungiwa kwa sababu liliandika habari ya uchochezi ikiwataka askari kuasi na kutotii amri.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mratibu wa Mtandao huo, Onesmo Olengurumwa alisema kuwa habari hiyo haikuandikwa na gazeti la MwanaHalisi bali gazeti jingine ambapo tayari watuhumiwa wamefikishwa mahakamani.

“Tunaamini kilichoandikwa na mwandishi wa gazeti hilo ndiyo kauli iliyotolewa na Rais Kikwete kwa sababu habari hiyo imeletwa na mhariri mzoefu na makini, na tunaamini hivyo kwa sababu rais ameitoa kauli hiyo mahali pake, wakati akiwasilisha ripoti ya Tathmini ya Utawala Bora (APRM),” alisema.

Aliongeza kuwa, wanashawishika kuamini kwamba iwapo siku zote Rais Kikwete alikuwa akiamini kuwa MwanaHalisi ndiyo waliochapisha habari inayohusu askari kugoma, basi alipotoshwa tangu mwanzo na hivyo anahitaji kuelimishwa vizuri juu ya suala hilo.
Alisisitiza kuwa, wanaendelea kuamini kuwa MwanaHalisi lilionewa kama sababu zilizosababishwa kufungiwa ni pamoja na zile ambazo gazeti hilo lilimnukuu Rais Kikwete huko Ethiopia.
Katika habari hiyo, Rais Kikwete alikaririwa akisema “...Ndio kuna gazeti moja tumelifungia na kuna watu wanaosema tuliondolee adhabu…tumesema hapana…kutaka Jeshi liasi huu sio uandishi wa habari.”

MwanaHalisi lilifungiwa na serikali Julai 30 mwaka jana, kutokana na habari yake iliyomhusisha ofisa wa Ikulu katika sakata la kutekwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, kudaiwa kuwa ni ya uchochezi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Hali Halisi Publishers (HHPL) inayochapisha MwanaHalisi, Saed Kubenea, alipoulizwa juu ya kauli ya rais, alisema ameipokea kwa faraja.
“Tuna taarifa za serikali kukamata na kushitaki mwandishi aliyeandika habari ambazo serikali ilisema zinachochea uasi katika majeshi; mhariri wa gazeti lililozichapisha na mwenye mtambo uliochapa gazeti. Lakini hayo yote hayahusu MwanaHalisi,” alisema.
Alisema kuwa kwake si gazeti wala waandishi wa habari wanaotuhumiwa uchochezi wa jeshi. Lakini kama walifungiwa kwa madai hayo, basi sasa rais ameibuka na ukweli ambao utawaweka huru.
                                           CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate